Está en la página 1de 20

www.annuurpapers.co.tz au facebook:annuurpapers@yahoo.

com

AHLU SUNNA WAL JAMAA HAJJ AND UMRA TRUST

Sauti ya Waislamu

ISSN 0856 - 3861 Na. 1180 SHAABAN 1436, IJUMAA , JUNI 5-11, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=

(12) KIJANA WA KIISLAMU, UMESHAHIJI?


Mtume(saw) ameagiza, Fanyeni haraka kwenda
kuhiji. Tunahimizwa tuende kuhijji tungali vijana
ili tupate maisha bora yenye kudhaminiwa na
Allah. Ni makosa kuakhirisha kwenda kuhiji.
Masahaba walikuwa wanashindana kwa wingi wa
Hijja. Muda unakwisha! Gharama zote kwa Hijja
ni Dola 4,500. Umra ya Ramadhani ni Dola 2,300.
Karibuni Ahlu Sunna Wal Jamaa kwa huduma nzuri
na uongozi bora. Wasiliana nasi: Tanzania Bara:
0765462022;0782804480; 0717224437.
Zanzibar:0777468018;0777458075;0777845010.

Tuhuma za ugaidi:

Takbir zarindima Mahakamani


Polisi wataka kutembeza virungu
Hakimu awazuiya kuepusha balaa
Ni baada ya Sheikh Hussein kuachiwa

JAJI Mstaafu Joseph Warioba (kushoto) akiwa na Waziri Mkuu mstaafu Dkt. Salim
Ahmed Salim.

SHEIKH Msellem Ali.

SHEIKH Farid Hadd

MHE. Mansour Himid.

MHE. Othman Masoud.

Masheikh Uamsho wambana Pinda

Wajiweka kapu moja na Mzee Moyo, Warioba


Wasema Kosa lao sawa la Mansour, Othman
Ila wao waliwahi tu kumfunga paka kengele
Uk. 3

Wahitimu Segerea wahoji


unga unaingiaje gerezani
WAZIRI mstaafu wa SMZ, Mzee Nassor Moyo.

Wadai bangi, madawa, yamekithiri


Serikali yatakiwa kuchukua hatua

Uk. 3

Tahariri/Habari

2
AN-NUUR

S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786


Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.
www.annuurpapers.co.tz
E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top
Usangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam

Wapiganaji Jihadi wanaotumikia


ubeberu: Hii inakuwaje?
MWANDISHI wa Kifaransa
Thierry Meyssan katika
makala yake Jihadists in
the Service of Imperialism
anasema kuwa hivi sasa nchi
za Magharibi hazifanyi tena
kuwa ni jambo la siri juu
ya namna wanavyowatumia
Wa i s l a m u w a p i g a n i a
Jihad, kufikia malengo
yao ya kibeberu.
Waliwatumia Libya, kama
f o o t s o l d i e r s k u m t o a
madarakani na hatimaye
kumuuwa Muammar elGaddafi. Wakati huo huo
katika vita ya Syria, Israel
iliondoa majeshi ya Umoja
wa Mataifa katika milima
ya Golan na kuwabadilisha
na wapiganaji wa Kiislamu
waliojipa jina al-Nusra ili
kuwapa wepesi Al- Nusra,
kwa mori wao wa kijihad,
wapambane na Bashar alAssad.
Thierry Meyssan, anasema,
wakati ni rahisi sana kufahamu
na kuelewa maslahi ya nchi
za NATO katika kuwatumia
Wapigana Jihad feki, kwa
hakika inakuwa ni vigumu
sana kubainisha ni vipi na
kwa jinsi gani wapiganaji
jihadi wanaweza kumtumikia
Uncle Sam kwa jina la Qurani
na wala wasijitambue kuwa
wanatumiwa.
Katika uchambuzi wake
Thierry Meyssan, anasema
kuwa katika mambo ambayo
ni ya kujivunia na kwa hakika
kuonyesha umahiri wake
katika kutekeleza majukumu
yake kwa nchi na watu wa
Marekani, ni jinsi Pentagon
(Makao Makuu ya Jeshi la
Marekani) na CIA (Shirika
Kuu la Ujasusi Marekani)
zinavyofaulu kuwarubuni
mamilioni ya Waislamu na
kuwapeleka kupigana kwa
maslahi ya Uncle Sam.
Katika kueleza hilo
anasema kuwa ni wazi kuwa
viongozi wa mujahidina
hao watakuwa ni mamluki.
Ila linalosikitisha na la
kuwaonea huruma, ni hao
wapiganaji jihadi ambao
watakuwa wanaamini kuwa
wanapigana na kufa ili kupata
njia ya kufika Paradiso.
Wamefikishwaje hapo?
Imekuwaje wakapumbaa
kiasi hicho? Hilo ndio swali
la msingi anajiuliza Thierry
Meyssan.
The answer is childishly
simple using the rhetoric of the
Muslim Brotherhood as a start,
its possible to evade human
reality and send them to kill
anyone you like as long as you

wave a red flag at them.


Katika kujibu swali hilo,
muuliza swali anasema kuwa
ni jambo la kushangaza pia
kwamba hata jibu la swali ni
la kitoto mno. Ila linahitaji
mtu mwenye kutafakari.
Anachosema ni kuwa watu
hao huwa wanachezewa akili
kitoto sana. Kinachofanyika
ni kucheza na saikolojia zao
kuwa wanachopigania ni
dini-ukiwa wekea vibwagizo
mfano Quran ndio Katiba
yetu, Uislamu ndio ufumbuzi
na Jihad ndio njia. Ukipata
kiongozi wa kuwajaza
maneno hayo, wakamuamini
kuwa ni Amri wa Jihad,
anasema, unaweza kuwatuma
watu hao wakamuuwa mtu
yeyote, wakiamini kuwa hiyo
ni katika kupigania dini.
Katika kuzidi kulichambua
jambo hili, Thierry Meyssan,
anasema kuwa tatizo kubwa
ni kuwa watu huwa hawataki
k u k u b a l i k u wa M u n g u
aliwaumba akawapa akili na
wanatakiwa wazitumie akili
hizo. Watu wanayachukulia
maisha wanayoita ya uchamungu kuwa ni jambo jepesi
na halihitaji kutumia akili.
It doesnt really matter if
the Creator has made us all
intelligent, we must, in all
cases, apply the Word of God
like a machine. And when the
situation is not dealt with in the
Book, we should just smash it to
pieces. The result is obviously
catastrophic.
Kwamba watu wanadhani
ucha-mungu ni kufuata dini
na maagizo ya Mungu kama
mashine. Hakuna kutumia
akili. Na watu wakifikishwa
hapo, inakuwa ni balaa
kwa sababu imani ya kidini
inaweza kuwafanya watu
wakafanya mambo ya kutisha
bila kuogopa kwa sababu
wanadhani ni njia ya kwenda
Peponi. Hilo ndio tatizo la
msingi.
Imeandikwa sana jinsi
Waislamu walivyotumiwa
kwa jina la Jihad kupigana
n a M r u s i , wa l i c h o p a t a
hakuna. Ikaelezwa sana
walivyotumika kumpiga
Gadhafi, kilichopatikana kwa
Waislamu wala sio sifuri bali
Negative, kwa sababu nchi
imeingia katika machafuko
yasiyo na dalili ya kukoma
kwa masiku na miaka ya
karibuni. Lakini Waislamu hao
hao, bado wamo tu. Hivi sasa
wanapigana Syria na Iraq, bila
kujua kuwa wanachofanya ni
kufanikisha kile kilichoitwa
"A Strategy for Israel in the

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Nineteen Eighties". (Tazama:


The Zionist Plan for the
Middle East)
Anasema Thierry Meyssan,
kuwa, kwa bahati mbaya
baadhi ya Dola za Kiarabu,
zimekuwa zikitumika katika
kufanikisha mpango huu wa
Kizayuni na kibeberu, wakiwa
wa o wa n a c h o t i z a m a n i
masilahi yao kama watawala,
tena ya muda mfupi bila
kutizama athari mbaya za
kudumu watakazoziletea nchi
zao, Mashariki ya Kati na nchi
za Kiislamu kwa ujumla.
Na kwamba kwa sasa
kinachoitwa Dola ya Kiislamu
(IS) ya Abubakr al-Baghdadi,
hakuna itakacholeta chenye
manufaa na Uislamu bali ni
kuutia Uislamu katika himaya
ya giza. Ni kama alivyosema
Waziri wa Mambo ya Nje wa
Ufaransa Laurent Fabius,
mwaka 2012, kuwa, Katika

medani ya vita, (mujahidina)


wanafanya kazi nzuri!
(kuufanyia ubeberu)
Tumeyaeleza haya kwa
sababu tunaona kuna haja
k u b w a k w a Wa i s l a m u
kutafakari kwa kina
walikotoka, waliko hivi sasa
na wanakoelekea. Historia
inatuonyesha kuwa Waislamu
ndio walioutoa ulimwengu
katika kiza, wakaleta
ustaarabu. Ikafika mahali,
wakaporwa nafasi hiyo na
watu wengine. Wakawa wao
ni watu wa kufuata wengine.
I m e f i k a s a s a Wa i s l a m u
wanatumiwa na kuwa kama
kituko.
Limesemwa jambo hapa,
jambo la kutumia akili. Na
yote haya ni katika ule msingi
kuwa jambo la mwanzo
n i k u s o m a . Tu m e k u wa
tukichapisha makala
zinazoandikwa na ndugu

yetu Hamza Rijal akionyesha


namna watangulizi wetu
walivyotoa mchango mkubwa
katika taaluma mbalimbali
zinazotamba ulimwenguni
hivi sasa, wakati sisi tukibakia
kuimba kuwa ni za Wazungu
na wengine kufikia mahali
kuziita za kikafiri.
Yote hii ni kuonyesha kuwa
matumizi ya akili katika
wakati wetu huu, yamekuwa
madogo mno.
Kuna haja ya kujirudi
na kurejea katika Quran
tuone namna Mola wetu
alivyotuhimiza juu ya
kutumia Neema ya akili
aliyotupa.
Labda tujiulize, Allah
(SWT) anapotuuliza katika
Q u r a n : J e , h a m f i k i r i ?
Hamtambui? Hamna akili?
Hamzingatii? Anachokusudia
nini?

Na Mwandishi Wetu

mahakamani wimbo
wa DPP ni mmoja tu:
Mheshimiwa Hakimu, kesi
imeletwa hapa kutajwa
tu, mahakama yako haina
uwezo wa kusikiliza kesi
hii. Tunaomba kupangiwa
t a r e h e n ye n g i n e k wa
kutajwa tenani mwaka
nenda rudi gerezani
Segerea-Mahakama ya
Kisutu.
Imeongeza barua
h i y o n a k u d a i k u wa
wa m e b a m b i k i wa k e s i
ya ugaidi kutokana na
msimamo wao wa wazi
kudai mamlaka kamili ya
Zanzibar.
B a r u a i k a t a j a wa t u
wengine
ambao
yamewakuta kwa kuwa
na msimamo tofauti na
ule wa CCM wa mfumo
wa muungano wa serikali
mbili.
Katika kulifafanua hilo
b a r u a i m e s e m a k u wa
hata wazee na makada
wa chama kama Mzee
Hassan Nassor Moyo,
aliye Muasisi wa ASP na
muasisi wa CCM aliyebeba
kadi namba saba ya CCM,
amefukuzwa chama na
wajukuu wasioijua hata
hiyo historia ya CCM.
Pamoja na Mzee Moyo
wakasema kuwa ndiyo
sababu ya kufukuzwa
Waziri Mansour Yusuf
H i m i d n a a l i y e k u wa
Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar, Othman Masoud
kwa msimamo wao wa
kutetea Zanzibar ndani ya
muungano.
Tofauti iliyopo baina yao
Uamsho na waheshimiwa
h a o n i k u wa t u wa o
Masheikh wamepachikwa
tuhuma nzito za ugaidi.
Lakini wote yanawakuta
kwa kuweka wazi
msimamo wao juu ya
mfumo wa muungano
uliopo kuwa haufai.
Kwa upande mwingine
barua ikasema kuwa, hata
waheshimiwa sana huku
Bara walioweka msimamo

wao ulio tofauti na ule


unaotakiwa na watawala
wa CCM wa serikali mbili,
hawakusalimika.
Kama hilo halitoshi,
Mzee Mstaafu Jaji Warioba
amekashifiwa bungeni
na hata kudhalilishwa
hadharani katika midahalo
na mikutano kwa vile tu
Tume yake ilipendekeza
Mfumo wa Muungano,
ambao unaonyesha
kutotakiwa na CCM.
Mh. Waziri Mkuu, hao
wote wamesimamia dai la
serikali tatu, wamefikwa
na hayo,je, sisi viongozi
wa dini tuliodai mamlaka
k a m i l i h a t a k a b l a ya
Tume ya Mabadiliko ya
K a t i b a k wa m a a n a
hukosei kusema kuwa
viongozi wa Uamsho ndio
waliomfunga paka kengele,
h e b u t u j i u l i z e , i k i wa
Waasisi (wa Mapinduzi
na CCM) wamefukuzwa
chama, wastaafu
wa m e d h a l i l i s h wa , n a
wenye vyeo serikalini
wamepoteza vyeo vyao,
haishangazi serikali ya
CCM kutubambikia kesi
ya ugaidi sisi tuliomfunga
paka kengele.
Hata hivyo, pamoja
na kusema hayo
wa k a k u m b u s h a k u wa
kutoa maoni ni haki ya
kila raia na kila mwananchi
na wakasisitiza kuwa
hawataacha wala kurudi
nyuma.
M h . Wa z i r i M k u u ,
tunapenda serikali ya CCM
ifahamu kuwa kutoa maoni
ni haki yetu kikatiba na
hatutaacha wala hatutorudi
nyumatunaamini iko
siku kwa uwezo wa (Allah)
Muumba wa mbingu na
ardhi, ukweli utadhihirika
na uongo utajitenga, tena
karibuni Inshaallah.
Katika barua hiyo kwa
Wa z i r i M k u u ya M e i
23, 2015 Masheikha hao
wameelezea masikitiko
yao juu ya kauli ya Waziri
Inaendelea Uk. 4

Masheikh Uamsho wambana Pinda


MASHEIKH wa Uamsho
wamejiweka katika kapu
moja na Mzee Hassan
Nassor Moyo na Mansour
Himid wakisema kuwa
kosa lao ni sawa na la
wanasiasa hao wakongwe.
Wa m e s e m a , p a m o j a
n a o p i a n i a l i ye k u wa
Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Othman Masoud
kwa mantiki kwamba,
wote yanawakuta
kutokana na msimamo wao
unaopingana na ule wa
watawala ndani ya CCM.
Aidha, masheikh
hao wanaoshikiliwa
kwa tuhuma za ugaidi,
wameonyesha wasiwasi
wao juu ya kutekelezwa
kwa ahadi ya Waziri Mkuu
ya kushughulikia suala
lao, wakisema yasije kuwa
yale yale ya Mahakama ya
Kadhi.
Katika barua yao ya
wazi kwa Waziri Mkuu,
Masheikh hao wanasema
kuwa wataendelea
kuamini kuwa hawana
kesi ya kujibu na kwamba
mashitaka waliyopachikwa
ni mashitaka bandia
yaliyotokana na mambo
ya kisiasa.
Sisi tunaimani kuwa
si wahalifu, na tuna imani
kuwa Tanzania hakuna
ugaidi, na tunaamini kuwa
tumebambikiwa kosa kwa
lengo maalum kutumia
mgongo wa Mahakama
kutufunga muda watakao
kwa (hoja) kuwa kosa la
ugaidi halina dhamana.
Imesema sehemu ya
barua hiyo ya wazi kwa
Wa z i r i M k u u a m b a y o
imeonyesha kuandikwa
na aliyejitambulisha
kama Kiongozi Mkuu wa
Jumuiya ya Maimamu
Zanzibar.
Wa m e f a n i k i wa
kutufunga ndani, huu
mwaka sasa hakuna kesi
wala upelelezi uliokamilika
kila
tunapofika

Habari

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Wahitimu Segerea wahoji unga unaingiaje Gerezani

mahabusu ambao wengi


wao wamo humo kwa
makosa ya kubambikiwa,
SERIKALI imetakiwa ulevi au ya wizi mdogo
kudhibiti uingiaji wa mdogo.
Wamedai ukiingia humo
madawa ya kulevya katika
unashangaa
kukuta mtu
gereza la Segerea Jijini Dar
anatuhumiwa
kwa kesi
es Salaam, ili kunusuru
ya
simu,
kesi
ya
kuku na
hali ya wafungwa na
Mahabusu wanaoingia wengine pesa, pengine
haifiki hata milioni,
gerezani humo.
Ushauri huo, umetolewa tuhuma ambazo zinaweza
na baadhi ya wafungwa kumweka mwaka mzima,
na mahabusu walioingi na akiwa mahabusu sababu
kutoka katika gereza hilo unaambiwa upelelezi hauja
na kushuhudia kukithiri kamilika.
Sidhani kama watendaji
kwa uingiaji na utumiaji wa
(Polisi) wanakuwa makini
madawa hayo.
Wakiongea na An nuur n a k a z i z a o , s i d h a n i
kwa masharti ya kutotajwa tuhuma kama hizo ndogo
m a j i n a y a o g a z e t i n i , ndogo zinaweza kuchukua
w a m e s e m a k u t o k a n a zaidi ya muda wa masaa
na hali hiyo, inapelekea 24, katika upelelezi na
miongoni mwa wafungwa kubaini tatizo. Amesema
na watuhumiwa gerezani m f u n g w a m w i n g i n e
humo kufanya matendo aliyemaliza muda wake.
Wakielezea namna gani
machafu.
madawa
hayo yanavyo
Hata hivyo, An nuur,
ingia
kutokana
na uzoefu
ilipowasiliana na Mkuu
wa Gereza hilo maarufu wao kwa muda waliokaa
Jijini Dar es Salam, Kiyangi gerezani humo, wamesema
A b d a l l a h , i l i k u p a t a bila shaka madawa hayo
ufafanunuzi wa hali hiyo, yanaingizwa na baadhi ya
alisema kwamba yupo
katika mkutano.
Wa k i o n g e a k wa
masikitiko wafungwa hao
wahitimu wa Segerea,
wa m e d a i k u wa wa p o Na Bakari Mwakangwale
wanaoingia gerezani humo
wakiwa hawatumii kilevi K I V U M O c h a Ta k b i r ,
chochote wala hawana k i l i r i n d i m a n d a n i y a
tabia chafu, lakini hujikuta M a h a k a m a K u u M j i n i
wakiingia katika mitihani Mtwara, baada ya Sheikh
hiyo kutokana na hali H u s s e i n M c h o m o l o
huru.
ngumu wanayokutana kuachiwa
Sheikh Mchomolo pamoja
nayo gerezani humo.
na Waislamu wengine watano,
Imeelezwa kuwa vilevi k w a p a m o j a w a l i k u w a
vilivyokithiri gerezani wakituhumiwa kujihusisha
humo ni unga, bangi, na ugaidi.
sigara pamoja na ugoro,
Takbira hizo ndani ya
n a k wa m b a h a l i h i y o Mahakama ziliwapelekea
m a g e r e z a n i h a i t o k u j a polisi waliokuwepo kutaka
kuisha mpaka pale Serikali k u w a c h u k u l i a h a t u a
itakapoamua kulipa uzito Waislamu, hata hivyo Hakimu
akaingilia kati.
suala hili.
Katika kutoa hukumu
Wanaoathirika zaidi ya kesi hiyo iliyovuta hisia
ni vijana na hili wazazi za wakazi wengi mkoani
wa n a t a k i wa wa e l e w e humo, hususani Waislamu,
kwamba, watoto wengi Hakimu aliyehukumu kesi
ambao wapo gerezani hiyo alisema Mahakama
wamesha haribika, wengine hiyo haijapata ushahidi wa
wa n a i n g i a h a wa f a n y i kutosha wa kuwatia hatiani
m a m b o m a c h a f u a u watuhumiwa.
Kauli hiyo ya hakimu,
hawatumii kilevi chochote
ilisababisha umma wa
l a k i n i k u t o k a n a n a ndiyo
Kiislamu uliofurika ndani
makundi ya mle ndani na na nje ya Mahakama hiyo,
kukithiri kwa madawa kuzizima kwa kivumo cha
hayo, yanamsukuma kijana Takbir, Allah Akbar.
kuingia katika mambo
Hata hivyo, kutokana na
hayo. Alisema mmoja wa sheria kutoruhusu kuongea
wafungwa hao aliyemaliza M a h a k a m a n i m b e l e y a
muda wake katika gereza Hakimu, Polisi alimfuata
Muislamu aliyepiga Takbir
hilo.
Katika maelezo yao, kwa lengo la kumchukulia
atua, lakini Hakimu
wamesema kwamba hali h
alimzuia.
hiyo inasababishwa na
Taarifa zinasema kuwa
mrundikano mkubwa wa baada ya Hakimu kumzuia
Na Bakari Mwakangwale

Askari magereza walikosa


uadilifu kwa Taifa lao.
Walipoulizwa ni kwa nini
wanawadhania watumishi
hao wa Jeshila la Magereza,
walisema uwezekano huo
ni mkubwa kufanywa na
Maafande, kutokana na
upekuzi mkali unaofanywa
kwa watuhumiwa
na wafungwa kabla ya
kuingizwa gerezani humo.
Wameeleza kwamba
k a m a k u n g e k u wa n a
utaratibu wa kuwasachi
pia askari Magereza
wanaoingia katika zamu
kama wanavyosachiwa
watuhumiwa na wafungwa,
hawadhani kama madawa
hayo yangeingia gerezani.
Serikali yetu ingetilia
mkazo kwa Maaskari wake
katika kudhibiti hali hii
kwa majaribio ya miezi
kadhaa tu kwa kuwasachi,
badala ya kuwakazania
watuhumiwa peke yao,
kisha waangalie kwamba
u i n g i z a j i wa m a d a wa
hayo unaongezeka au
unapungua. Wameshauri.
Wakielezea ugumu kwa

wafungwa na mahabusu
kuingia au kuingiza
madawa hayo, wamesema
hawajui kama ni utaratibu
au ni sheria kuwa kila
anayepelekwa gerezani, ni
lazima apekuliwe akiwa
amevuliwa nguo.
Wameeleza kuwa wakati
mwingine ukifikishwa
gerezani, katika ukaguzi
wao unalazimishwa
utoe haja kubwa lengo
ni kujirizisha kuwa
mtuhumiwa hana dawa
z a k u l e v ya , n a k a m a
huna utaletewa chakula
ule ili mradi utoe haja
wahakikishe huna kitu
ndipo uingie gerezani.
Aidha, wameeleza kuwa
kitendo cha kuvuliwa
nguo, kurushwa kichura
u c h i wa m n ya m a n a
kupekuliwa sehemu za haja
kubwa, ni suala la kawaida
unapopokelewa Segerea,
wakahoji katika hali kama
hiyo mtuhumiwa huyu
ataingizaje vilevi hivyo.
Kwa kweli ni
udhalilishaji mkubwa na
mateso makubwa, lakini

yote hayo wanadai ni


kuzuia kuingia na vitu
kama hivyo na vingine vya
hatari.
Sasa cha ajabu ukitoka
katika upekuzi huo
ukaingia ndani unakuta
watu wanatumia,
unajiuliza haya madawa
yanaingiaje humo
gerezani. Wameeleza.
Wa m e s e m a k u w a
unapokuwa humo
gerezani, ndipo utakapo
pata jibu kuwa madawa
hayo yanaingiaje, kwa
maana nyingine ni
kwamba miongoni mwa
hao maaskari walio katika
ngome ya Segerea, ndio
wenye biashara ya madawa
ya kulevya, sigara, ugoro
na hata bangi.
Wamedai kuwa kuna
u s i r i m k u b wa k a t i k a
kufanya biashara hiyo,
kwani hata Maafande hao
hawajuani kwa sababu
kila mmoja anafanya kwa
siri kubwa, pamoja na hali
hiyo hawadhani kwamba
kama Serikali ikiamua
itashindwa kumaliza tatizo
hilo.

wa amani iliyopo nchini na


Ulimwenguni hasa kutokanan
na kuwepo tishio la ugaidi,
Mahakama imemuamuru
kuripoti kwa R.C.O, kwa
muda wa mwaka mmoja kila
ifikapo mwisho wa mwezi.
Alisema hesabu hiyo
imeanza Machi 5, 2015, siku
aliyopata dhamana baada ya
kukamatwa na Polisi, lakini
pia Mahakama imemtaka
k u wa r a i a m we m a k wa
kipindi chote na asijihusishe
na mambo yanayo ashiria
uvunjifu wa amani.
Pia wamenitaka kuwa
mtu wa kuhamasisha amani ili
nchi iwe salama, lakini kabla
ya kumaliza hukumu, hakimu
alinitaka niongee kama nina
lolote la kuongea mbele ya
Mahakama. Alisema Sheikh
huyo.
Alisema baada ya kupata
f u r s a h i y o k u t o k a k wa
Hakimu, aliuliza swali akitaka
kujua ni ipi hali ya ugaidi
nchini.
Hakimu alijibu kuwa ni
kutoa mawaidha makali
yanayoashiria ushawishi kwa
jamii.
Alipojibiwa alihoji
tena, endapo atawaambia
Waislamu kwamba, Waislamu
wenzetu wanazidi kushikwa
na wanateswa sana huko
mahabusu, hivyo Serikali
inafanya dhulma kwa
Waislamu, atakuwa amefanya
ugaidi?
A l i j i b i wa n a H a k i m u
kwamba, kama hilo

analosema ni sahihi itakuwa


si kufanya ugaidi na kama
anafanya hamasa ili watu
waichukie Serikali, basi
itakuwa anafanya ugaidi.
Alisema maelezo ya
Hakimu huyo na hukumu
ya kesi yake ni wazi imetoa
picha halisi na uhalisia wa
tuhuma za kesi za Waislamu
kuhusu ugaidi, kwamba hizo
ni tuhuma za kusingiziwa tu
ili kuwatia dosari Waislamu
na Uislamu.
Sheikh Mchomolo,
aliwashukuru Waislamu
kwa duwa zao, hususani
Wa i s l a m u wa m k o a wa
Mtwara na miji yake ambao
walikuwa wakijitokeza kwa
wingi kila inaposikilizwa
kesi yake kwa muda wote
aliokuwa anakabiliwa na kesi
hiyo.
Hata hivyo alisema lililo
muhimu kwa Waislamu ni
kutoacha kupinga dhulma
dhidi yao na kupigania dini
yao kwa kuhofia adhabu za
duniani, kwani adhabu ya
Allah (s.w) ni kubwa kuliko
chochote.
Sheikh Hussein Mchomolo,
alikamatwa na Polisi Februari
2 mwaka 2015 na kukaa
rumande kwa muda wa mwezi
mmoja, kabla ya kukubaliwa
dhamana ambapo alitoka
rumande Machi 5, 2015.
Sheikh huyo ni miongoni
mwa Waislamu waliokumbwa
na kamata kamata ya Jeshi
l a P o l i s i , a k i t u h u m i wa
na Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kuwa
anajihusisha na masuala ya
kigaidi nchini.

Takbir zarindima Mahakamani


polisi kuchukua hatua
aliyokusudia dhidi ya
Muislamu huyo, alieleza
k wa m b a k i v u m o h i c h o
kilitarajiwa kutokea kutokana
na hali ya kesi hiyo kuwa ni
ya dini.
Hivyo aliamuru Muislamu
huyo aachwe na wala
asibughudhiwe.
Maneno aliyoyasema
hakimu yalinitia ujasiri
mkubwa na kwa mara ya
kwanza Waislamu wamepiga
Takbir wakiwa Mahakamani,
alisema Sheikh Mchomolo.
Katika hukumu hiyo
iliyochukua saa tatu na
dakika arobaini kusomwa,
Sheikh Mchomolo alionyesha
alimtaka Hakimu amueleze ni
ipi hali ya ugaidi nchini.
Awali akiongea na Annuur kwa njia ya simu muda
mfupi mara baada ya hukumu
hiyo, Ust. Mchomolo, alisema
M a h a k a m a i m e s h i n d wa
kumtia hatiani kutokana na
kukosa ushahidi wa kumtia
hatiani.
Maamuzi ya kesi yangu
hapa leo (Alhamisi iliyopita)
ni kuwa, Mahakama
imeshindwa kunitia hatiani
kwa sababu haikupata
ushahidi wa kutosha kufanya
hivyo, kwa hiyo nimeachiwa
huru lakini kwa masharti
m a a l u m k wa m u d a wa
mwaka mmoja. Alisema
Sheikh Mchomolo.
Alisema katika maelezo
yake, Hakim alieleza kuwa
kutokana na hali ya uvunjifu

Makala
Na Mussa Ame

MADA hii ya sheria


za Kiislamu kuhusu
kumkufurisha mtu, ni
muhimu sana wakati huu
ambao makundi mbali
mbali yenye fikra zilizokuwa
tofauti na sheria yameibuka,
kiasi kwamba kuna wasiwasi
kuwa huenda vikundi hivi
vinavyoibuka kukufurisha
watu ama vinaundwa na
maadui wa Uislamu au
vinasaidiwa na wao. Kwani
akitokea Muislamu kufanya
kazi ya kafiri, basi kafir yeye
hupumzika.
Huko Nigeria waliyaachia
makundi yenye fikra
potofu na walifikiria kuwa
hayawezi kupata wafuasi,
matokeo yake vijana kadhaa
wakajiunga na Boko Haram
na kusababisha vifo vya
Waislamu kwa mamia kama
si amelfu. Walianza na fikra
potofu kuwa elimu ya shule
ni haramu, na wanaosoma
wanakuwa makafiri. Ndio
maana juhudi kubwa ya
Boko haharamu ni kuwaua
Waislamu wenzao badala ya
kuwalingania makafiri.
Fikra hii pia inafatwa
na baadhi ya vikundi
vinavyojitokeza siku hizi
ambavyo vina kasoro kubwa
katika itikadi zao, na ikiwa
hawakuelimishwa, wanaweza
wakageuka kuwa kirusi
kibaya (virus) kama Boko
Haram. Katika baadhi ya
nchi watu hawa wenye fikra
potofu hujitenga mwituni
kwani wanaamini kuwa
nchi hizi ni Daru kufru na
ili awe salama Muislamu
ahamie mwituni. Huamini
kwamba Waislamu wenzao
wamekufuru na ni makafiri
wa n a o s t a h i k i k u u wa wa
ndiyo maana usishangae
ukamkuta mwanafunzi wa
kike anayesomea udaktari
anaacha chuo, kwa kuamini
kuwa kusoma elimu ya shule
ni ukafiri na waliosoma elimu
hii wamekufuru.
Watu hawa wanakosa
kuelewa kuwa hiyo elimu ya
sayansi ilianzishwa na Salafu
wema. Wazungu walikuja
kuipata baada ya kutekwa
Spain. Ndiyo maana mpaka
leo kuna athari ya Uislamu
kwenye sayansi. Algorithim
ni fani aliyoianzisha Al
khawarism. Neno alkali ni
neon la Kiarabu. Algebra ni Al
Jabir wote hao ni Maulamaa
wa Kiislamu waliotokana na
Salafi Wema.
Mada hii itaendeleza
kufafanua kuhusu ukafiri ,
kwa sababu makundi mengi
yanayoibuka hivi sasa yenye
itikadi kinyume na itikadi
za Ahli sunaa, yanafanana
katika suala moja tu: Namna
wanavyokufurisha wenzao,
na kutumia muda mwingi
kwa ubishi na mijadala isiyo
na manufaa. Na kuanza kazi
ya hukumu wala Kiyama
bado. Wakamtia ukafirini na
motoni kila anayewakosoa.
Dini yao wao, ni
k u wa s e n g e n ya we n z a o ,
kuwadharau na kuwakejeli.

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Misingi ya Ahli Sunaa katika


kumtia mtu kwenye ukafiri

ni makafiri! Mbona Mtume


(SAW) alimlingania ami yake
Abi Talib aliyekuwa kafiri,
mpaka anakata roho anampa
d a a w a . M t u m e ( S AW )
alimlingania Abuu Jahli zaid
ya mara mia tena kwa upole
na huruma. Nabii Musa (AS)
alimwendea Firauni kwa
lugha laini kumlingania. Sasa
kinachohitajika ni daawa
ienezwe.
Kuna sehemu huko
mikoani hali inatisha sana.
Uislamu haujulikani kabisa.
Daawa haijafika. Sasa, tuache
malumbano ya kujadili kama
Saidi Qutub ni kafir au laa.

Sisi hatutaulizwa kuhusu


hao, tutaulizwa kuhusu hawa
makafiri wa sasa wanaokosa
daawa. Tutaulizwa kuhusu
Waislamu waliokosa elimu
ya a q i d a wa k a t i we t u .
Tutaulizwa kuhusu wazee
wetu ambao wamezaliwa
katika mazingira ya
kutambika, kufanya uchawi,
kuacha sala, kuzini ,kulewa
na kufanya maasi. Sasa kabla
hatujawahukumu, kuwa ni
makafiri, basi tuwalinganie
kwanza.
K u n a f i k r a ya S a l a f i
k u h u s u k u wa t e n g a n a
kutowasemesha watu wa
bidaa. Kuhusu hili unahitaji
kutumia kidogo tu akili
yako na kutizama historia.
Kwamba Mtume (SAW)
aliamrisha kutosemeshwa
kwa kina Kaab bni Malik
(RA) wakati Madina ilikuwa
dola ya Kiislamu yenye
kuongozwa na sheria za
Kiislamu na wale Masahaba
walifanya kosa hili baada
ya kuwa na elimu juu ya
kosa lenyewe na kuwawekea
vikwazo kulileta faida ya
kuwarekebisha. Hivi leo
usipowasemesha Waislamu
wenzako kwa kufanya kosa
lile lile la Kaab, jee faid gani
itapatikana. Kwanza hao
waovu ndiyo wengi katika
jamii, wanaosali ni wachache
tena hii si dola ya Kiislamu ni
nchi tu ya kijahili. Sasa wakati
kama huo wa kijahili Mtume
(SAW) hakumtenga mtu
wala kumuwekea vikwazo.
Alikuwa akipiga daawa.
Daawa kwanza kuwaadhibu
waovu baadaye. Ukipata
mamlaka. Kila kitu kina
wakati wake. Huwezi kuvuna
mpunga kabla kuupanda
ukaupalilia .
Sasa tusome dini na
tutumie akili zetu. Ndivyo
Mtume (SAW) alivyokuwa
akiwaambia Maswahaba
a l i p o wa p e l e k a s e h e m u
mbalimbali.
Wabillahi tawfiiq

Inatoka Uk. 2
wa Mambo ya Ndani
Mheshimiwa Mat hias
Chikawe juu ya malalako
yao.
Wamesema kuwa kauli
ya Waziri Chikawe kuwa
mtuhumiwa aliyelalamika
k u d h a l i l i s h w a
achunguzwe isije ikawa
kafanyiwa mambo
ambayo ni mchezo
wake aliozoeya ni ya
kumdhalilisha mlalamikaji
na isiyotarajiwa kutoka
kwa kiongozi mstaarabu
wa serikali.
K wa l ug ha nye p e s i
tu, barua hiyo imemtaka
Mheshimiwa Chikawe
kupima kauli yake kwa
kujiuliza kama angeweza
kutoa kauli kama
hiyo iwapo ingekuwa
malalamikaji ni mtu
anayemuhusu.
Kwa kumalizia barua
hiyo imekariri madai ya

Masheikh hao kwamba


wanataka walioumizwa
wachunguzwe afya zao na
kupatiwa matibabu.
Na pili wakashitakiwe
Zanzibar kwa sababu hata
kule kuna Mahakama Kuu
na ndiko inakodaiwa kosa
kufanyika.
Sisi Wazanzibari dai
letu turejeshwe nchini
kwetu Zanzibar. Zanzibar
tuna Mahakama Kuu
kongwe kuliko ya Bara.
Tuna Gereza Kuu, Tuna
Rais, tuna DPP, tushitakiwe
Mahakama Kuu Zanzibar,
sio Kisutu wala Mahakama
Kuu Tanganyika (Tanzania
Bara) iliyovaa koti la
muungano. Hatuna imani
nayo.
Imehitimisha barua hiyo
ya wazi kwa Waziri Mkuu
ambayo gazeti hili imepata
nakala yake.

WANAWAKE wa Nigeria walipoandamana kupinga vitendo vya Boko Haram.


Na hilo ni kosa kubwa
kisheria. Maulamaa wa
Kisalafi wamekuwa mstari
wa mbele kupinga watu
kuitwa makafiri kiholela bila
ya hoja za wazi.
Ibnu Taymiya anasema,
Mimi nimekuwa mbele
kupinga watu kuitwa
makafiri au wanafiki bila ya
ushahidi wa Hadithi sahihi
ya Mtume(SAW) yenye
kuthibiisha ukafiri huo.
(Majmoo fatawa 3/229).
Imam Naway anasema,
ukafiri ni kujitoa kwenye
Uislamu na hii hutokea
kwa maneno ya kikafiri au
vitendo vya kikafiri vya
wazi na kwamba afanya
mtu kwa makusudi, bila
ya kulazimishwa, kama
akasujudia masanamu au jua
au akajiingiza katika uchawi
unaohusiana na kuabudu
jua au kuabudu viumbe.
(Rawdha Talibyn-7/283-284).
Fatwa ya Maulamaa wa
Kisalafi wa Saudi Arabia
kuhusiana na ukafiri wa mtu
asiye na elimu na akawa
anakejeli dini, na akawa
anaabudu makaburi kwa
kwenda kuomba maiti
makaburini. Kamati hii amiri
wake alikuwa ni Ibnu Baaz
(Allah amrehemu).
Kuifanyia mzaha na
kukejeli dini, kama kuikejeli
Qurani au sunna, ni ukafiri
ikiwa unatokana na mtu
mwenye akili timamu
mtu mzima, italazimika
kuambiwa kuwa huu
ni ukafiri ili atubu, lakini
kama ataendelea baada ya
kuelimishwa, basi atakuwa
kafiri, kwa mujibu wa Suratu
Tawba, (9:65-66)
Kuabudu makaburi na
kuabudu miungu kinyume

na Allah (SW), ni ukafiri


mtu anayefanya haya
Lazima kwanza aambiwe na
aelezewe hukma ya masuala
hayo, kama akakubali sawa,
akikataa atakuwa mshirikina
na akifa atakufa katika shirki
na ataishi milele motoni
(Kamati ya kudumu ya
utafiti na fatwa mjeledi wa
pili-Aqida uk 13-14 , pia
fatwa no 5213 ya 15/1/1404H)
Kutokana na fatwa hizo
za hao Masalafi, ni dhahir
kwamba vijana wetu wana
m a k o s a ya k u u f a h a m u
msimamo wa Salafi, na
labda hukosea kuchukua
misimamo ya pahala fulani
wakaileta kwengine bila
ya kuchunguza tofauti ya
mazingira. Mfano mzuri
ni ule msimamo wao wa
kuwaona wanaoomba
makaburini huku Tanzania
ni sawa na wale wa Saudia.
Kule Saudia wameeleweshwa
na wakakatazwa sasa
a n a ye s h i k i l i a k u a b u d u
kaburi kwa kuliomba huwa
kafiri. Lakini huku kwetu
tumezaliwa katika bidaa na
kuomba makaburini , sasa
kinachotakiwa cha kwanza ni
kuwaelimisha watu hawa (sio
kuanza kuwatukana wakati
wanafanya kwa kutokujua),
kuwaeleza ubaya wa bidaa
zao, na kuwafahamisha kuwa
kuabudu makaburi ni shirki,
na haya yanahitaji upole na
hikma siyo kutukana watu
tu. Huo si Uislamu.
Na pia ni makosa kusema
kuwa hutaki kuwasemesha
watu wa bidaa, na wakati
mwengine hao ni wazee wako.
Sasa ndiyo maana vijana
hawa hufanya mambo mengi
bila ya ruhusa ya wazee wao
eti kwa sababu wanawaona

Masheikh Uamsho wambana Pinda

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Somalia yatimiza miaka 20 ya vita tangu kuangushwa Siad Barre


Na Shaaban Rajab
SOMALIA ambayo
ilijulikana kama Jamhuri ya
Demokrasia ya Somalia, ni
nchi iliyopo katika pwani ya
Afrika ya Mashariki katika
Pembe ya Afrika. Kijiografia,
imezungukwa upande
wa Kaskazini-Mashariki
na Ethiopia na Djibouti
na upande wa magharibi
imepakana na Kenya.
Mashariki kuna Ghuba ya
Aden.
Somalia ilikuwa koloni la
Italia tangu miaka ya 1888
hadi mwaka1960 ambao ndio
mwaka nchi hiyo ilipopata
uhuru. Kuanzia mwaka
1888 Italia ilijipatia nchi ya
Somalia kupitia mikataba ya
ulinzi dhidi ya Masultani
m b a l i m b a l i wa l i o k u wa
wakitawala maeneo madogo
kwenye pembe ya Afrika.
Ukoloni wa Italia ulianza
kuwekeana mikataba kuanzia
mwaka 1889 na Sultani wa
bandari ya Hobyo na mtawala
wa Usultani wa Majerteen.
Mwaka 1892 Sultani wa
Zanzibar alikodi bandari ya
Banadir iliyokuwa kati ya
Mogadishu hadi Brava kwa
Italia. 1905 Italia ilinunua
eneo hili kutoka Zanzibar na
kulitangaza kuwa koloni na
Mogadishu kuwa mji wake
mkuu.
Baada ya vita kuu ya
kwanza ya Dunia, Waitalia
wa l i k a b i d h i wa e n e o l a
Kismayu kutoka Uingereza.
Walilitawala kwa jina la
Oltre Giuba (Ngambo ya
mto Juba) na kuliunganisha
na Somalia ya Kiitalia Juni
30, 1926. Wakati huo huo
waliamua kumaliza hadhi
ya Sultani za Majarteen na
Hobyo ya kuwa nchi iliyo
chini ya ulinzi na kuchukua
maeneo ya Masultani hao
na kuyafanya sehemu kamili
ya koloni lake ndani ya
Somalia. Uamuzi huu wa
Italia ulisababisha vita kali
iliyopiganwa kwa kipindi cha
miaka miwili, kwa sababu
Masultani waliona mikataba
yao ya ulinzi ilivunjwa,
wakapinga jeshi la Italia.
Mwaka 1936 Italia
ikaiunganisha Somalia na
Ethiopia na kuifanya kuwa
koloni lake ndani ya Afrika
ya Mashariki.
Wakati wa vita kuu ya
pili ya Dunia, koloni la Italia
lilivamiwa na Uingereza
mwaka1941. Mwaka 1949
Somalia ilirudishwa tena
mikononi mwa Italia kwa
niaba ya Umoja wa Mataifa.
M wa k a 1 9 6 0 u t a wa l a
wa kikoloni ulikwisha na
Somalia ikapata uhuru wake.

SIAD Barre
Somalia ya Kiingereza
Somalia ya Kiingereza au
British Somaliland lilikuwa
ni eneo linalokaliwa na
Uingereza katika Somalia ya
Kaskazini. Eneo hilo tangu
mwaka 1961 lilikuwa sehemu
ya Jamhuri ya Somalia na
mwaka 1991 likawa Jamhuri
ya Somaliland, yaani nchi
isiyotambuliwa na umma wa
kimataifa lakini yenye tabia
zote za nchi huru.
Uingereza iliingia katika
eneo hili baada ya Misri
kuondoka mwaka 1885,
baada ya kushindwa na
jeshi la Mahdi huko Sudan.
U i n g e r e z a i l i i n g i a k wa
sababu iliona umuhimu wa
kutawala pande zote mbili
za Bab el Mandeb, ikihofia
nchi nyingine za Ulaya hasa
Ufaransa iliyokuwa na koloni
lake la kwanza Ubuk (Obok)
katika nchi ya Djibouti ya
sasa tangu 1862. Somaliland
ilitawaliwa awali kama mkoa
wa Uhindi wa Kiingereza na
baadae ikawa chini ya Wizara
ya Makoloni huko London.
Hata hivyo Uingereza
ilikutana na upinzani mkali wa
wenyeji kuanzia mwaka 1899
wakiongozwa na kiongozi
wa k i d i n i , M o h a m m e d
Abdullah Hassan, aliyeitwa
na Waingereza Mullah
Majununi. Waingereza
walijibu vita iliyopiganwa
miaka 20 iliyoua takriban
theluthi moja ya wakazi wote
wa eneo.
Mwisho wake Uingereza
iliweza kumaliza upinzani
kwa teknolojia mpya ya

ndege za kijeshi zilizotumia


kwa mara ya kwanza katika
Afrika, mabomu na bunduki
za mitambo kutoka angani.
Wakati wa vita kuu ya pili ya
Dunia, eneo likatwaliwa tena
na Italia tangu Agosti 1940
lakini likachukuliwa tena na
Uingereza Machi 1941.
Somalia ilipata uhuru
wa k e i l i p o f i k a 2 6 J u n i
1960. Julai Mosi ikawa ni
muungano wa Somalia (Ya
Kiingereza na Kiitalia). Hata
hivyo baada ya kuporomoka
kwa serikali ya Jamhuri
ya Somalia, eneo la awali
la Somalia ya Kiingereza
likatangaza uhuru wake Mei
1991 na kujiita Jamhuri ya
Somaliland.
Kwa sasa, nchi ya
Somalia haina mamlaka
ya serikali ya umoja wa
kitaifa, imegawanyika kati
ya makundi ya wapiganaji
wa madhehebu ya Kiislamu,
wanajeshi wa serikali
wa k i s a i d i wa n a v i k o s i
vya Umoja wa Afrika na
wanamgambo wa koo na
wababe wa vita.
Tarehe 26 Januari 1991
Dikteta Mohamed Siad Barre
aliyeitawala Somalia kwa
zaidi ya miaka 20 alilazimika
kuachia madaraka na
kukimbia nchi baada ya
kuvurumushwa na mbabe
wa kivita, Mohammed Farah
Aidid. Kuanguka kwa dola
ya Somalia kulikolezwa zaidi
baada ya kumalizika vita
baridi.
Katika enzi za vita baridi,
Mohammed Siad Barre
alikuwa kipenzi cha kambi
ya kijamaa ya nchi za Ulaya

Mashariki, lakini baadaye


aligeuka na kuwa kipenzi
cha nchi za Magharibi. Lakini
baadae nchi za Magharibi
ziliiona Somalia kwamba
kuanguka siasa za magharibi
nchini humo na katika ukanda
wa pembe ya Afrika, kwa
nchi hiyo kubadili mwelekeo
na kuegemea zaidi ujamaa.
Misaada ya nchi za
magharibi ambayo ilikuwa
muhimu katika kuimarisha
nguvu ya dola ya Somalia
ilikoma. Kutokana na
kukosa nguvu za kuimarisha
mfumo wa siasa za nchi,
Rais wake wakati huo Siad
Barre alishindwa kuiendesha
nchi na jeshi lake. Katika
miaka ya 1980, utawala wa
Siad Barre ulipata upinzani
mkubwa hivyo kusababisha
kungolewa madarakani
dikteta huyo wa kijeshi
mwaka 1991.
Januari 1991 alipinduliwa
na kutolewa Mogadishu
na vikosi vya uasi vya
United Somali Congress
(USC) ambavyo vilikuwa
v i k i o n g o z wa n a F a r a h
Aideed aliyekuwa akipata
msaada zaidi kutoka kwa
jamii ya Hawiye, ambao ni
ukoo mkubwa na uliokuwa
unalimiliki eneo la kati Kusini
mwa Somalia. Tangu wakati
huo Somalia imetumbukia
katika janga la vita vya
wenyewe kwa wenyewe,
huku ikikosa serikali imara
hadi sasa.
Kuanguka kwa dola
ya Somalia kulitokana na
msururu wa sababu. Kuna
sababu za ndani kwa ndani
na zile za nje. Yaani sababu
za wakoloni na mataifa
jirani na wasomali wenyewe
ndani ya nchi. Miongo ya
vurugu iliendelea kutawala
nchini Somalia. Vita vya
wenyewe kwa wenyewe vya
kumiliki dola vikatamalaki.
Mogadishu ilikuwa kama
uwanja wa uhalifu mtupu
wa kuwania madaraka,
ambayo makundi mbalimbali
ya kisiasa, kikoo na kidini
walipigana kwa ajili ya
ukuu katika nchi jambo
lililoendeleza umwagaji
damu. Kwa muda mrefu
nchi, haitawaliki, hakuna
kinachofanyika, taifa
limeandamwa na mikosi ya
kila aina, njaa, uhalifu, vita
nk.
Tangu wakati huo hadi
sasa, nchi imekosa serikali
imara, wapiganaji wa
madhehebu ya Kiislamu
wanataka kuydhibiti dola
kwa kuwa muda mwingi
serikali dhaifu na kibaraka
ambayo imeshindwa
kusimamia ustawi wa nchi.
Lakini pia wapo wababe

wa koo kubwa za Kisomalia


ambao nao wanataka kudhibi
dola.
Kuna wakati vilikuwepo
vita baina ya dola ya Somalia
na dola za jirani na zaidi
vikiwa ni vita vya Ogaden
vya mwaka 1977 hadi 1978
kati ya Somalia na Ethiopia.
Kulikuwa na mzozo wa
ndani kati ya mamlaka kuu
na tawala za kifalme na jamii
zilizokuwa za mfumo wa
maisha ya kifugaji, yote haya
yalisababisha kuvurugika
k wa m a m l a k a ya n c h i .
Kuna wakati kiliundwa
chama cha Somali National
Movement (SNM) mwaka
1982 ambacho kilitokana na
ukoo wa Isaaq. Wapiganaji
wa SNM walikuja kuzua vita
kamili vya wenyewe kwa
wenyewe mwaka 1988 pale
waliposhambulia ngome za
serikali za Burco na Hargeisa.
Ambapo Serikali ilijibu
mashambulizi hayo kwa
kutoa kipigo kwa ukoo wa
Isaaq na kuua watu 50,000 na
kusababisha wengine 650,000
kukimbilia nchi jirani za
Ethiopia na Djibouti.
Kuna wakati wapiganaji
wa Kiislamu waliunganisha
nguvu zao na kuunda Umoja
wa Mahakama za Kiislamu
chini Sheikh Sharif Ahmad,
ambaye baadae alikuja kuwa
Rais wa serikali ya mpito
S o m a l i a n a k u f a n i k i wa
kuiondoa madarakani
serikali dhaifu waliyoiona
kuwa ni serikali kibaraka.
Somalia ikapata mweleko
mpya. Lakini hilo nalo
halikukubaliwa na nchi za
Magharibi listawi. Fitna
ikapenyezwa na Marekani
na Ethiopia ikatumika
kuondoa madaraka Umoja
wa Mahakama za Kiislamu
uliokuwa umeanza kuleta
nuru Somalia.
Yakawepo makundi ya
wapiganaji wa Kiislamu
n a Wa p i g a n a j i wa k o o
kubwa hama Hawiye na
wote wanadhibiti baadhi
ya maeneo ya nchi hiyo,
huku kukiwa kuna chochote
kilichopatikana.
Hata serikali ya mpito
i n a y o u n g wa m k o n o n a
Umoja wa Afrika haina
nguvu za kutosha.
N c h i h i y o ya p e m b e
ya Afrika imekuwa kama
haina mwenyewe, wapo
walioigeuza kuwa ngome ya
maharamia, wapo wanaotaka
kuitawala kulingana na ukoo
wenye nguvu zaidi.
Hakuna utawala
madhubuti wa sheria,
hakuna mamlaka yenye
nguvu kusimamia watu
wote, kila upande unafanya
upendavyo. Kwa miaka
sasa ni ghasia, rushwa,
unyanganyi na vifo.
Nchi imekuwa ya maisha
ya vita na mauaji kila upande.
Maisha ya uzima ni ya
kubahatisha.

6
Na Mwandishi Wetu
KUNA usemi na usemi huu
ni wa Kichina ambao tafsiri
yake ni:
Nyayo iliyonyoka,
haikiogopi
kiatu
kilichopindika. Maana
ya usemi huu ni kwamba
mtu mwenye maadili
yaliyonyoka, haogopi
umbeya au udaku. Yaani,
huwa haogopi kusengenywa
au kutiwa hewani, kama
wasemavyo mitaani. Madhali
anachofanya au anachosema
mtu huyo ni cha haki na
cha kweli, kisicho ila wala
waa, madhali ameongoka na
amenyoka, hapaswi kuwa na
hofu ya kutiwa midomoni.
Kwa bahati mbaya,
baadhi yetu wenye uchu
ya kuwapiga darubini
wanasiasa, hususan wale
wenye madaraka, hatukosi wa
kuwatia hewani kila uchao.
Wanajitakia wenyewe. Hayo
husababishwa na hulka yao
kwani tabia moja waliyo nayo
wanasiasa, wa mirengo na
rangi mbalimbali za kisiasa,
ni ya kuupindapinda ukweli.
Hufanya hivyo wakijuwa
kwamba wanadanganya na
kwamba wanaowadanganya
wanajuwa kwamba
wanadanganywa. Lakini
hawawezi kujizuia
wasidanganye.
Inawezekana kwamba
wanapodanganya, nafsi
zao huisuta midomo yao.
Hatujui. Tujuacho ni kwamba
wa m e z o e a k u d a n g a n ya
na kwao kudanganya
kumekuwa kama mchezo.
Kama kucheza bao chini ya
mwembe.
Mtu huwa na mengi ya
kujiuliza anaposimama
Waziri Mkuu bungeni kama
alivyosimama Waziri Mkuu,
Mheshimiwa Mizengo Pinda
wiki iliyopita na kusema,
akiwa na macho makavu
na b ila ya k uyapepesa,
kwamba hayajui yaliyowafika
mashekhe 24 wa Jumuiya ya
Uamsho na Mihadhara ya
Kiislamu, kwa ufupi Uamsho,
waliokamatwa Zanzibar na
kupeleka kufungwa gerezani
Bara kwa tuhuma za ugaidi.
Mahabusu
hao
wanashitakiwa kwa makosa
manne ya ugaidi na kesi yao
iko katika Mahakama ya
Kisutu jijini Dar es Salaam.
Washitakiwa wamekuwa
wa k i l a l a m i k a n a k u d a i
kwamba mashitaka hayo
ni ya bandia na kwamba
kilichowachongea ni
msimamo wao wa kuupinga
mfumo wa Muungano uliopo,
halikadhalika kupigania
Zanzibar irejeshewe
mamlaka yake kamili.
Wamekuwa wakidai kwamba
huo msimamo wao ndio
ulioikera serikali na kuifanya
iwabambikie mashitaka ya
ugaidi.
Katika nyakati tofauti,
walipofikishwa mbele ya
Mahakama, mahabusu
h a o wa l i e l e z a , b i l a ya
kubania, unyama wanaodai
kwamba walifanyiwa
wakiwa gerezani. Shutuma
hizo zimeenea nchini,
zinazungumzwa mitaani,
b a r a z a n i n a z i m e t a j wa
kwenye vyombo vya habari.
Inawezekanaje kwamba
Waziri Mkuu awe peke yake
asiye na fununu yoyote ya
shutuma hizo? Itakuwaje
mtu mwenye wadhifa wa
kuongoza serikali, kama

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

La UAMSHO na alichosema Pinda

MHE. Muhammed Sanya.

MHE. Mizengo Pinda.

MHE. Mariam Msabah

alionao yeye, asijulishwe


pale vyombo vinavyomsaidia
kusimamia sheria
v i n a p o t u h u m i wa k u wa
vimepotoka?
Na hata kama hajapashwa
habari na wasaidizi wake,
h u wa h a s o m i m a g a z e t i
na kufuatilia mambo
kwenye vyombo vya
habari? Hana afisa maalum
anayeshughulika na habari
na anayemjuza yanayojiri
nchini kila siku? Haingii
akilini kwamba Waziri Mkuu
msomi kama yeye hana
utaratibu huo.
Walipofikishwa awali
Mahakamani washitakiwa
hao walidai kwamba
walipokuwa gerezani
walipigwa, waliteswa na
baadhi yao waliingiliwa
kimwili kinyume na
m a u m b i l e . K wa u f u p i ,
walilawitiwa. Huu ni unyama
usio kifani, ni unyama wenye
kulivunjia heshima taifa la
Tanzania, serikali yake na
viongozi wake.
Huo ndio unyama ambao
Waziri Mkuu anatwambia
kwamba hana habari nao
ilihali uliripotiwa kwa kina
na waandishi wa habari
waliokuwapo mahakamani
wakati shutuma hizo
zilipokuwa zikitolewa.
Kwa vile hizo ni shutuma
nzito ambazo baadaye
zimekuwa zikizungumzwa
mitaani, barazani na kwenye
vyombo vya habari, unakuwa
na haki ya kujiuliza, Waziri
Mkuu huyu anaishi nchi
gani? Anaongoza serikali
ipi?Anawatumikia wananchi
wepi?
Wa l a h u t o l a u m i w a
ukifikiria kuwa labda yeye ni
miongoni mwa wale wenye
masikio yaliyozibwa kwa
vizibo maalum ili yasisikie
yasemwayo.
Au p e n g i n e a n a h i s i
kwamba hana ubavu wa
kuwakosoa wanaotuhumiwa
kukiuka haki za binadamu?
Labda ana uungwana wa
kutoweza kufanya hivyo
kwani si yeye aliyewahi
kuwaruhusu polisi wawatie
adabu waandamanaji kwa
kuwapiga? Alijisema wakati
huo, wapigwe tu!
Hatujasahau yaliyojiri
B u n g e n i wa k a t i m m o j a
pale Waziri Mkuu Pinda

alipokuwa akimjibu Mbunge


wa Kilwa Kaskazini, Murtaza
Mangungu, aliyelilaumu
jeshi la Polisi kwa nguvu
linazotumia linapopambana
na wananchi wanapokuwa
wanaandamana.
Pinda alimjibu Mangungu
kwa kusema: Ukifanya fujo
umeambiwa usifanye hiki
ukaamua wewe kukaidi
utapigwa tu maana hakuna
namna nyingine maana wote
lazima tukubaliane nchi hii
tunaiendesha kwa misingi
ya kisheria sasa kama wewe
umekaidi hutaki unaona
kwamba ni imara zaidi, wewe
ndio jeuri zaidi watakupiga tu
na mimi nasema muwapige
tu, kwa sababu hakuna
namna nyingine maana
tumechoka sasa.
H a p o Wa z i r i M k u u
Pinda amekiri mwenyewe
kwamba amewashajiisha
polisi watumie nguvu badala
ya sheria kupambana na
wa a n d a m a n a j i a k i j u wa
vyema kwamba wananchi
hao hawakuhalifu sheria
n a k wa m b a wa m e k u wa
wakitumia haki walizopewa
na Katiba ya nchi.
Sasa ikiwa Pinda
amewaamrisha polisi
wawapige wananchi
wenye kutumia haki zao
za kikatiba za kukusanyika
na kuandamana, atawezaje
k u wa k e m e a p o l i s i h a o
hao wakiwatesa mahabusi
wanaotuhumiwa kwa ugaidi?
Ndio maana Mei 21 kwenye
kikao cha maswali ya papo
kwa papo Bungeni alijifanya
k a m a m t u a l i ye j i b a n z a
nyuma ya miti na asiyeona
wala kusikia yaliyo bayana
mitaani.
Kwenye kikao hicho
Mbunge wa Mji Mkongwe,
Muhammad Sanya, alimtaka
Waziri Mkuu aunde Tume
M a a l u m ya U c h u n g u z i
itayochunguza tuhuma
za ukatili na unyama
zilizotolewa na viongozi
wa Uamsho walio gerezani
Tanzania Bara.
S a n ya a l i t u m i a n e n o
unyanyasaji lenye maana
ya kutesa, kudhalilisha au
kuonea. Na ikiwa tuhuma za
Sheikh Farid Hadi Ahmed,
mmoja wa mahabusu hao,
zina ukweli, basi hivyo ndivyo
wa l i v y o f a n y i wa w e n g i

wao gerezani huko Bara:


waliteswa, walidhalilishwa
na walionewa.
Vi t e n d o v y o t e h i v y o
ni vyenye kukiuka haki
za binadamu, ni vyenye
kwenda kinyume na
maadili ya utawala bora
na ni sababu za kutosha
zinazoweza kuwafikisha
wenye kuvitenda mbele ya
Mahakama ya Kimataifa ya
Jinai mjini Hague, Uholanzi.
Alichopaswa kukifanya
Mheshimiwa Waziri Mkuu
Pinda na mawaziri wake
wa Sheria na wa Mambo
ya Ndani mara tu baada
ya kuibuka shutuma hizo
Mahakamani, ni kuunda jopo
maalum la kuzichunguza au
walau kutoa taarifa rasmi
ya kiserikali kuzikanusha
kama ni shutuma zisizo na
mashiko. Iwapo shutuma
hizo zina ukweli, hata ikiwa
ni nusu ya chembe ya ukweli,
basi ilikuwa wajibu wake
kuwachukulia hatua zifaazo
wenye kuhusika. Katika hali
hiyo mawaziri wa sheria
na wa mambo ya ndani
wangewajibika kujiuzulu
pamoja na maofisa wa ngazi
za juu wa magereza.
Waliotambulika kuwa ndio
waliotesa wangefikishwa
Mahakamani wakashitakiwa
na kupewa adhabu
inayostahiki, watapopatikana
na hatia. Mheshimiwa Waziri
Mkuu Pinda hakuchukuwa
hatua zozote alizostahili
achukuwe. Badala yake
alikimbilia msituni kujibanza
nyuma ya miti akijidai
kwamba hakuwa akijuwa
Sanya akisema nini.
Alisema alikuwa hajui
S a n ya a n a wa z u n g u m z a
kina nani, seuze kujuwa
iwapo wamo gerezani, wala
hakujuwa wamekamatwa
kwa kosa gani licha ya
kwamba walishafikishwa
kabla mahakamani zaidi ya
mara moja.
Lenye kutisha zaidi ni
k wa m b a h a wa n i wa t u
wanaoshitakiwa kwa makosa
ya ugaidi, si kosa moja, ni
makosa manne na Waziri
Mkuu anasema hana habari
nao. Tena katika kesi ya
kwanza ya aina yake nchini.
Wala hakuwa akijuwa jinsi
mahabusi hao walivyoteswa.
Na ikiwa hujui kitu ndio

hujui. Unakuwa huna


dhambi. Huna lawama wala
hulaumiki. Ikiwa Pinda
ametumia mantiki hiyo, basi
ametumia mantiki finyu
iliyopindika.
Ukweli wa mambo ni
kwamba hatuwezi kumtoa
lawamani, kwani ni muhali
kabisa ya kuwa hajui
yaliyowafika hao mashekhe
wa Uamsho.
Mwisho hivi majuzi tu Mei
11, Farid aliyaeleza Mahakama
k wa u f a s a h a n a u wa z i
namna walivyotendewa.
Miongoni mwa aliyoyasema
n i k wa m b a t u k i wa a c h a
wao 24 walioshitakiwa kwa
kesi moja kwa jumla kuna
Wazanzibari wasiopungua
50 walio katika magereza ya
Bara wakishutumiwa kwa
makosa ya ugaidi.
Farid alieleza jinsi wengi
wa o wa l i v y o c h u k u l i wa
majumbani mwao saa
nane za usiku, wengine
walivyovunjiwa milango
yao na kusafirishwa kutoka
Zanzibar kupelekwa
Tanganyika, hatua ambayo,
alisema, ni ya udhalilishaji
k wa v i l e Z a n z i b a r i n a
Mahakama yake Kuu yenye
hadhi sawa kama Mahakama
Kuu yaliyo Bara.
Aidha, Farid alisimulia
namna walivyokuwa
wakihojiwa kishenzi,
kikatili walipofika Bara.
Alitoa mfano wa jinsi
a l i v y o k u wa a k i s a i l i wa
m s h I t a k i wa m w e n z a k e
Sheikh Msellem bin Ali,
a l i ye m u e l e z e a k u wa n i
mtu mwenye kuheshimika,
kiongozi wa Jumuiya ya
Taasisi ya Kiislamu na mfasiri
wa Quran Tukufu. Alisema
kwamba Msellem alihojiwa
akiwa uchi kama mnyama.
Aliongeza kwamba
takriban wote walihojiwa
namna hiyo. Kwa mujibu
wa Farid, Msellem baadaye
alihojiwa akiwa ametundikwa
huku akifungwa pingu hali
akiwa uchi.
Farid na mwenzake Salum
Ali walimueleza Hakimu
kwamba wenzao wanne
wamegoma kula chakula na
hali zao ni mbaya na ndio
maana hata hawakudiriki
kufika Mahakamani. Kati ya
waliohudhuria walikuwepo
waliokuwa wakichechemea
kwa sababu ya kuteswa,
walidai kina Farid.
Kiongozi huyo wa Uamsho
aliongeza kudai kwamba kesi
yao ni ya kisiasa kwa sababu,
alisema, walitiwa nguvuni
kwa vile wamekuwa wakidai
Zanzibar irejeshwe heshima
yake na kwamba pawepo
usawa baina ya Zanzibar na
Tanganyika.
Farid, aliyesema:
hatuwezi kudhulumiwa
haki yetu tukakaa kimya.
Alimwambia Hakimu
kwamba yeye na wenzake
wanahitaji Jaji Mkuu,
Mwanasheria Mkuu wa
Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Mwanasheria
Mkuu wa Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania
na Waziri wa Katiba wa
Zanzibar, waende gerezani
kuonana nao.
Ni ajabu kuona kwamba
yote hayo yakijiri, Waziri
Mkuu anasema kwamba
yeye hajui chochote kuhusu
kadhia hiyo.
(Makala hii ni kwa hisani
ya Zanzibar Daima)

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Propaganda za udini shuleni Tanzania-5

Profesa Ibrahim Noor Shariff


MUDA waliokuwa baadhi
ya Wazanzibari na Waarabu
wa m e n u n u a wa t u m wa
ulikuwa ni mdogo sana
ukilinganisha na ule
walioutumia Wazungu. Na
Zanzibar yenyewe ni nchi
ndogo sana tukilinganisha
na nchi zilioko Amerika. Sir
John Gray anatuelezea kwa
Kiingereza kuwa:
Tafsiri: [] Ama mwishoni
mwa 1821 au mwanzoni
mwa 1822 yeye [Sayyid Said]
aliwapelekea barua maofisa
wake Afrika kupiga marufuku kuwauzia watumwa
dola yoyoyote ya Kikristo.
Kwanini Sayyid Said
akapiga marufuku kuuzwa
watumwa 'nchi za Kikristo?
Moja katika sababu ni namna
ya ukhabithi waliokuwa
wa k i f a n y i wa wa t u m wa
wa Kiafrika na Wazungu
Wakristo. Hata Bwana akizaa
na mtumwa wake, basi si
ajabu akipungukiwa na
pesa kumwuza mwanawe
aliyemzaa pamoja na suriya
wake. Angalia kisa cha Keze
katika kitabu cha Alex Hailey
"Roots."
Sasa iwapo kuanzia 1822/3
Sayyid Said bin Sultan alipiga
marufuku, katika mamlaka
zake (mulimokuwa wakiishi
Waswahili na Waarabu)
kuuziwa watumwa Wakristo
wakati ambao Wafaransa
na Waportugizi wametia
fora katika kununua na
kusafirisha watumwa
kutoka Msumbiji na
sehemu za Afrika Kusini
na Magharibi (kuwapeleka
katika nchi zilioko Amerika)
na Waswahili na Waarabu
hawakuwa wakienda
Bara ndani kuwakamata
watumwa, sasa waliokuwa
wakifanya hili ni nani? Jawabu
liko wazi kabisa, makabila
ya Kiafrika yaliyokuwa
n a n g u v u . K wa h i v y o
walioshtadi na kuikakania
biashara hiyo walikuwa
Wazungu wakifuatiwa na
Waafrika, wala sio Waarabu
wala Waswahili. Waislamu
wengi wametenda mengi
kuondosha biashara
ya utumwa. Ukweli huu

kukhusu aliyoyatenda
Sayyid Said bin Sultan kwa
mfano hausomeshwi kabisa
katika shule za Tanzania.
Badala yake yanayooneshwa
vitabuni na kusomeshwa
ni maovu matupu kukhusu
Waislamu. Anayesifiwa ni
Mwingereza peke yake.
Tumeonesha waziwazi
kuwa usomeshaji wa historia
Tanzania umejaa propaganda
za udini dhidi ya Uislamu,
na Waswahili na Waarabu
wa n a t u m i wa t u k a t i k a
propaganda hizo. Hili liko
wazi kabisa kuwa miongoni
mwa wale waliopewa jukumu
la kuandika vitabu vya
historia vinavyofundishwa
m a s h u l e n i Ta n z a n i a
hawakuitendea haki ile
dhamana waliopewa na
wameonesha unafiki na
chuki zao za wazi kabisa
dhidi ya Uislamu, Waislamu,
Waarabu na Waswahili, na
wa m e o n e s h a wa z i wa z i
mapenzi yao juu ya siasa kali
za udini ambazo ukiziangalia
utaona hata hazilingani na
mafunzo ya Yesu.
Ili kuhakikisha uongo
huu na fitna hii inatapakaa
na kuganda katika bongo
za wanafunzi, basi kila
sehemu ilipotajwa utumwa
na kuoneshwa picha utaona
picha hiyo ni ya Mwarabu
au ya Mwafrika Mwislamu
ili kuonesha taswira ya kuwa
watendaji wa uovu huo si
wengine bali ni Waislamu.
Ingawa waandishi wa vitabu
kama hicho cha Historia cha
Form Two, Perazia Kaloly, na
Felix Kiruthu wamesisitiza
katika jalada la mwisho
la kitabu hicho umuhimu
wake wa kuweka michoro
ili kuonesha uhalisia thabiti
wa kitendo au tokeo lile,
wameandika yafuatayo:
Ilustrations and
photographs throughout
the book to depict authentic
situations.
Tafsiri: Michoro na picha
katika kitabu chote ni
kuonesha uhalisia thabiti wa
matokeo.
Inasikitisha kuona baadhi
ya picha zilizomo vitabuni
ama zimeghushiwa au zile
za matokeo yaliyobuniwa
ambayo kwa hakika
hayakutokea kabisa Afrika
Mashariki, na hata Afrika
kwingineko, bali zimeingizwa
kwa makusudi kwa lengo la
kupotosha ukweli na hapana
shaka zitakuja kuleta chuki
na mifarakano katika jamii,
kama si leo, basi karibuni.
Waandishi hao wa vitabu
hivyo vya shule vya historia
wamesahau kuwa tunaishi
katika ulimwengu ambao
umepevuka kimtandao
wa khabari, na ni rakhisi
mtu kugundua kila
lililoghushiwa. Nitanakili
picha nyingine ziliomo
vitabuni na mukhtasari wa

Hii ni picha iliyochorwa karibuni na wenye siasa kali


za udini Tanzania yenye udanganyifu usioingia akilini.
maelezo yake ili ufanye
milingano na tathmini na
uwe hakimu wa kuzihukumu
p i c h a z e n ye we , n a p i a
uwahukumu waandishi wa
vitabu hivyo vya historia,
khalafu ufanye uamuzi ama
uwe pamoja na upotofu huo
na uwaachilie watoto wetu
wa e n d e l e e k u p o t o s h wa
na kujazwa chuki dhidi
ya ndugu zao Watanzania
wenzao na binadamu wenzao
wasiokuwa Watanzania,
na patakapoanza pata
shika na nguo kuchanika,
na haya yameshaanza
Tanzania, tufahamu tu kuwa
hapatakuwa na mshindi
ila kuenea vifo na khasara
kubwa kwa nchi nzima.
Nakariri, hakuna atakaeibuka
kuwa mshindi, nchi yote
itakhasirika ila pasimame
haki na kukemewa batili
na kuondoshwa dhulma za
propaganda ili kuondosha
mfarakano katika jamii.
Soko za Kuuza na Kununua
Watumwa Afrika Mashariki
Picha mbili zinazofuata
zinakhusu soko za watumwa
Afrika Mashariki. Ya kwanza
nitakayoizungumzia ni ile
inayotokana na maelezo ya
soko la watumwa Zanzibar
iliochorwa katika miaka
hiyo kama jinsi soko hilo
lilivyoshuhudiwa na
Stanley. Picha na khabari
zake zaidi utazipata katika
kitabu kinachoitwa Journey
through Africa. Picha ya

pili Tafsiri ya maneno


yaliyoandikwa chini ya picha
inasema:
Mateka wepya wa TIPO
wakipelekwa utumwani
Yameshuhudiwa na Stanley.
Kama tulivyoelezea
kabla, Tipu Tip aliwahi
mara moja tu kuwakamata
wanyonge bara na kuwauza
hukohuko bara. Kwa ajili
ya tokeo hili moja, wenye
siasa kali za udini wanamtaja
Tipu Tip kama ndiye yeye
aliyekuwa mkamataji na
mfanya biashara mkubwa
kabisa wa watumwa. Pia
tumeeleza kabla kuwa Tipu
T i p h a k u wa m k a m a t a j i
mkuu wa watumwa wala
hajawahi kufanya misafara
ya watumwa na kuwapeleka
pwani. Kama kweli alikuwa
n a wa t u m wa , k wa n i n i
asiwatumie watumwa hao
kumchukulia bidhaa zake
bara badala ya kuwaajiri
wa p a g a z i n a k u wa l i p a
mapesa? Stanley pia aliajiri
wapagazi kupitia kwa Tipu
Tip. Jee, na Stanley pia
alikuwa mfanya biashara
mkuu wa watumwa?
tutakayoi-zungumzia pia
inaonesha soko la utumwa
Zanzibar ambayo imechorwa
katika kitabu cha Darasa
la Tano, ukarasa wa 42 na
mchoraji Cloudy Chatanda,
katika kitabu kilichoandikwa
na Denis H.S. Mangwela.
Iangalie hii picha ya kwanza
kwa makini:
Picha hii inatupa hali

inayoingia akilini ya soko


la watumwa lilivyokuwa na
inaelezea mengi kama vile
kuwatambulisha wanunuzi,
wa u z a j i , wa p a g a z i , n a
watazamaji ambayo ni hali
ya kawaida inayoonekana
katika kila soko, iliyobakia
wewe mwangaliaji uiangalie
picha hiyo vizuri, na umweke
kila aliechorwa hapo sehemu
anayostahiki kwani tokeo hilo
lilitokea na kushuhudiwa na
mtu ambaye anaaminiwa na
wengi. Mimi tafsiri yangu
ya mchoro huo ni kuwa,
wa t u m wa n i Wa a f r i k a ,
madalali ni Wazungu au
M u h i n d i , wa n u n u z i n i
Wa z u n g u , w a m i l i k i ,
wapagazi na wasafirishaji
ni Waafrika, watazamaji
ni Waarabu na Waswahili,
wanunuzi wa pembe za
tembo na bidhaa nyingine ni
Waarabu na Waswahili. Hivi
ndivyo picha inavyosema.
Lakini, hapana shaka yoyote
kuwa na baadhi ya Waarabu
na Waswahili pia walishiriki
katika ununuzi wa watumwa
ingawa picha hii haioneshi
hilo, na sababu yake ni
wazi kabisa, nayo ni kuwa
waliokuwa wanawahitajia
watumwa kwa wingi sana ni
Wazungu katika makoloni
yao na si Waswahili na
Waarabu.
Sasa soma maneno
ya f u a t a y o ya a l i e k u wa
Muakilishi wa Ubalozi wa
Kiingereza Zanzibar uyaweke
katika picha hio na uhukumu
kama yalivyo-nukuliwa na
R.Coupland:
Tafriri: Wakati Hammerton
alipopandisha bendera
ya U i n g e r e z a Z a n z i b a r
mwaka 1841, alikuta
jumla ya Wahindi raia wa
Kiingereza kisiwani au katika
miji ya mwambao ndani
ya utawala wa Said katika
Afrika Mashariki ilikuwa
tayari ni kubwa; alihisabu
idadi yake mwaka 1844
kuwa karibu ya Mabaniyani
khamsu mia na Wahindi
Waislamu baina ya sita na
saba miya. Khalafu mapema
akagundua biashara karibu
zote za Afrika Mashariki
zilikuwa katika mikono yao.
Sehemu kubwa ya biashara
ya utumwa, pembe za ndovu,
na sandarusi, aliandika
mwaka 1841, [biashara hizo]
zinafanywa na wenyeji wa
India, Waarabu wanafanya
machache au hawatendi
chochote katika hayo. Na
mwaka 1844 [kaandika]:
Alimradi Waarabu wakiweza
kununua watumwa kwa bei
rahisi kuwalimia mashamba
yao ya karafuu, ambayo
huwapatia faida kubwa,
ni machache unayoweza
kutegemea kutoka kwao.
Yaani, Warabu walikuwa
hawakujishughulisha
na kukamata wanyonge
Inaendelea Uk. 13

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Uchaguzi Mkuu Oktoba, ujumbe kwa Waislamu!


Tushiriki siasa kwa kuchunga mipaka ya Uislamu
Na Said Rajab

UCHAGUZI Mkuu wa Urais,


Wabunge na Madiwani
u m e k a r i b i a s a n a . K wa
Waislamu, mazingira ya
uchaguzi Mkuu wa mwaka
huu, ingawa yanaonekana
kuwa tofauti na chaguzi
zilizopita, lakini kimsingi
hakuna tofauti yoyote.
Wa i s l a m u k a m a j a m i i ,
h a wa j a wa h i k u n u f a i k a
na ushiriki wao katika
siasa za nchi hii. Nguvu
zao za kisiasa zimekuwa
zikitumika tu kuuweka
na kuupalilia mfumo
ambao umewakandamiza
n a
u n a e n d e l e a
kuwakandamiza. Tangu enzi
za mapambano ya uhuru,
Waislamu, kama raia wa nchi
hii, wamekuwa mstari wa
mbele kupigania heshima na
ustawi wa taifa hili. Ingawa
wametoa mchango mkubwa
sana katika mapambano
ya k u m n g o a m k o l o n i ,
lakini mchango wao huo
umefichwa kwa makusudi
na kumekuwa na jitihada
kubwa za kupoteza historia
hii adhimu ya Waislamu.
Kwa kipindi kirefu sana,
Waislamu wamekuwa na
madai yao ya msingi. Na
kama ilivyo ada, Serikali
ya nchi hii, katika awamu
zake zote, imekuwa
ikipuuza madai hayo.
Waislamu wamelalamika,
wamefanya makongamano,
wamekaa Itikafu, wamelia,
wameandamana, wamejaribu
kutumia kura zao, lakini bado
Serikali imekuwa kiziwi kwa
madai ya Waislamu. Imefikia
mahali Waislamu tunajiuliza,
nini itakuwa hatma yetu na
kizazi chetu hapa Tanzania?
Kwa wale wanaofuatilia
mambo sawasawa, utaona
tangu wakati wa mapambano
ya kudai uhuru, mfumo wa
kisiasa uliowekwa nchini
Ta n z a n i a u n a w a e n g u a
Waislamu. Mfumo hauwataki
Waislamu, bali unataka
majina yao tu! Ili Waislamu
wanufaike na mfumo wa
kisiasa uliopo, basi lazima
wa s h i r i k i s i a s a b i l a ya
Uislamu! Lakini wenzao
wa upande wa pili, mfumo
unawabeba, wanashiriki siasa
wakiwa na dini yao. Huo ndiyo
mtego uliowekwa kwenye
uwanja wa siasa Tanzania.
Waislamu wanatakiwa wawe
Watanzania (wazalendo) zaidi
kuliko walivyo Waislamu!
Baada ya Mswaada
wa Mahakama ya Kadhi
kukwama Bungeni, kutokana
na nguvu ya Wakristo, kuna
baadhi ya watu wameshaanza
kuwachagiza Waislamu,
kutumia kura yao vyema
wakati wa uchaguzi Mkuu
wa Oktoba mwaka huu.
Nimeona nizungumze kidogo

MHE. Edward Lowassa (kushoto) alipokuwa katika harambee


ya kuchangia Msikiti wa Patandi, Arusha hivi karibuni.
kuhusu ushiriki wa Waislamu maadili yake na mwenendo
katika siasa, ili watu wabaya wake. Waislamu nchini
wasije kuwachuuza kama Tanzania lazima waendelee
wanavyofanya kila wakati. kutekeleza Uislamu na kuwa
Tuwe tunawaambia ukweli mabalozi wazuri wa Dini
Waislamu kuhusu mfumo hii ya Mwenyezi Mungu.
wa kisiasa wa Tanzania na Yaani waufahamu Uislamu,
tuache kujipa matumaini wautekeleze, waufundishe,
hewa. Kweli kabisa, mfumo wa l e e wa t o t o wa o k wa
wa kisiasa wa Tanzania misingi yake na muhimu
umewaangusha Waislamu zaidi, waulinganie Uislamu
kwa kipindi kirefu mno. katika jamii pana zaidi. Hii
Kuwanganganiza Waislamu ni pamoja na kuunga mkono
washiriki siasa zilizojengwa Umma wetu popote ulipo
juu ya mfumo huo, bila ya duniani na kutafuta ufumbuzi
kutafuta majawabu halisi wa madhila yanayoukabili.
ya kwanini umeshindwa Wakati hili linaonekana kuwa
kuwasaidia tangu awali, gumu katika mazingira ya
ni kusaidia tu jitihada za sasa, lakini kimsingi, ndilo
kuwatosa Waislamu. La linaloleta radhi za Mwenyezi
msingi zaidi kwa Waislamu Mungu, kwa kusimamia
hivi sasa ni kutafakari kwa ujumbe wake. Mwenyezi
k i n a , v i p i wa t a e n d e l e a Mungu anasema:
kubaki na dini yao katika
Na ni nani asemaye kauli
mazingira haya magumu. bora zaidi kuliko aitaye
Kwa kuzingatia muktadha (viumbe) kwa Mwenyezi
huo, nitaangazia nukta nne Mungu, na (Mwenyewe)
muhimu ambazo nahisi akafanya vitendo vizuri na
zinahitaji ufafanuzi mzuri, husema (kwa maneno yake
ili Waislamu waweze kutoa na vitendo vyake): Hakika
tafsiri sahihi ya mambo mimi ni miongoni mwa
yanayotokea hapa nchini, Waislamu, (kwa hivyo niko
hususan yale yanayowahusu pamoja nao kwa kila jambo)
wao na dini yao.
Qur (41:33).
Kwanza kabisa, ni vyema
Ajenda yetu siyo kuupalilia
Waislamu wakafahamu kuwa mfumo uliopo au kuingizwa
kipaumbele chao cha msingi (assimilated) kwenye mfumo
ni kutekeleza Uislamu, huo unaopingana na dini

yetu. Waislamu wakikubali


hilo na kuliona ni jambo la
kawaida, watakuwa sawa
na jamii nyingine za kidini
z i l i z o g e u z wa k u wa z a
kisekula. Huwezi kuingizwa
kwenye mfumo huu, halafu
ukabaki na Uislamu wako
kamili. Haiwezekani kamwe!
Pale jamii za Kiislamu duniani
z i l i p o k u b a l i k u i n g i z wa
kwenye mifumo, maadili na
taratibu zisizo za Kiislamu,
zikajikuta zimeachana kabisa
na Uislamu, hususan katika
maeneo yake muhimu ya
kisiasa, kijamii na kiuchumi,
na hatimaye zikawa hazina
tofauti sana na jamii za
Kimagharibi. Leo hii
jamii nyingi za Kiislamu
zinakabiliana na matatizo
yale yale yaliyopo kwenye
Ulimwengu wa Magharibi
- maadili mabovu ya vijana,
familia kusambaratika,
majanga ya ngono holela
na vurugu nyingine za
kijamii. Hayo ni matokeo ya
kwenda kinyume na mfumo
wa maisha ulioelekezwa na
Mwenyezi Mungu:
Na atakayejiepusha na
mawaidha yangu (hayo), basi
kwa yakini atapata maisha
yenye dhiki, na siku ya Kiama
Tutamfufua hali ya kuwa
kipofu Qur(20:124)
Hata hivyo, haiwezekani
kutekeleza Uislamu kwa
Wa i s l a m u k u j i t e n g a n a
jamii. Lazima tuingiliane
na jamii pana zaidi, ili
t u we z e k u wa s i l i s h a n a
kufafanua ujumbe wa
Kiislamu. Kwa hiyo, wakati
tunakataa assimilation,
lazima pia tukatae kujitenga.
Tunapaswa kushirikiana na
wengine kwa misingi ya
Kiislamu, ndani na nje ya
jamii yetu. Tukishiriki kichwa
kichwa kwenye mfumo wa
kisiasa uliopo, haitatufikisha
kwenye dhamira hii. Tena
itatutoa kabisa kwenye lengo
kuu la Uislamu na kutufanya
tukumbatie, mila, desturi,
maadili, tamaduni na taratibu
za kisekula, ambazo kimsingi
zinapingana na dini yetu.
Tutaitwa tu Waislamu, lakini
bila ya Uislamu.
Pili, ni vyema Waislamu
wakafahamu pia kwamba
m f u m o h u u wa k i s i a s a
unaifanya jamii kuwa ya
kisekula. Lengo hasa la
kuwashawishi Waislamu
kushiriki siasa za kisekula
ni kuhakikisha kwamba
Waislamu wanaunga mkono
na kukumbatia mfumo
huu wa kisiasa usio wa
Kiislamu. Matokeo ya hili,
kama tulivyoona, kadri
Wa i s l a m u wa n a v y o z i d i
kujiingiza kwenye mchakato
huu wa kisekula, ndivyo
wanavyozidi kuifanya
mitazamo yao kuwa ya

kisekula zaidi, na hatimaye


kuunga mkono kwa uwazi
kabisa misimamo isiyo
ya Kiislamu. Utashangaa
kumuona Muislamu
anatafuta hoja na mashiko
ya Kiislamu, ili kuhalalisha
jambo ambalo msingi wake
ni ukafiri! Kwa kuwa yeye
ameshatumbukia kwenye
mtego, hawezi kujinasua,
sasa anataka na wenzake
watumbukie! Tumeshuhudia
kwa miaka mingi wabunge
Waislamu wakiupa kisogo
Uislamu na kuunga mkono
misimamo isiyo ya Kiislamu.
Kweli kabisa, kuunga mkono
vyama vya siasa kwenye
mfumo wa kisekula, aidha
k wa k u j i u n g a , k u f a n ya
kampeni au kuvipigia kura,
bila ya uangalivu wa kutosha,
ni sawa na kuidhinisha sera
za maangamizi dhidi ya
Uislamu!
Ta t u , Wa i s l a m u p i a
wanapaswa kuelewa kuwa
mchakato wa kisekula wa
kisiasa huwa hauna tija sana
kwa wananchi wanyonge
walio wengi. Watu wengi
wa kawaida katika nchi za
kisekula wanazidi kujiengua
kutoka kwenye siasa. Idadi
ya wapiga kura inazidi
kupungua. Hoja yao ni rahisi
tu: kupiga kura hakuna maana
- hakuleti mabadiliko yoyote
katika maisha yao. Hii hisia
kwamba kupiga kura hakuna
maana inasukumwa zaidi na
ukweli kuwa kwenye nchi
za kisekula, zinazoongozwa
na Ubeberu, mfumo wa
utawala unatumikia vigogo
wachache, siyo wananchi
wa k a wa i d a . Wa n a n c h i
hutumika tu kuhalalisha
mfumo wa kidhalimu.
Uhusiano wa matajiri,
watu mashuhuri na
wanasiasa, ndivyo
vinavyoamua sheria na sera
za nchi. Kinachofanyika
kupitia uchaguzi ni kuingiza
tu udikteta madarakani
kwa njia ya kura (elected
dictatorship). Utawala ni wa
vigogo, unawekwa na vigogo,
kwa ajili ya vigogo! Kura
ya mtu wa kawaida haina
maana yoyote. Nitashangaa
sana nikisikia, bado kuna
Wa i s l a m u h a p a n c h i n i ,
wanaoamini kwamba kura
yao ina thamani! Wanaamini
kura yao inaweza kuleta
mabadiliko ya kuwanufaisha
wao na dini yao, ndani ya
mfumo wa kisiasa unaopinga
Uislamu! Kuamini kwamba,
Wa i s l a m u wa k i j i p a n g a
vizuri, wanaweza kuingiza
wabunge wengi zaidi, walio
marafiki wa Uislamu ni
kutapatapa tu - ni kuendeleza
hoja ile ile potofu ambayo
kwa miaka nenda miaka
rudi, haikuwahi kuwasaidia
Waislamu hata kidogo! Miye
ninavyofahamu, kama watu
wamechoshwa na mfumo
Inaendelea Uk. 13

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Namsikitikia sana Waziri Mkuu Pinda


Na Mwadini Ali

N AYATA FA K A R I m a j i b u y a
kiongozi mtendaji mkuu wa serikali
alipoulizwa swali bungeni akitakiwa
kutoa msimamo wa serikali kuhusu
kadhia ya masheikh na maulamaa wa
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya
Kiislamu (JUMIKI) wanaolalamika
kudhalilishwa ndani ya magereza
kiasi cha kutishia kuanzisha mgomo
wa kula.
Swali lililoulizwa kwa zaidi
ya sekunde 240, muulizaji akitoa
maelezo ya kina na kwa ufasaha,
linajibiwa kwa chini ya sekunde 150,
mjibuji akitoa kauli tata, zisizotoa
mwelekeo wa kutegemewa kuleta
utatuzi wa malalamiko.
Mara nyingi imetokea nikamsikia
kwa mashikio yangu Waziri Mkuu
Mizengo Kayanza Peter Pinda
akitoa maelezo yanayozua utata na
kusababisha mjadala mkali, lakini
sikufikiria kuwa kiongozi huyu
atafikia hatua ya kutoa matamshi
ya n a y o m v u a u a d i l i f u n a m n a
nilivyomshuhudia hivi karibuni. Na
kwa sababu nimekuwa nikimfuatilia
kauli zake na kuzipima, mantiki
ninayoipata binafsi na hapo hapo
nikitafakari kile alichokusudia
k u k i e l e we s h a a u k u d h a m i r i a ,
mantiki hiyo ndiyo anayotaka
igande sawasawa akilini mwa
wale wanaomsikiliza wakati huo
anapozungumza, na umma kwa
ujumla wake. Sasa nafika hatua
kujiuliza maswali ambayo sipati
majibu.
Waziri Mkuu Pinda, yule ambaye
alipoteuliwa tu kushika wadhifa huo
Februari 2008 aliliambia bunge kuwa
yu mtoto wa mkulima, akimaanisha
anatoka kwenye familia masikini,
naona amebadilika sana. Akiwa
aliyeanza vizuri na kwa umakini
utaratibu wa kuulizwa maswali
ya papo kwa papo bungeni na
kuyajibu kwa ufasaha, katika kipindi
cha karibuni, Waziri Mkuu Pinda
amekuwa kiongozi tofauti kabisa na
vile alivyojitokeza na kujionesha siku
hizo za mwanzo za uteuzi wake.
Waziri Mkuu Pinda amekuwa
mjanja badala ya Mtu makini. Mtata
badala ya kiongozi mnyoosha mambo
hasa anapoulizwa jambo lililojaa
utata, kila anapozungumza. Kiongozi
asiyetabirika hata pale unapotarajia
ajibu kwa ufasaha na umakini
akitumia maneno machache kuhusu
kile alichoulizwa.
Pengine Waziri Mkuu Pinda ni
kweli kama wasemavyo baadhi ya
ninaokutana nao tukamuongelea,
amekuwa ni muoga kiuongozi. Na
labda amekuwa hivyo kwa sababu
amejifunza katika miaka yake saba
ya wadhifa anaoshika, ukitaka
kuishi na mfumo wa uongozi wa
serikali inayoongozwa na Chama
Cha Mapinduzi (CCM), basi nawe
uwe muoga, usiyeaminika na mtu
dhaifu usiyetabirika. Hapo ndipo
Waziri Mkuu Pinda huyu tunayemjua
alipojifikisha. Nami namuona amefika
hapo hasa. Ndivyo watu hata wa
kawaida, achilia mbali wale wenye
weledi katika kuyatafakari mambo
yanavyokwenda ndani ya jamhuri
yao, wanavyomtathmini.
Watu hawa wa kawaida, ambao

RAIS Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kushoto).
Katikati ni Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal.
mtu ungetarajia ndio mheshimiwa
angewashinda nyoyo zao katika
kumuamini na kumtetea anapojikwaa,
wanamuona Pinda amekengeuka
hata ile taswira ya kuwa ni mtu
makini, muadilifu na asiye na
makuu, aliyoijenga pale mwanzoni
alipoteuliwa. Siku wananchi hao hao
waliokuwa wamejenga imani naye,
wanamtizama kivingine kabisa.
Siku hizi tunazoenda na pengine
inachochewa na mwelekeo wa
uchaguzi mkuu wa Oktoba, Waziri
Mkuu Pinda amekuwa kiongozi
asiyeeleweka. Ni kama vile amesahau
jukumu la Uwaziri Mkuu. Wala
haoni vibaya tena kukwepa swali
la mbunge. Amekosa hata huruma,
kama vile alisahau alivolia bungeni
kuhusu mauaji ya watu wenye
ualbino.
Shida inakuja zaidi anapoulizwa
bungeni na mbunge wa kambi
rasmi ya upinzani, siku hizi ikiwa
imekolezwa mvuto na UKAWA
Umoja wa Katiba ya Wananchi usoni
anaonesha, siwezi kusema jeuri,
lakini labda kutokujali, na akianza
kujibu huanza kwa kejeli.
Ndivyo alivyosomeka alipoulizwa
na Mbunge wa Mji Mkongwe,
Muhammed Ibrahim Sanya wiki
iliyopita. Aliulizwa kama serikali
inaweza kuunda Tume ndogo
itakayoshirikisha pia wabunge
kutoka Zanzibar na Tanganyika,
kuchunguza malalamiko ya kuhusu
kinachoelezwa kama kesi ya tuhuma
za ugaidi inayowakabili viongozi
wa Uamsho, pamoja na vijana wao
wanaosaidia harakati za kuelimisha
Waislam juu ya haki zao zikiwemo za
kujihusisha na mambo yenye maslahi
na nchi yao.
Katika siku hii ya Alkhamis,
Mei 21, kama kawaida, ukumbi wa
bunge ulikuwa kimya wakati Mama
Spika Anne Makinda alipomuita

Waziri Mkuu, Mheshimiwa Pinda


kukaa kizimbani ili ajibu maswali ya
wabunge. Haikuwa rahisi kujua kile
alichokiazimia mheshimiwa Sanya,
mbunge anayesifika kwa hoja nzito
anapokamata kipaza sauti. Alianza
kutoa maelezo marefu na alipogusa
hoja yenyewe ikaonekana alipolenga.
M h e s h i m i wa S a n ya a l i s e m a
masheikh wa Uam sho kutoka
Zanzibar, wanaokabiliwa na kesi ya
ugaidi wamelalamika na vyombo vya
habari vikaripoti malalamiko yao,
kunyanyaswa na kudhalilishwa na
kunyimwa haki ya kupata matibabu
ya kiwango.
Wamefanyiwa vitendo vibaya,
visivyo vya kibinaadamu ambavyo,
yeye alijizuia kuvieleza bayana,
akisema si utamaduni wa bunge
kusikia vitendo hivyo vikitajwa
ukumbini.
Mbunge Sanya ambaye kitaaluma
ni mwalimu, alisema haamini
kama serikali imeamrisha madhila
waliyokutishwa masheikh hao, na
kwa hivyo ingefaa serikali ikaanzisha
uchunguzi na kutoa tamko rasmi
bungeni.
Kwa jumla, alisema angependa
kumsikia Waziri Mkuu akitoa tamko
lililoshiba ili kuondoa hali ya hewa
isiyofaa nyoyoni mwa masheikh
wenyewe, ndugu na familia zao,
ambao wakati kesi yao inaendelea
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,
Dar es Salaam, ni haki yao haki zao
na usalama wao kuzingatiwa na
kulindwa.
Wa z i r i M k u u P i n d a k a m a
vile ameshushwa tu ghafla pale
bungeni kutoka kusikojulikana,
alisema haelewi hasa alichokusudia
kukiwasilisha mbunge. Swali haliko
wazi kiasi cha kutojua vya kumjibu.
Hofu yangu ni kwamba huyu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya zaidi
ya watu 45 milioni anajishusha, kwa

kiasi cha kutisha. Haiyumkiniki


kiongozi wa hadhi aliyo, asijue
masuala makubwa yanayohusu
wananchi anaowaongoza kama hili
la masheikh.
Eti hajui kwamba kuna masheikh
kutoka Zanzibar wanashitakiwa kesi
ya ugaidi. Hajui masheikh wapatao
20 wanafikishwa mahakamani kila
baada ya wiki mbili wakifuatilia
kesi iliyofunguliwa zaidi ya mwaka
sasa. Hajui kesi yao inaendelea
kwa hatua ipi wala hajui kama
masheikh hao wako rumande au vipi.
Hajui. Anahitaji aulize watu aliosema
wenzangu wamueleze suala hilo
likoje.
Nini maana ya kauli hii? Ni
kwamba akawaulize wenzake, ambao
tuseme ni watumishi wa serikali,
wasaidizi wake kikazi, kwamba hivi
kuna masheikh wangapi, majina yao
nani na nani, mitaa yao na familia
zao ni zipi!
Akawaulize wasaidizi wake hao,
kwamba masheikh hao walikamatwa
lini, maana hajui kama wengi wao
walifuatwa majumbani mwao usiku
wa manane; aulize walikamatwa
na nani; kama wanatoka Zanzibar,
walifikaje Dar es Salaam; kama
Dar, ni ofisa gani aliamuru walale
wanapolala.
Awaulize wasaidizi wake kwani
wale masheikh wa Uamsho na sina
shaka itabidi pia Pinda awaulize
wasaidizi wake hii Uamsho ni kitu
gani na madhumuni yake hasa ni
nini wanalalamika nini na nini
mahakamani. Inasikitisha Waziri
Mkuu hana khabari kamwe kuwa
masheikh hao, wametangaza kuanza
mgomo wa kula ifikapo Juni mosi.
Masheikh hawa kesi yao haiendi,
juzi tu wakili wa serikali aliieleza
mahkama upelelezi wa kesi
haujakamilika na kesi Jumatatu
wiki hii iliitwa kwa ajili ya kutajwa.
Aliomba hakimu apange siku
nyingine ya kuja kuitaja kesi.
Masheikh wamekuwa
wakilalamika kuwa walipigwa na
hawajapata tiba nzuri, kiasi cha
baadhi yao kuoza maeneo waliyopata
majeraha. Wamelalamika baadhi yao
kudhalilishwa kimaumbile. Waziri
Mkuu anasema kuna utaratibu wa
mahabusu kupatiwa tiba kule ndani.
Sasa kwa haya, ndiyo maana
nikasema huyu Waziri Mkuu Pinda
amefika pabaya. Huyu ndiye Waziri
Mkuu aliyepo begani kwa Rais Jakaya
Kikwete. Tena, cha kushangaza zaidi,
huyu mwanasiasa, mwanasheria
huyu, aliyeishi Ikulu kama mtumishi
kwa miaka mingi, anataka kugombea
urais. Urais upi jamani?
Inahitaji kipawa kweli kwa
kiongozi wa hadhi yake kusubiri
mwaka mzima kujua kama kadhia
ya masheikh wa Zanzibar ndiyo ile
vijana wanaita khabari ya mjini
kwa Wazanzibari, hasa wapenda
mabadiliko. Hajui na anataka kuuliza
wenzake.
Kipimo cha uwezo wa mtu katika
kuongoza ni staili yake ya uongozi.
Bali kwa hulka anayoionesha Waziri
Mkuu Pinda bungeni, tena wakati
akijibu maswali ya wabunge wenzake,
wawakilishi wa wananchi, wengi
hatupati picha!

10

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Ijuwe hakika ya Msikiti wa Alaqsa


Na Hamzah Z. Rijaal

QUBBA au kama kwa


Kizungu ijulikanalo
kwa jina la Dome of
t h e r o c k , i l i j e n g wa
mwaka wa 687 C.E na
Kiongozi wa Kiislamu
Abd al-Malik ikiwa ni
kama miaka 50 baada ya
kufa kwa Bwana Mtume
Muhammad S.A.W. Jabali
hilo ni sehemu muhimu
kwani hapo ndipo Bwana
Mtume Muhammad
S.A.W alipoanzia safari ya
Miraji kama inavyoelezwa
kwenye Sura ya 17:1.
Sehemu hii ina umuhimu
mkubwa kwani ni alama
ya kuunganisha umoja wa
wanadamu kutokana na
baba wa Mitume Mtume
Ibrahim (A.S). kwa kifupi
sehemu hii ni muhimu
kwa Waislam, Wakiristo
na Mayahudi.
Qubba ni moja katika
sanaa kubwa ya kifundi
a m b a y o Wa i s l a m u
walifanikiwa katika
ujenzi huo wa msikiti, na
alikuwa Sayyidna Umar
Bin Khatab aliyelijenga
mwanzo msikiti huo kwa
mbao ikiwa kama alama ya
kuunganisha waumini na
alipokuja kiongozi Abd alMalik ndio yeye aliyeweza
kulijenga jengo hili lenye
kivutio kikubwa.

Kizungu Mkuti Cha Baytil


Muqadas
Kutoelewa kwa
Waislamu walio wengi
ni upi Msikiti ujulikanao
kama Kubati Sakhra
na upi Msikiti wa Al
Aqsa, kunaleta mashaka
m a k u b wa n a k u t o wa
ushindi kwa maadui wa
Waislamu. Kutoelewa huku
kunatokana na juhudi nzito
na za makusudi ambazo
zinafanywa na Mayahudi
kupotosha ukweli ili lengo
kuu walilolikusudia la
kutaka kuuvunja Msikiti
wa Alaqsa ufanikiwe na
kujenga hekalu ambalo
eti wao wanasema kuwa
pahali palipo msikiti wa
Qubati Sakhra ndipo
alipoweka Msikiti Mtume
Suleyman (A.S).
Kwa kweli kama
nilivyotangulia hapo mbele

PICHA juu Msikiti wa Al Aqsa uliopo Jerusalem. Qubba (Dome of the Rock)

kusema kuwa Msikiti wa


Qubati Sakhra ni moja
ya kazi nzito ya ufundi wa
hali ya juu iliyofanywa

na Waislamu, na Msikiti
huo unaonekana
mnara wake wa rangi
ya dhahabu yenye
kupendeza kabisa. Sasa
Wayahudi mbinu zao
kubwa ni kuufanya
Msikiti huo uwe ndio
Msikiti wa Alaqsa na
ufahamike hivyo kwa
dunia nzima, ikiwa mie
na wewe vile vile tujuwe
hivyo.
M t e g o
h u o
umetuangukia na utaona
hata post card nyingi
zenye kutengenezwa na
Waislamu hutoa picha
ya msikiti wa Qubat

S a k h r a b a d a l a ya
Msikiti wa Al Aqsa.
Katika kipindi
ambacho Kiongozi wa
ki-Palestina Yasir Arafat
amezungukwa na kabla
ya kupewa uhuru wake
wakuondoka huko
Ramallah, television
nyingi duniani ikiwa
pamoja na za nchi za
Kiislamu zimekuwa
zikionyesha Msikiti
wa Qubat Sakhra
na kutoonyesha Qibla
cha mwanzo ambacho
Waislamu katika zama
za Mtume Muhammad
S . A . W wa l i p o k u wa
wakielekea nacho ni
Msikiti wa Al Aqsa. Huu
ni upotoshaji na kuna
haja kwa kila Muislamu

kuuelewa ukweli na
baada ya kuufahamu
ukweli akamfahamisha
mwenzake na kujuwa
hakika ni upi Msikiti wa
Al Aqsa na umuhimu
wake.
Wachache ndio wenye
kuelewa juu ya uhakika
wa Msikiti wa Al Aqsa na
ukweli ulivyo. Waislamu
wamepotezwa na
wamepotea na mara tu
M ayahudi watapotaka
kuitekeleza azma yao iliyo
ovu ya kuubomoa msikiti
wa Al Aqsa, Waislamu
wataona kuwa Msikiti wa
Al Aqsa upo na nini tena
cha kupiga kelele?
Hivi karibuni Wayahudi
wenye misimamo mikali
walikuwa na azma ya

kutaka kuuharibu na
kuubomoa Msikiti wa
Alaqsa lakini juhudi hizo
ziliweza kugundulikana
na mapema na vijana
shupavu wa Kiislamu
waliojitolea kupambana
na udhalimu na uharamia
wa Mayahudi wenye siasa
kali na kuweza kufanikiwa
kuizima dhana nzima ya
ufisadi huo.
Jambo
ambalo
lakusikitisha habari hii
ya k u t a k a k u v u n j wa
kwa msikiti wa Al Aqsa
haijaelezwa na vyombo
vya habari vya Magharibi
a m b a v y o n d i o wa t o a
habari wakuu na wenye
propaganda duniani kote.
La kushukuriwa ni kuwa
sio haba Waislamu nao
wameingia na kufanya
kazi katika Tekenolojia
ya habari Information
Technology na moja ya
mashirika ya Kiislamu
lilokuwa mstari wa
mbele kuzieleza habari
hizi ni International
Islamic News Agency.
Tutahitajika tufanye kazi
kubwa ya kuelimishana na
kuamshana juu ya khatari
iliyopo duniani kote katika
kuupiga vita vya dhahiri
na vya nadharia Uislamu
ili uwe dhaifu kama ulivyo
hivi sasa Ukoministi. La
kuwazindua maadui
hao ni kuwaambia kuwa
jitahada zao ni kubwa
lakini Allah ameahidi
kuwa ataulinda Uislamu na
ndio maana juhudi nyingi
zifanyazwo kuuangamiza
Uislamu unashindikana
n a h a u t a f a n i k i wa n a
matokeo yake kila kukicha
kunaonekana Uislamu
kuweza kupata nguvu.
Kutoka tokeo la
September 11 na
kuangushwa kwa serekali
ya Ta l i b a n ! t a k w i m u
zilizokuwa bado
hazijathibitishwa lakini ni
zenye kuaminika ni kuwa
zaidi ya watu nusu milioni
duniani kote wamesilimu
na hili ni tokeo kubwa kwa
watu wengi kuukubali
Uislamu kwa mara moja
tangu zama za Bwana
Mtume Muhammad
S.A.W.
Ewe Mola tufungulie
yalio ya haki na haki
tuijuwe na batil tuielewe
na tuiepuke AMIN

11

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Mafundisho ya Quran

Fethullah-Gulen
WANAFIKI wametajwa
katika Quran kwamba
wa o : H a l i ya k u wa
wanayumba kati ya hilo
hawahusiki na hawa na
hawahusiki na hawa.
[A-Nisaa 143].
Maana wanayumba kati
ya waumini na kati ya
makafiri. Mara utawaona
huku na mara utawaona
huko wanasumbuwana na

WAARABU walitokana
na Nabii Ismail na
Wayahudi walitokana na
Nabii Is-haq. Kwa hiyo
Waarabu ni mabinamu
wa Wayahudi. Isikize
Biblia inavyotuambia juu
ya ndugu hawa-Waarabu
na Wayahudi:
Yale maji, ambayo
Ibrahimu alimuachia
Hajiri (Hagar) na mwana
wao Ishmaeli yakaisha
katika kiriba, akamlaza
kijana (Ishmaeli) chini
ya kijiti kimoja. (Hajiri)
Akaenda akakaa
akimkabili (Ishmael) mbali
naye kadiri ya mtupo wa
mshale, maana (Hajiri)
alisema, Nisimwone kijana
(lshmaeli) akifa (kwa kiu),
naye akakaa akimkabili,
akapaza sauti yake, akalia.
Mungu akasikia sauti ya
kijana (Ishmaeli). Malaika
wa Mungu akamwita
Hajiri kutoka mbinguni,
akamwambia una nini
Hajiri? Usiogope, maana
Mungu amesikia sauti ya
kijana (Ishmaeli) huko
aliko (Ewe Hajiri, hebu)
Ondoka ukamwinue kijana
(Ishmaeli), ukamshike
mikononi mwako, Kwa
kuwa nitamfanya kuwa
taifa kubwa (la Waarabu).
Mungu akamfumbua
m a c h o , n a ye a k a o n a
kisima cha maji (Zamzam)
akaenda akakijaza kiriba
maji, akamnywesha
kijana. Mungu akawa
pamoja na huyo kijana

kunyimwa mwangaza wa
macho yao na mwangaza
wa hisia zao na kuelewa
kwao. Kisha kwa hakika
wao kwa sababu ya kuwa
kwao wanadhani kwamba
maisha yamethibitika
katika maisha haya ya
dunia, tunawaona wamo
katika joto la kubobea juu
ya ladha za hii dunia.
Kwa hiyo, kuamini na
kukufuru kuko sawasawa
mbele zao. Mahali popote
ambapo starehe na
maisha laini yenye raha
yanapatikana, wanafiki
wa t a k we n d a k w e n y e
m a i s h a h a y o . Wa k a t i
wanapoona kwamba
maslaha yao yamo
katika kwenda Msikitini,
wanakwenda msikitini (Ila)
Na pindi wanaposimama
kwenda kwenye swala,
wanasimama hali ya kuwa
wavivu wanawaonyesha
watu. [A-Nisaa 143].

Maana ni kwamba wao


wanayadumisha maisha
yao kwa namna yoyote.
Hivyo katika Uislamu
wanazichukua sehemu
zao nyuma ya mjumbe
wa Mwenyezi Mungu

(S.A.W.) isipokuwa kwa


macho yaliyo mapofu,
yasiyoona na kwa nyoyo
zenye kiza na kwa fikra
i s i y o k u wa n a i m a n i ,
ukweli na ikhlasi. Maana
kurudi kwao utupu kuliko

Nabii aliyekuwa akingojewa


Zisemavyo Taurati na Zaburi

(Ishmaeli), naye akakua,


akakaa katika jangwa,
akawa mpiga upinde.
(Ishmael) Akakaa katika
jangwa la Parani, mama
yake (Hajiri = HaJara =
Hagar) akamtwalia mke
katika nchi ya Misri.
(Mwanzo 21: 15-21)
Na k ama t u ju a v y o,
kisima cha Zamzam pia
kiko katika eneo lile la
Parani (yaani kule Makka),
kama ilivyosema Quran:
M o l a we t u M l e z i !
Hakika mimi nimewaweka
baadhi ya dhuriya zangu
(Hajara na Ismaili) katika
bonde (hili la Makka) lisilo
kuwa na mimea, kwenye
Nyumba yako Takatifu
(ya Al- Kaaba), ewe Mola
wetu Mlezi, ili washike
swala. Basi zijaalie nyojo
za watu zielekee kwao,
na waruzuku matunda,
ili wapate kushukuru.
(Surar Ibrahim, 14:37)
Ni kwa sababu ya tabiri
za dhahiri kama hizi
hata ndani ya Taurati (ya
watu wa Kitabu, yaani
Mayahudi na Wakristo),
ndiyo Mayahudi walimjua
na kumtazamia kuja Nabii
wa Mwisho, na wakajua
kwamba atatokea kule
Parani, yaani Makka. l

Aya ya Kumbukumbu
la Torati (Deuteronomy)isemayo:
Naye
(Musa)
alikuja kutoka Sinai.
Akawaondokea kutoka
Seiri kuja kwao; Aliangaza
kutoka kilima cha Parani,
na alikuja na watakatifu
elfu kumi. Kutoka
katika mkono wake wa

kuume ilikuja sheria


motomoto kwa ajili yao.
(Kumbukumbu la Torati
33:2)
Kwa muji wa Makala ya
Kiarabu iliyopigwa chapa
jijin i L o nd o n m na m o
mwaka 1944, imeandika
kama hivi:
Deuteronomy 33:2 He
came with myriads of holy
ones, in his right hand was
an axe of fire with two
edges.

kukubwa sana na ubaya


wa bahati yao yanajengeka
hayo katika kutokuwa na
ikhlasi na ni kama hivyo
Quran tukufu inatumia
katika kuwaelezea mifano
ya hawa kwamba wao
Hawarudi maana
hawarejei kwenye haki
na kwenye hakika. Na
hawarejei kwenye
tabia ya maumbile yao,
yaliyosalimika.
Kutokana na msingi huu,
tunaona katika sifa zao
ambazo zimekuja katika
surat Al-Munafikiqoun
kwamba wao Hawajui
(hawafahamu) isipokuwa
haziji katika haki yao.
Sifa zilizo katika mifano
ya (hawelewi) au
(hawafikiri) kwa sababu
sifa hizi zinafungamana na
kutokuamini.
(Imenukuliwa kutoka
Kitabu: Miyangaza ya
Quran katika mbingu
ya hisia, cha Muhammad
Fethullah Gullen
kilichotafsiriwa kwa
Kiswahili na Sheikh
Suleiman Amran
Kilemile)

Ambayo maana yake


kwa Kiswahili ni kama hii
ifuatavyo:
Alikuja na watakatifu
wengi (maswahaba); na
katika mkono wake wa
kuume akiwa na shoka
(Jambia) lenye ncha mbili.
(Kumbukumbu la Torati
33:2)
Aya hii inaongea juu
ya Nabii aliyetabiriwa
ambae atakuwa na
Maswahaba wengi ambao
ni watakatifu sana, na
ataruhusiwa, ataamriwa
kupigana na maadui zake
wakimchokoza.

MCHANGO WA UJENZI WA MSIKITI

Waislamu wa Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Mkuranga


, Kitongoji cha Mlamleni , Kijiji cha Kimbangulile
wanaomba kujengewa Msikiti.
Ndugu zetu wanafanya Ibada ya Swala katika hali ngumu
kama inavyoonekana katika picha.
Ukiwa Umeguswa na hili tunaomba MCHANGO WAKO
WA VIFAA VYA UJENZI.
VIFAA VYA AWALI

1.Cement, 2.Tofali, 3.mchanga, 4.Vifaa vya


Kuchimbia Majembe, Panga , chepe N.k
Maazimio yetu tuanze Ujenzi pale tu
tutakapo pata uwezo wa kulifanya hili.
Tunawakaribisha mtembelee eneo hilo
wale ambao Mtakuwa Na Muda wa
kufanya hivyo.
Michango yenu tunaomba muwasilishe
kwa Namba ya Simu.
0 7 1 5 8 0 0 7 7 2 ( T i go Pe s a ) G H A L I B
MONERO.
+255689604780 +255689604780 AIRTELMONEY .
Kwa wale waliopo Nje ya Tanzania :
WESTERN UNION : GHALIB NASSOR
MONERO
Waliopo KENYA tafadhali wasiliana /
Wasilisha kwa ALI BAJIY NASOR no'
0725113783 M-PESA.
Taarifa zaidi kuhusu Michango ya Msikiti
huu Tafadhali Tutembelee : facebook
: Kijana wa Kiislam Dsm or Whatssap
Number : +255689604780 +255689604780
Au P i g a S i m u : + 2 5 5 7 1 5 8 0 0 7 7 2
+255715800772

12

Tangazo/MASHAIRI

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

KHATMA YA MAFATANI

Naanza kuwasalimu, Bara na Zanjibariya,


SALAMU ALAYKUMU, wa biladi na kariya,
Walaykumu salamu, mjibu natarajiya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.

Kwa jaha na taadhimu, baada yayo tahiya,


Namhimidi QAYYUMU, KHALIQUL-BASHARIYA,
Thuma swala na salamu, kwake khairu bariya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Fitna tangu kadimu, si jambo zuri ni baya,
Lahilikisha kaumu, japo kadiri ya woya,
Kwa wa kwake uhujumu, afadhali ya manaya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
BAQARA yatulazimu, sura ya pili kuuya,
Yuatujuza ALIMU, ndani kwa thineni aya,
Kuzidhukuru muhimu, kwa huba na si kwa maya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Moja tisa moja dumu, bukurata wa ashiya,
Mbili moja saba kumu, kuidurusu sawiya,
Swadaqallahul-adhimu, kwazo fitna i mbaya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Kitatangewe rajimu, shetani mwanahizaya,
Yu jini na binadamu, ALLAH ashatuambiya,
Soma upate 'fahamu, SURATUN-NASI Makiyya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Mafatani mlizamu, wa fitna kutapaya,
Kwa ndimizo masmumu, hueneza zao puya,
Lengolo kutukasimu, tubaki kuwayawaya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Kawimu tusitakimu, kupembua zao chuya,
Kwalo tusipojihimu, kweli tutawayawaya,
Na mwisho kujilaumu, kwa kutofikia ghaya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Akitujia dhalimu, nayo yoyote hekaya,
Kuichungua muhimu, kwa ya HUJURATI aya,
Si kuja kujilaumu, mwisho kwa ujahiliya,
Khatma yao fedheha, duniani na akhera.
Kaditamati nudhumu, ya indhari si ghinaya,
Fitnani kwa kudumu, duniani ni udhiya,
Kadhalika jahanamu, khatma yake hawiya,
Naweka chini kalamu, yenye wino wa hidaya.
ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.

GHURURI YA 'VUNJAJUNGU'

Ni ada kwa kila mwaka, si Bara si Visiwani, '


Vunjajungu' kunadika, karibu na Ramadhani,
Bilhaki yanishika, shaka kwalo mtimani,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.

Dhahiria hunadika, kwa nderemo pasi soni,


Kasiye hasa hushika, mwezi huu wa Shabani,
Kwa ilani kurushika, yalo jungu mavyomboni,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Chombezole husikika, kwa lahani redioni,
Kadhalika hupambika, kwa suwari runingani,
Mwishowe huandikika, kwa hati magazetini,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Jungulo kwa uhakika, ni husuni ya shetani,
Ndanimwe hujumuika, watovu kwa RAHMANI,
Kinyume hutambulika, watiifu wa shetani,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Rajimu husururika, kwa insi kuwazaini,
Wapate kughururika, na kudakhili junguni,
Kwa jungu kusharifika, lengo la funga shakani,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Si geni latambulika, BAQARA kadurusuni,
Muhali kwalo kufika, kwa wafunga Ramadhani,
Jungu wasoliepuka, kwa ndanimwe kusakini,
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Mayaza kukithirika, ya jungu adhimu nduni,
Kucha kutwa hunadika, hata kuchwapo jioni,
Funga kutangulizika, kwa maasi lengo nini?
Ebu tuiepukeni, ghilba ya 'vunjajungu'.
Kituo leo naweka, kidogo si cha mwishoni,
Kwani bado sijafika, mwisho enyi ikhiwani,
Kwa kathiri kumulika, wiki kesho karibuni,
Shime tujitanibuni, na baa la 'vunjajungu'.
ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.

TAMASHA LA KITAIFA
ILONGO MBEYA
05 12 JUNI , 2015

Waislamu wote nchini mnaalikwa kuhudhuria


Tamasha la Ujenzi wa Kituo cha Kiislamu Ilongo
Mbeya litakalofanyika kuanzia tarehe 05, 12
Juni, 2015.
Shime Waislamu tujitahidi kuhudhuria kwa
wingi. Wasio na wasaa wa kuhudhuria wachangie
fedha na vifaa vya ujenzi.
Tukumbuke, tukifanya hivyo tutakuwa tumefanya
biashara na Allah (s.w) kwa mafanikio ya hapa
duniani na malipo ya Pepo Quran (61:10-13)
Usafiri / Gharama:
Kutokana na Miundombinu ya barabara kwa
sasa kila mkoa utaratibu safari ya Mbeya kupitia
Maamir wa Mikoa
Kwa kupitia Dar es Salaam nauli ni Tshs. 70,000/kwenda na kurudi Dar. Kuripoti Dar es Salam ni
tarehe 04/06/2015 (0689665045/0713 992395).
Kipindi hiki Mkoa wa Mbeya una baridi, hivyo
wanatamasha waje na nguo za kuzuia baridi.
Wabillah Tawfiiq
AMIR TAIFA

13

MAKALA

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Propaganda za udini shuleni Tanzania-5

Inatoka Uk. 7
waliokuwa Bara wala
kuwasafirisha kutoka
Bara ndani mpaka pwani
wala kuwa madalali wa
biashara ya watumwa. Wao
walichokifanya ni kununua
watumwa walioletwa na
Waafrika kutoka Bara kwa
ajili ya kulima mashamba
ya mikarafuu, na kuelezea
ukweli ni Waarabu wachache
wa l i o m i l i k i m a s h a m b a
hayo. Wengi wao, kama
tulivyoonesha kabla,
walikuwa watu wa kawaida
waliokuwa wakipigana na
maisha na hadi kufanya kazi
ngumu pia.
Picha hii ya pili inaonesha
kuwa muuzaji, wamiliki na
wanunuzi wa watumwa ni
Waarabu Waislamu:
Tukiweka upande kuwa
hayo mavazi waliyovishwa
hao Waarabu pichani si ya
wale waliokuweko Afrika
M a s h a r i k i , ya a n i s i ya
Wayemen na Waomani.
Inasikitisha kuona jinsi
vile propaganda za udini
na chuki za waandishi na
mchoraji zilivyowapelekea
hata kuwafanya kuwa vipofu
wasione ukweli na haki. Soko
gani la utumwa katika Afrika
Mashariki lililokuwa lina
Waarabu peke yao ambao
ni wamiliki, madalali na

wanunuzi wa watumwa?
Wanataka kumdanganya
nani leo kuwa Waafrika na
wengineo hawakuwemo?
Wanataka kumdanganya
nani isipokuwa masikini
watoto wadogo wa shule,
kuwa wanunuzi wa
watumwa wakati ilipokuwa
ikifanywa biashara hiyo
walikuwa Waarabu peke
yao? Ukweli ni kuwa biashara
hiyo iliwagusa wachache
kutokana na makabila karibu
yote yaliyokuwa yakiishi
Z a n z i b a r n a P wa n i ya
Afrika Mashariki, wakati
ule wakiwemo Wazungu,
Wahindi, Waarabu, Waafrika,
Washirazi na kadhalika.
Jonathon Glassman ametuelezea:
Tafsiri: Zaidi ya hivyo,
v y o v y o t e v i l e u t u m wa
katika Zanzibar ulivyokuwa
ukionekana wakati wowote
ule, kulikuwa hakuna
chochote kile kinachoufanya
kuwa ni wa Kiarabu,
wamiliki wengi wa Watumwa
walikuwa Waafrika.
Akaongeza:
Ta f s i r i : K wa m a n e n o
mengine, kinyume na historia
za kigozi za Utumwa wa
Kiarabu ambao ulilenga
khasa kuondosha utumwa,
we n g i wa wa m i l i k i wa
watumwa walikuwa hawana

kabisa asili ya Mashariki ya


Kati.
Yaani, walikuwa hawana
asili ya Kiarabu, na fikra hizo
zenye lengo la kuwalaumu
Waarabu na Waswahili peke
yao ziliingizwa wakati wa
siasa za kimishinari kutaka
kuwapaka uchafu Waarabu
na Waswahili kwa lengo
la kuutweza Uislamu.
Kaandika pia Edward A.
Alpers:
Tafsiri: Katika nusu ya
mwanzo ya karne ya kumi
na tisa Afrika Mashariki
iliongezeka harakati za
biashara ya utumwa.
K a t i k a m wa m b a o w o t e
haja ya kumiliki watumwa
ilizidi kuongezeka, kwa
kuwa Waarabu, Wabrazili,
Wafaransa, wafanya biashara
ya utumwa wa Kispaniola
kutoka Kuba na Wamerekani
walipoigundua Afrika
Mashariki wakati ambao
ulianzishwa harakati za
Kiingereza za kuzuia utumwa
katika Afrika Magharibi.
Iangalie tena picha
iliyotangulia iliyochorwa
na mtu aliyejitosa katika
propaganda kali za udini
ikisha ilinganishe na maneno
yaliyozungumzwa na
wana-historia wa kweli wa
Kizungu na pia uilinganishe
na picha iliyochorwa kwa

m u j i b u wa m a e l e z o ya
Stanley. Jiulize: Kwa nini
mchoraji hakuwaonesha
wauzaji na wanunuzi wa
Kiafrika na wanunuzi wa
makabila mengine? Kwanini
wakamataji/wamiliki,
madalali na wanunuzi wote
wawe ni Waarabu tu peke
yao?
Ni muhali katika
soko la nchi ambalo lina
mchanganyiko wa makabila
mbalimbali sokoni pale
upate watu wa aina moja tu,
hapo juu tunaona watumwa
ni Waafrika, muuzaji ni
Mwarabu, dalali ni Mwarabu,
na wanunuzi ni Waarabu
hii haiingi akilini. Lakini
kuchora yanayoingia akilini
si shabaha ya wenye lengo lao
lisilokhusiana na kuelezea ya
kweli, na hawa ni pamoja na
wafuasi wao ambao hurejelea
propaganda kikasuku bila
ya k u p i m a u k we l i u k o
wapi na bila ya kutumia
akili zao na bila ya kutumia
uadilifu. Madam hadafu yao
inawaelekeza kuwanyooshea
kidole cha lawama Waarabu
Wa i s l a m u p e k e ya o i l i
walifikie lengo lao, basi
hivyo ndivyo wafanyavyo,
na potelea mbali iwapo
wanaunyonga ukweli na
harufu ya mzoga wa uwongo
ikaenea ulimwenguni.

L e n g o l a o wa a n d i s h i
na wachoraji wameliweka
wazi wenyewe na lengo
hilo si kuelezea au kuchora
yaliyokuwa ya kweli, bali
kutapakaza propaganda
za chuki. Ukweli huingia
akilini katika bongo za wenye
kutumia akili zao. Utapakazaji
wa chuki hutokana na wale
wasioipendelea nchi yao
wema na salama kwani chuki
mwisho wake ni khasama na
uvurugaji wa nchi. Tanzania
leo ina matatizo mapevu na
mivutano ya siasa mbovu
za udini inayotokana na
propaganda chafu kama
hizo zenye kupalilia
mtafaruku. Sidhani kama
kuna Mwislamu yoyote leo
atakayekubali mwanawe
asomeshwe shuleni kuwa
ni wavyele wake tu ndio
waliofanya kila ovu kuanzia
ukamataji wa wanyonge
wa Kiafrika Bara, kuwauwa
idadi kubwa ya wanyonge
hao, kuwafunga minyonyoro,
kuwapakia pembe nzito za
ndovu, na wanapokhalifu
a m r i k u wa p i g a m b o k o ,
kuwaendesha kwa miguu
m p a k a p wa n i , k u wa t i a
mnadani, kuwauza
n a k u wa s a f i r i s h a n c h i
mbalimbali.

Uchaguzi Mkuu Oktoba, ujumbe kwa Waislamu!

Inatoka Uk. 8
ulioshindwa kuwasaidia kwa
miaka mingi, basi wanatafuta
mbadala wake, lakini cha
ajabu baadhi ya Waislamu
wanaotumikia mfumo huo,
b a d o wa n a u r e m b a k wa
Waislamu mfumo ule ule
uliowaangusha! Mfumo
ambao wanajua unapiga vita
Uislamu!
Na nukta ya mwisho,
ningependa kuangazia
zaidi ushiriki wetu katika
siasa kama Waislamu na
maadili ya dini yetu. Baadhi
ya Waislamu wanaamini
k wa m b a u s h i r i k i we t u
kwenye mfumo wa siasa za
kisekula utatuletea manufaa,
ikiwa ni pamoja na kusaidia
kuondoa chuki iliyojengeka
dhidi ya Uislamu. Hawa
wako tayari hata kuvuka
mstari mwekundu na kuunga
mkono Ilani za vyama vya
kisekula kwa matumaini
hewa kwamba jamii ya
Waislamu inaweza kunufaika,
ingawa wanafahamu vizuri
kwamba vyama hivyo
vinapinga Uislamu kwa
asilimia mia moja. Ndugu
zangu katika Imani, si tu
kwamba jambo hilo siyo

kweli, bali limewashusha


mno Waislamu na kuwafanya
kuwa ombaomba wa haki
zao kwa miaka yote hii. La
msingi zaidi kufahamu ni
kwamba kushiriki siasa kwa
kuunga mkono vyama hivyo,
siyo jambo linalokubalika
m o j a k wa m o j a k a t i k a
Uislamu, kwa sababu vyama
hivyo vinasambaza wito
unaopingana na Aqeeda ya
Kiislamu.
Mwenyezi Mungu
anasema: Sema: Mimi
nimekatazwa kuwaabudu
wale mnaowaabudu
kinyume cha Mwenyezi
Mungu (peke yake) Sema:
Sifuati matamanio yenu,
maana hapo nitapotea na
sitakuwa miongoni mwa
walioongoka Qur(6:56).
Kuna case studies
nyingi tu zinazoonyesha
Waislamu, bila ya kushiriki
kwenye michakato ya siasa
za kisekula, wameweza
kuanzisha na kuendesha
shughuli zao zinazolinda
maslahi yao ya Kiislamu,
kwa kuzingatia zaidi
misingi ya kujitegemea wao
wenyewe. Waislamu hapa
nchini wameweza kujenga
na kuendesha shule zao

kwa nguvu zao wenyewe,


baada ya kuona mfumo wa
Elimu wa taifa unawabagua.
Wamepiga kelele sana, lakini
walipogundua kuwa mlango
wa siasa ni mgumu, kwa
sababu msingi wenyewe
u l i o j e n g e wa s i a s a h i z o
(usekula) hautaki Waislamu,
basi wakachukua hatua
sahihi. Sasa shule zipo na
watoto wetu wanasoma kwa
maadili yetu!
Waislamu nchini Tanzania,
bila ya kushiriki michakato
ya siasa za kisekula,
wameweza kuanzisha
taasisi zao huru, ambazo
zinasimamia kiukweli
maslahi yao. Waligundua
kwamba kuendelea
kulalamikia BAKWATA,
ambalo hawakuliunda wao ni
kupoteza wakati. Wakaunda
Taasisi zao wenyewe na
zinafanyakazi vizuri tu, licha
ya kuwepo changamoto za
hapa na pale.
Waislamu pia wamejenga
Misikiti, wameanzisha vituo
vya afya, wameanzisha
vyombo vya habari vyenye
heshima, ambavyo vinatetea
na kulinda maslahi yao,
bila ya kuingia kwenye
mchakato wa kisiasa wa

kisekula. Mbona mambo


haya yanawezekana tu watu
mkijipanga!!
Ndugu zangu katika Imani
naomba muwe makini sana.
Huu ni mwaka wa uchaguzi.
Kuna watu katika mfumo
huu wa utawala, ambao
unawabagua Waislamu,
wanawinda kura zenu kwa
udi na uvumba, ili maslahi
yao binafsi yaendelee
kudumu. Hao ni walaghai
tu na maadui zetu. Tangu lini
mfumo wa siasa wa Tanzania
ukawasaidia Waislamu!?
Tu s i i n g i z w e k w e n y e
mijadala ya watu
wa n a o j i f a n ya we n z e t u ,
kumbe ni mawakala wa
mfumo unaotukandamiza.
Tusilazimishwe kulegeza
misimamo ya Dini yetu, kwa
matarajio ya kupata manufaa
h e wa . L a z i m a J a m i i ya
Waislamu, kama kipaumbele
chake cha kwanza, itekeleze
Uislamu kwa kujiamini, licha
ya mitazamo hasi dhidi ya
Uislamu inayojengwa na
vyombo vya habari.
Tutaweza tu kupambana
na uongo na dhana potofu
dhidi ya Uislamu, iwapo tu
tutaufanya Uislamu kuwa
ajenda yetu kuu na kufuata

njia ya kisiasa inayokubaliana


na maadili yake, badala ya
kujikomba kwa watawala
na kuwamwagia sifa
wa s i z o s t a h i l i . H a wa n i
wanasiasa waovu ambao
wamewatumia Waislamu
k a m a n g a z i ya k u f i k i a
malengo yao binafsi ya
kisiasa.
Kwa kumalizia, niwausie
Wa i s l a m u h a p a n c h i n i
kushikamana na maadili
ya Kiislamu na kufuata njia
ya kisiasa iliyoelekezwa na
Uislamu - kuamrisha mema
na kukemea maovu. Tulinde
umoja wetu na tukatae kabisa
ahadi hewa tunazopewa na
wanasiasa kwa gharama
ya kupoteza Dini yetu.
Heshima na Izzah ya jamii
yetu inatokana na Uislamu.
Tukipoteza Uislamu wetu
kwa sababu ya ujinga tu,
hakuna shughuli yoyote ya
kisiasa itakayoweza kutuletea
matokeo ya maana, kama
alivyobainisha Mwenyezi
Mungu:
Wa l a m s i w a t e g e m e e
(mkawa pamoja nao)
wale wanaodhulumu;
usije ukaguseni Moto. Na
hamtakuwa na mlinzi mbele
ya Mwenyezi Mungu; kisha
nyinyi hamtasaidiwa (na
yeyote huko) Qur (11:113)

14

Makala

Mchango wa Waislmau katika maendeleo ya Dunia - 13


Abu Nasr Al-Farabi

Na Ben Rijal
Na Ben Rijal
ABU Nasr Muhammad
al- Farabi ni katika
vigogo wa Kiislamu
aliotopea katika
ilimu katika karne
ya tisa. Alikuwa
g w i j i wa k u e l e wa
lugha mbalimbali
na ndio aliosaidia
kueleweka nadharia
za Wanafalsafa wa
K i y u n a n i Pl a t o n a
Aristotle katika
ulimwengu wa
Kiislamu. Aidha ni
Al-Farabi aliompa
mvuto mkubwa
gwiji mwengine wa
Kiislamu kwa jina Ibn
Sina.
A l i ya f a n z i a k a z i
kubwa falsafa za
Plato na Aristotle na
k u we z a k u z i p a n u a
zaidi na kuweka fikra
zake. Kutokana na
umahiri wake wa ilimu
ya Falsafa, akaitwa
jina la utani Mallime-Sani ikimaanisha ni
anayofwatia bada ya
Plato na Aristotle.
Al-Farabi alizaliwa
mwaka wa 870 ikiwa ni
karne ya 8 na kufariki
mwaka wa 950 ikiwa ni
karne ya 10. Al-Farabi
alifanya kazi nzito
katika uga wa Falsafa,
lakini bahati mbaya jina
lake halikungaa kama
lilivyokuja kungaa
jina la Ibn Sina ambaye
gwiji huyu Ibn Sina
alimsoma vya kutosha
Al-Farabi na kujaribu
kuzifwata nyayo zake.
Al-Farabi katika ilimu
ambazo akizichezea
na kuzisarifu ilikuwa
falsafa, mantiki na

Abu Nasr Al-Farabi


muziki. Wakisema kuwa
anapopiga kinanda
al-Farabi ataweza
k u p i g a m t i n d o wa
kukutia huzuni, furaha,
kufikiri mbali na hata
kukuhamasisha. Na
waliosoma maandishi
ya k e , wa l i s t a a j a b u
kuona
namna
alivyokuwa anaandika
juu ya muziki.
Bahati mbaya alFarabi hajajiandika
kuhusu maisha yake na
kwa kifupi walijitokeza
watu kumuandika
na taarifa zake. Sasa
nyengine zinaongezewa
chumvi. Al-Farabi
alilewa na maandishi
ya Aristole na kutumia
mtindo wa Aristole
katika uandishi wake.
Kitabu chake cha alMadina al-fadila,
kitabu hiki alikwenda
mbali mno katika
kufwata nyayo za Plato
na kuambatana na
nadharia za Napoleon
juu ya muumba. Hapa
utakuta maadishi ya
kitabu hicho yapo baina
ya Plato na Napoleon
n a Wa n a f a l s a f a wa
Kiislamu hawakuwa
wanajikurubisha sana
na maandishi yake.
Alikuja na nadharia ya
asili, maumbile, mbinu
na uchache wa uelewa
wa mwanadamu
(epistemology). Hapa
alikuja kuziunganisha
nadharia za Wanafalsafa

Fatilia
kuandama kwa Mwezi
Leo Ijumaa ni tarehe 17 Shaaban 1436

AH sawa na tarehe 5 June 2015


Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa
Ramadhani tarehe 17 June 2015
Kutoka leo Ijumaa ya tarehe 5 June, 2015
hadi kufika Ramadhani tumebakisha
siku 13

wawili wakiwa
Aristotel na Napoleon.
Kwa kuzichanganya
na kuingiza fikra zake,
ndipo waliokuja baada
yake kama Ibn Sina,
Yahya ibn 'Adi, alSijistani, al-'Amiri na alTawhidi kutekwa katika
falsafa ya Al-Farabi
mbali ya Wanafalsafa
wa Kiislamu hata gwiji
la Falsafa aliokuwa
Mkiristo wa huko Ulaya
Thomas Aquinas
Maisha yake
Jina lake khasa ni
Abu Nasr Muhammad
ibn Muhammad ibn
Tarkhan ibn Awzalagh
al-Farabi. Ingawa
baadaye Ibn Sina alikuja
kumfunika, lakini Ibn
Sina ujuzi wote kautoa
katika kumsoma AlFarabi. Ibn Sina alijaribu
kumsoma Aristotle
kuweza kufahamu juu
ya misingi ya kuhoji
na kuja na nadharia
ya falsafa ya Aristotle
ilimwia ugumu
kufahamu juu ya fani
hio (Metaphysic).
Lakini alivyosoma
maandiko ya Al-Farabi,
aliweza kuelewa kwa
urahisi kabisa. Ibn Sina
aliandika mwenyewe
juu ya maisha yake
na ndio ikapelekea
kufahamika zaidi na
maelezo juu ya maisha
ya k e k u t o k u wa n a
utata.
Al-Farabi ni kizazi
cha Mapersia. Alizaliwa
Turkestan na kuhamia
Baghdad kwenda
kujifunza lugha ya
Kiarabu na inafahamika
kuwa vitabu vyake
vyote aliviandika
akiwa yupo Baghdad.
Katika kupendelea
kujifunza na kufanya
tafiti, alisafiri na kuzuru
nchi nyingi na miji

ikiwemo Damascus,
Egypt, Harran and
Aleppo. Hapa Aleppo
kuna mengi ya kuacha
athari. Lakini Dola
Islamiyah (ISIS) kwa
sasa wanabomoa na
kuondosha alama
zote zenye athari za
Kiislamu.
A l i k u w a
akizungumza lugha
n y i n g i n a we n g i n e
wamefika kusema kuwa
zinafika hata zaidi ya 30
kitu ambacho kigumu
kuingia akilini. Juu ya
hayo katika miji yote
aliofika akakaa, basi
muda mfupi akiweza
kuzungumza lugha
ya mahala hapo.
Alipofika katika safari
zake katika mji wa
Hamdani mtawala wa
hapo baada ya kuelewa
uwezo wa kiakili na
ilimu wa Farabi, alikuja
kumfanya kuwa ndio
mtu wake wa karibu.
Maisha yake
yanaelezewa kinamna
yake, kwani hata
alivyomalizia uhai wake
wengine wanaelezea
kuwa alifariki kifo cha
kawaida na wengine
wanaelezea kuwa
alipokuwa katika safari
zake, alihujumiwa na
majambazi na kuuwawa
alipokuwa anatoka mji
wa Damascus kuelekea
Ascalon.
Baadhi ya kazi zake
ni kitabu cha muziki
cha Kitab al-musiqa
al-kabir, kitabu kizito
ambacho ndio AlFarabi ni al-Madina
al-fadila na al-Madina
al-fadila ndio yeye,
kwani bila ya kuandika
kitabu hiki, Al-Farabi
angekosa umaarufu
aliokuja kuupata na
kuzungumzwa. Kitabu
kimoja chenye vitabu
vingi ndani yake
ambacho alikiandika
ni Risala fi'l-'aql. Hiki
a l i k u wa a n a e l e z e a
juu ya ufahamu na
uhodari anaokuwa nao
mwanadamu. Kisha
akaandika kitabu juu
ya maandishi Kitab alhuruf na Kitab ihsa'
al-'ulum.
Falsafa ya siasa
Al-Farabi katika alMadina fadila hapa ndio
unamkuta anakwenda
sambamba na nadharia
za Plato. Unaposoma
Sura ya 1 hadi ya pili na
Sura ya 3 hapa unakuta
anapowachanganya
watu juu ya maelezo ya
maumbile na uongozi
uweje. Hapo anaielezea
roho inavyokuwa na
inavyomuelekeza
mtu, yeye mwenyewe.
I n a f a h a m i k a k u wa
alikuwa mtu wa
miraba minne mwenye
maguvu. Akipenda
kusoma na alikuwa na
kumbukumbu iso ya
kawaida. Akihangaika
katika Uungu na

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

kumpoteza katika
imani ya Kiislamu na
wengine, yeye na Ibn
Sina wamefika kusema
na kuwakufurisha kuwa
sio Waislamu kutokana
na maandishi yao khasa
katika Tawhid.
Katika hali ya kijamii,
Al-Farabi aliigawa jamii
katika mafungu 3, ikiwa
iliokamilika akiweka
kutokana na ukubwa
wa waliopo katika jamii
hio. Kisha akaelezea
j u u ya m i j i i l i o n a
utulivu na kupendeza.
Hapa kaandika kwa
upana juu ya miji hiyo
namna ilivyo na namna
inavyotakikana iwe.
Kisha akaandika juu
ya miji minne iliyo
ndani ya kukamatana
na rushwa. Akaielezea
miji ya wapumbavu almadina al-jahiliyya, miji
iliojaa ufuska -madina
al-fasiqa, miji iliyo na
mahaini, al-madina
al-mubaddala na miji
iliyoenda mrama almadina al-dalla.
Akafahamisha kuwa
wakaazi wa miji hio
mwishowe hupotea na
kutodhukuriwa tena.
Katika miji ya wala
rushwa, Al-Farabi
alielezea kutokana na
maandishi ya Plato na
kama utasoma nadharia
hizo, basi utaona AlFarabi maandishi yake
hayo kayaandika jana.
Al-Farabi alipendeza
sana katika ulimwengu
wa Ulaya na kupewa
mgongo na Waislamu.
M b a l i ya I b n S i n a ,
aliwaathiri nadhari zake
wasomi kama Yahya ibn
'Adi, Abu Sulayman alSijistani, Abu 'l-Hasan
Muhammad ibn Yusuf

al-'Amiri na Abu
Hayyan al-Tawhidi.
Na hao ndio waliokuja
kuita taaluma yake na
kuiweka katika Chuo
cha Al-Farabi.
Ya h y a i b n A d i
alikuwa Mkristo
anayeamini kuwa
Mungu ni mmoja.
Alikuwa kati ya
wanafunzi wa AlFarabi katika mji wa
Baghdad. Yahya alijikita
zaidi katika mantiki na
kuja kujikuta akipenda
kufahamu imani
ya kitu na siasa. AlSijistani huyu alijifunza
vya kutosha ilimu ya
mantiki kwa Al-Farabi
mpaka kushindwa
kuwatenganisha
m w a l i m u
n a
mwanafunzi.
Kwa wanafunzi
wa Falsafa, ni vyema
wakavipitia vitabu hivi
vya Al-Farabi navyo
ni: al-Madina al-fadila
(Juu ya miji na uzuri
wake) au Abu Nasr
al-Farabi's Mabadi'
Ara Ahl al-Madina alFadila. Kitabu chengine
ni Risala fi'l-'aql, Kitab
al-huruf, Kitab ihsa'
al-'ulum, Kitab almusiqa al-kabi. Vitabu
hivi vimefasiriwa kwa
Kiengereza na lugha
nyenginezo.
Waandishi wa kigeni
kama Alon, I. Black,
D, Galston, M, Netton,
I.R., wamemuandika
na kumnukuu kati
ya vitabu vyake na
kumweka juu baada ya
Plato na Aristotle.
Tafsri ya Kitab ihsa'
al-'ulum ilioandikwa
kwa lugha ya Kilatino
na Gerard wa Cremona.

UWANJA WA VIJANA - JIONGEZEE MAARIFA

CHEMSHA BONGO namba 8


6

1.Kipindi baina ya kuteremshwa Wahyi kwa mara ya


kwanza na Wahyi wa pili kilikuwa ni kipindi cha muda
gani? Miezi 2, 6, 10. Jawabu 6
2.Sahaba gani aliokuja na shauri la kuukusanya
Quran bada ya kufa Mtume SAW? Uthman, Umar,
Khalid bin Walid. Jawabu Umar
3.Surah ngapi zimetajwa kwa majina ya Wanyama na
Wadudu, Zitaje kwa Idadi na uziandike.
4.Mnyama gani alifwatana na watu wa Pangoni?
Ngamia, Mbwa, Farasi. Jawabu Mbwa
5.Mtaje Mtume Ummah wake wakifanya mapenzi
kinyume cha jinsia. Jawabu Lut
6.Katika Surat Arrahhman kalima Sura ya 57 : Kalima
Fabiayi Alai Rabikuma Tukadhibani, limerejewa mara
ngapi? 40, 31, 52 Jawabu 31
7.Ndege 100 wapo juu ya miti akapigwa risasi na
kuuliwa mmoja, Jee watabaki ndege wangapi juu ya
mti? Jawabu Habaki yoyote.
8.
9.Mpaka ulioitwa International Boundary ndio
mpaka uliokuwa na marefu makubwa duniani
wakishirikiana nchi gani na gani? Jawabu USA, Mexico
10. Nchi gani inaongoza kusafirisha muhogo
duniani? Jawabu Thailand
11. Nchi gani inaongoza kwa uzalishaji wa
muhogo duniani? Jawabu Nigeria.

15

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Ya CCM-dola na siasa za watende wao!

Na Mwandishi Maalum
WA H E N G A w a
Waswahili walipata
kusema; Watende wao,
wakitenda wenzao,
huwa mwao!
Msemo huu utakuwa
kiini cha mjadala
wangu katika makala

hii inayonisukuma
kuandika mada yenye
k i c h wa c h a h a b a r i
kinachoonekana na
kusomeka hapo juu.
Kwa nini naandika
hivi? Wacha kwanza
niwarudishe kwenye
historia fupi.
Inafahamika

UWANJA WA VIJANA
JIONGEZEE MAARIFA

Jee unajua?

1. Katika nyakati tafauti Quran


imepigwa marufuku kutotumika kabisa
katika baadhi ya nchi na ukipatikana
nayo unahukumiwa kama kesi ya Jinai.
Quran ilipigwa marufuku Urusi kuanzia
mwaka wa 1926 hadi mwaka wa 1957.
Hivi karibuni mwana siasa mmoja nchini
Uholanzi alipeleka ombi mahakamni
Quran kupigwa marufuku ilishindikana
na huku Uhispania Imran Firasat alipeleka
ombi kama hilo la kupigwa marufuku
Quran, ikashindikana.
2. Kuwa mama yake Mtume Issa
anatajwa katika Quran na kupewa Sura
kamili, ikiwa hamna kitu kama hicho
katika Babilia.
3. Nchi za Ulaya zinasemekana kuwa
uzazi unapungua kwa kasi kutokana na
wengi wawanawake kuwa matasa, hasa
katika Ulaya ya Mashariki na Urusi.
Inakisiwa kuwa ifikapo mwaka wa 2050
idadi ya wakazi wa Ulaya itapungua
kutoka watu milioni 740 iliopo sasa na
kuna na idadi ya wakazi milioni 732.
4. Zaidi ya wasichana milioni 14 wenye
umri baina ya miaka 15 na 19 wanazaa kila
mwaka kutokana na kubakwa na ndoa za
lazima.
5. Ukipanda miti kuzungusha nyumba
yako utapunguza mahitaji ya kiyoyozi (air
condition) kwa asilimia 30.
6. N i s h a t i ya u m e m e i n a we z a
kufanyika kutokana na mafuta, maji,
upepo, jua, joto la ardhini. Megawatt 600
ya gesi ya asili inaweza kutoa nishati kwa
nyumba zisopungua 220,000.
7. Mwaka wa 2012, duniani kote
inakadiriwa kuwa wanafunzi milioni 31
wa skuli za Primari walikatiza masomo
na kama wanafunzi milioni 32 wamerejea
madarasa.
8. Kutokana UNESCO kuwa idadi ya
watoto kama milioni 61 hawajaanikishwa
kujiunga na masomo ya Primari katika
mwaka wa 2010.
9. Miaka 30 iliopita nchi ya Marekani
ilikuwa ikiongoza na kutoa wanafunzi
waliosomesheka. Hivi sasa nchi ya
Marekani inashika nafasi ya 36.
10. Kutokana na malengo ya Millenium
inatakiwa ziada ya walimu milioni 2 kwa
nchi zinazoendelea.

kwamba Zanzibar kama


sehemu ya Jamhuri ya
Muungano iko chini
ya utawala wa CCM.
Ingawa kwa upande
wa Z a n z i b a r k u n a
Serikali ya Umoja wa
Kitaifa, inayoundwa na
CCM na CUF, nguvu
na mamlaka ya CCM
bado ni makubwa. Ni
makubwa kwa sababu
CCM ndio dola. Na
zaidi ya habari, CCM
ndicho chama chenye
kushika hatamu nchini.
Ndio chama chenye
kushika mpini.
Lakini pamoja na
kuwa CCM ndiyo
inayoshika mpini
wa dola, katika nchi
ya kidemokrasia,
inayojivunia amani,
utulivu na utawala
b o r a , h a i j u z u wa l a
haileti maana njema
kusema kuwa CCM
ina mamlaka au uwezo
wa kufanya itakalo,
eti tu, kwa kuwa
imeshika mpini. Hivi
sivyo, ingawa ndivyo
ilivyozoeleka katika
kipindi chote cha
miaka 50 ya CCM ikiwa
madarakani.
CCM kwa kuamini
wa m e s h i k a m p i n i ,
wamejipa mamlaka
ya kufanya watakalo,
watakavyo, kwa
watakaye, mahala na
saa watakazo. Kwa nini?
Kwa vile wamejivisha
mwavuli na magwanda
ya dola. Haya yote ni
kwa uchache tu. Ila
kwa ufupi, CCM wana
u we z o wa k u f a n ya
lolote wala lisiwe kosa
kisheria wala kikatiba.
C h a
a j a b u ,
watende wao tu,
wa k i t e n d a we n z a o
hata yasiyokuwa
mabaya, ilimradi
hayawafurahishi tu hata
kama ni ya ukweli na ni
ya haki na ya kisheria,
basi kwa wao huwa
mwao. Akitokezea mtu
au kikundi cha watu
wakafanya lolote tu
dhidi ya utashi wa CCM
jambo hilo huwa kosa
na haliwi kosa dogo.
Hii ni kana kwamba
CCM iko juu ya Sheria
kwa sababu matukio
mengi yanayofanyika
nchini yanathibitisha
k a u l i h i y o . Tu a n z e
kwa machache yaliyo
wazi. Wako wapi wana
UAMSHO hivi leo?
Chambilecho Balozi
Seif Ali Idi, wako huko
wana...! Kwanini?
Jibu liko wazi: Waliapa
kuuamsha uma na
kupigania uhuru
wa Zanzibar ndani
ya Muungano. Hilo
kweli kosa? Lakini

MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif


Ali Idi.
kwa vile wametenda Hapakuwa na haja ya
dhidi ya Dola, leo hii kumsafirisha kwenda
Uamsho yanawakuta naye Unguja bure kama
ya kuwakuta huko bara. kweli nchi hii inafuata
Hilo moja.
misingi ya utawala bora
H i v i k a r i b u n i na utawala wa sheria.
tulishuhudia vijana L a k i n i k w a k u w a
k a d h a a w a C U F waliofanyiwa ni wale
wakijeruhiwa vibaya wale watende wao
kwa mapanga na vitu alichokisema Said Ali,
vyenye ncha kali wakati kimekuwa mwao!
wakirudi mkutanoni
Nilifuatilia sana
Makunduchi.
kisa cha Said Ali na
Wa l i o f a n y a v i l e kwa hakika sijaona
yaaminika kuwa ni kama alikosea kiasi
vijana wa Janjaweed cha kusafirishwa kama
waliokuwa katika gari haini kwenda Unguja
la wazi la mmoja ya k u h u k u m i wa . K wa
Viongozi wa jimbo moja ufupi alichokisema
Unguja. Tukasema sana Said kama Mwenyekiti
juu ya tukio hili. Lakini w a J U V I C U F n i
kwa kuwa waliofanya kuwa Balozi Seif Idi
vile ni watu wao, hili asije Pemba kufanya
nalo halikuwa kosa MIKUTANO kwa kile
wala hakuna hatua anachodai kuwa Balozi
iliyochukuliwa dhidi alizuia wafuasi wa CUF
ya wahalifu wale wa kwenda mikutanoni
Janjaweed. Watende mashamba. Hilo ndilo
wao hao!
la Said kwa watawala
Kati ya Tarehe 20 na 21 wetu, CCM-DOLA.
mwezi wa tano, mwaka
Kinachoshangaza
huu, tumeshuhudia zaidi, kama unafuatilia
kiongozi wa Jumuiya hutuba za baadhi ya
ya V i j a n a ya C U F m a k a d a w a C C M
(JUVICUF), Wilaya ya mfano Borafya na Shaka
Mkoani Bwana Said Hamdu Shaka, utaona
Ali, akikamatwa na kuwa hotuba zao zote
Polisi na kusafirishwa wanamtukana Maalim
h a d i U n g u j a k w a Seif, tena matusi ya
m e l i i l i k w e n d a nguoni na baadhi ya
kujibu mashitaka ya wakati mbele ya Vigogo
kumkashifu Balozi Seif wa CCM na serikali ya
Ali Idi.
Zanzibar.
Nchi yetu inatajwa
Kama kawaida ya
kuwa imekubali na wa t e n d e wa o , k wa
kupitisha azimio la v i l e w a n a o s e m a
haki za Binadamu. Na hayo ni makada wa
moja kati ya haki hizo CCM, hili halikuwa
ni haki ya kujieleza kosa. Kosa likawa la
na kutoa maoni huru. Said tu. Kwa maana
Alichokifanya Bwana nyepesi, hapa utaona
Said Ali ni kutoa maoni kuwa; kumdhalilisha
yake na hisia zake tu Makamo wa kwanza
na sio chengine. Sasa wa Rais hadharani sio
kwa vile aliyemsema kosa, lakini kumsema
n i D o l a , n a k a m a Makamo wa Pili wa
nilivyokwishatangulia Rais ni kosa la uhaini au
kusema CCM- Dola Iko kosa la jinai. Hizi ndio
juu ya Sheria, Said Ali siasa zetu Zanzibar.
akatiwa hatiani.
Mfano mwingine,
Cha kushangaza, hivi juzi juzi tu, yaani
kosa lolote atakalokuwa wiki moja iliyopita,
nalo Said Ali, basi wananchi wa kijiji cha
naamini mahakama Kwale, Micheweni
z i p o z a k u t o s h a , Pe m b a a m b a o n i
Pemba za kumshitaki. wakereketwa halisi

wa c h a m a t a wa l a ,
walijaribu kuiteremsha
bendera ya CUF
iliyokuwa imepachikwa
pale na mwanachama
mmoja wa chama hicho.
Hoja yao kuu ya kutaka
kuishusha bendera hii
walidai kuwa hawataki
CUF katika kijiji chao.
Hivi hii ni hoja sahihi
kisheria?
Nini basi kilitokea?
Mwenye bendera ya
CUF alipoona wanakijiji
wanataka kuishusha
bendera, alitoka na
panga akawaonya kuwa
atakayesogea kuishusha
bendera hiyo, atakiona
kilichomfanya punda
asiote nundu. Kifo
si swahiba mwema.
Wa k e r e k e t wa wa l e
walipoona hali
imekuwa ngumu,
waliita Polisi. Polisi
walipofika walipiga
risasi juu na kumtishia
mwenye kupachika
bendera. Akakimbia.
H a p o k wa m s a a d a
wa Dola, bendera ya
CUF ikashushwa juu
ya mlingoti na wana
CCM-DOLA wa Kwale.
H a b a r i
h i i
ilipowasilishwa
bungeni siku iliyofuata,
wahusika wote
wa k a c h u k u l i wa n a
Polisi na kuswekwa
rumande huko
We t e . K a t i ya h a o
waliokuwamo ni
Afisa Elimu Wilaya ya
Micheweni Mbwana
Shaame Hamad, Afisa
wa Tume ya Uchaguzi
Wilaya ya Micheweni
Bwana Khamis
Massoud na Mwalim
Mkuu skuli ya Shumba
mjini Mwalim Bakari.
Kuwekwa ndani kwa
wana dola hawa ambao
wanashika nyadhifa
nyeti za Serikali,
hakukudumu masaa.
Siku ya pili tu tangu
watiwe mbaroni, kauli
ilitumwa kwamba
watolewe mara moja.
Wa t u h u m i w a h a o ,
wakaachiwa huru
huku ikisemwa kesi
yao itasikilizwa wakiwa
nje kwa dhamana.
Wananchi wenzangu,
hebu tukae chini
tutafakari: ingekuwa
waliofanya jaribio hili
ni waumini wa chama
chengine au tuseme
wapinzani, ingekuwaje?
Jawabu utakalolipata,
malizia na ujumbe
wangu:
Wa t e n d e w a o ,
wa k i t e n d a we n z a o
huwa mwao! Na kwa
hali kama hii - Je,
tutafika?

16
SAUMU kilugha ni kujizuiya
na kitu, yaani kutofanya kitu
fulani; kama ilivyo kwenye
Qurni Tukufu:
"Hakika mimi nimeweka
n a d h i r i k wa M we n ye z i
Mungu ya kufunga; kwa
hivyo leo sitasema na mtu".
(Maryam : 26).
Kisharia Saumu ni kujizuia
kula, kunywa na matamanio
ya utupu; tangu alfajiri mpaka
kutua jua pamoja na kutia nia
ya hio saumu.
Hivi kutia nia ni kwa qauli
ya Mtume wetu Mpenzi
s.a.w. kwa kukhusu kila
ibada, yaani kutimia ibada
ni kuwepo na kutimia nia:
"Hakika ya kila kitendo ni
kwa nia yake".
Hukmu Yake: Saumu ni
nguzo ya nne kati ya nguzo
tano za Uislamu. Kulazimika
saumu kumekuja kwa
Qauli ya Mwenyezi Mungu
Mtukufu, na kufasiriwa
kwa qauli ya Mtume wetu
Mpenzi s.a.w. na wanazuoni
wakawafiqiana juu ya hili.
Amesema Mwenyezi Mungu
Mtukufu:
"Enyi mlio amini!
Mmeandikiwa Saumu,
kama waliyo andikiwa walio
kuwa kabla yenu ili mpate
kuchamngu. (Al Baqara :
183).
Na Mwenyezi Mungu
Mtukufu amesema:
"Basi ataye kuwa
mjini katika mwezi huu
naafunge.......".(Al Baqara :
185).
Na Hadithi ya Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.:
"Umejengwa Uislam juu ya
(Nguzo) tano".
Katika nguzo tano hizo,
ikatajwa nguzo ya nne kuwa
ni Saumu ya mwezi wa
Ramadhani.
Mtu alimuomba Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.
amfahamishe saumu
alioifaridhisha Mwenyezi
Mungu Mtukufu juu yake.
Akasema Mtume wetu
Mpenzi s.a.w.: Saumu ya
Mwezi wa Ramadhani".
Saumu imewajibikishwa
juu ya Muislamu, baalegh,
mwenye akili kaamili,
mwenye uwezo wa kufunga.
Saumu haimuwajibikii Kafiri
wa asili, wala haisihi juu
yake Saumu, kwa vile yeye
si mwenye kuhisabika kuwa
ni katika wenye kufanya
ibada. Vilevile Saumu
haimuwajibikii mtoto
mdogo. Saumu haimlazimikii
mtoto, lakini mtoto
huzoeleshwa kufunga tangu
udogoni. Vilevile Saumu
haimuwajibikii mgonjwa wa
akili. Hivi ni kwa qauli ya
Mtume wetu mpenzi s.a.w.:
"Imeondoshwa kalamu
(kulazimika na hukmu za
Sharia) kwa watu watatu:
mwenye kulala mpaka
aamke, mtoto mdogo mpaka
a b a l e g h e , n a m g o n j wa
wa akili mpaka apowe".
(Imehadithiwa na Abu Daud).
Ama yule asieweza
kufunga, au kama
atafunga atapata madhara
ambayo hayatarajiwi, hivi

MAKALA

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Funga ya Ramadhani-Nini Saumu

ni kama vile mtu mzima


(mkubwa wa umri), au mtu
mwenye maradhi ambayo
hayatarajiwi kupona, hawa
haiwajibikii juu yao kufunga,
lakini itawalazimikia kafara.
Kafara ya katika hali hii ni
kutoa kibaba cha chakula cha
kawaida cha nchini kwa kila
siku anayoshindwa kufunga,
ikiwa ni mwenye uwezo
wa kufanya hivyo, ikiwa
hana uwezo, baadae akapata
uwezo, itamlazimu atekeleze
kafara hii ambayo ni dhima
juu yake.
Fardhi za Saumu
Saumu ina fardhi tano: Ya
Kwanza, nia; na mahala pake
ni moyoni; na ni waajib kutia
nia kila usiku wa kuamkia
(kabla ya alfajiri) siku ya
saumu. Hivi ni kwa qauli ya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
"Asietia nia (ya kufunga,
Saumu ya fardhi) tangu kabla
ya alfajiri, basi hana Saumu".
(Imehadithiwa na Ahmad na
wapokezi wa Hadithi).
Ya Pili na Tatu, kujizuia
kula na/au kunywa hata
chembe ndogo tangu kuingia
alfajiri mpaka kuingia
magharibi. Kujizuia huku
ni kwa kujizuia na kila kitu
kufika tumboni/ndani ya
mwili kwa njia ya tundu za
mwili zilizo wazi, kujizuia
huku kuwe kunakusudiwa
khaasa kwa ajili ya kutekeleza
hii ibada ya saumu.
Ya Nne, kujizuia kuingilia
utupu wowote ule na/au
kujitoa manii kwa njia yoyote
ile, ikiwa kwa mkono au kwa
kuchezeana. Haya ni kwa
Qauli ya Mwenyezi Mungu
Mtukufu:
"Basi sasa changanyikeni
nao na takeni aliyo
k u a n d i k i e n i M we n ye z i
Mungu. Na kuleni na
kunyweni mpaka ubainike
kwenu weupe wa alfajiri
katika weusi wa usiku. Kisha
timizeni Saumu mpaka
usiku.........". (Al Baqara : 187).
Ikiwa mtu atatokezea akala
au akanywa hali ya kuwa
amesahau kuwa ana saumu;
Saumu yake haitaba'tilika;

hivi ni kwa qauli ya Mtume


wetu Mpenzi s.a.w.:
"Mwenye kusahau kuwa
kafunga, akala au akanywa;
basi naatimize Saumu yake
k wa n i ye ye a m e l i s h wa
na amenywishwa na
Mwenyezi Mungu Mtukufu".
(Imehadithiwa na Jama'a
Wapokezi Hadithi)
Vilevile kwa qauli ya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
"Hakika Mwenyezi Mungu
Mtukufu amewasamehe
umati wangu kwa la
kukosea na la kusahau na la
kulazimishwa".
(Imehadithiwa na Ibnu
Maajah na Al 'Tabrany na Al
Haakim).
Ya Ta n o , k u j i z u i a n a
kujitapisha. Ikiwa atatapika
bila ya kukusudia, basi
Saumu yake haitaba'tilika,
hivi ni kwa qauli ya Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.:
"Mwenye kutapika (si
makusudi) nae amefunga,
haimlazim kuilipa Saumu
yake, na mwenye kujitapisha
(makusudi), basi naailipe
Saumu yake".
(Imehadithiwa na
Wapokezi Hadithi).
Yenye Kuba'tilisha Saumu
M a m b o
k u m i
yanaba'tilisha Saumu: La
Kwanza, kutia kitu kwa
makusudi ndani ya mwili
kwa kupitia tundu za mwili
zilizowazi, kama vile mdomo,
pua, masikio au tundu
za tupu mbili; kitu hicho
ikiwa ni chakula, kinywaji
au chenginecho, miongoni
mwa hivyo ni moshi, yaani
kuvuta sigireti na mfano wa
sigireti. Kutia kitu mwilini ni
kitu kufika tumboni, ikiwa ni
dawa au chakula au maji, au
majimaji. Hivi ni kwa Hadithi
ya Ibni 'Abbaas r.a.:
"Hakika kufungua ni kwa
kinachoingia wala si kwa
kinachotoka".
Ikiwa mtu wakati anatia
udhu akafanya mno katika
kusukutua na/au kupandisha
maji puani yakafika maji
tumboni, basi saumu yake
itaba'tilika, hivi ni kwa vile

kukatazwa kufanya mno


katika kusukutua na/au
kupandisha maji puani hali
ya kuwa umo kwenye Saumu.
Haya ni kwa qauli ya Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.:
"Fanya mno katika
kusukutua na kupandisha
maji puani, ila ikiwa
umefunga".
Lau kama kufanya
mno katika kusukutua na
kupandisha maji puani
hakufunguzi, basi Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.
asingalikataza kwa mwenye
kufunga kufanya mno katika
kusukutua na/au kupandisha
m a j i p u a n i . I k i wa h i v i
katika kutia udhu maji
yatamponyoka na yakafika
tumboni bila ya kufanya
mno katika kusukutua au
kupandisha maji puani, basi
Saumu yake haitaba'tilika;
kwani hivyo imetokea bila ya
yeye kukusudia. Ikiwa atatia
maji mdomoni au puani
bila ya haja ya kusukutua
wala kupandisha maji puani
kwa kutia udhu, maji hayo
yakamponyoka na yakafika
tumboni; basi Saumu yake
itaba'tilika, kwa sababu
amefanya hivyo bila ya haja
yenye kujuzisha kufanya
hivyo, yaani katika kutia
udhu. Ikiwa mwanamke
wakati akistanji akatia kidole
chake ndani ya utupu wake,
basi Saumu yake itaba'tilika
kutokana na Hadithi
tuliotangulia kuitaja ya Ibni
'Abbaas, na kwa vile lenye
kutakiwa ni kuondoa uchafu
ulioko nje ya utupu wala si
kwenda mno katika kustanji
kwa kilioko kwenye sehemu
iliofichika ya ndani ya utupu.
La Pili, kutia kitu
t u m b o n i ; k wa s i n d a n o
au kwa mpira (pipe) kwa
njia ya tundu ya utupu;
wa mbele au wa nyuma.
Hivi ni kwa hii Hadithi ya
Ibni 'Abbaas tuliotangulia
kuitaja, yenye kusema kuwa:
"Hakika kufungua ni kwa
kinachoingia wala si kwa
kinachotoka".
Kukhusu kuingia kitu
tumboni inasameheka kama
vile kuingia nzi, vumbi la
unga, moshi wa kufukiza,
vumbi la njiani; haya yote
hayaba'tilishi Saumu kwa
vile haikuwa kuingia kwa
kukusudia. Kukhusu kutoka
kitu mwilini/tumboni Saumu
huba'tilika kwa kutoka
damu ya hedhi, damu ya
uzazi - nifasi, kujitapisha,
kujitoa manii; haya yote
yanaba'tilisha Saumu.
Kupiga (kudunga, kuchoma)
sindano kuna rai tafauti za
wanazuoni. Wako wanazuoni
wenye kusema kuwa kupiga
sindano kunafunguza;
na wako wanaosema
hakufunguzi. Wanaosema
kupiga sindano kunafunguza
wao hoja yao ni hii hii Hadithi
ya Ibni 'Abbaas r.a. kwamba:

"Hakika kufungua ni kwa


kinachoingia wala si kwa
kinachotoka".
La Tatu, kujitapisha (si
kutapika); imeshatajwa dalili
ya hili.
La Nne, kuingilia kwenye
utupu kwa makusudi; itakuja
dalili ya hili na maelezo zaidi.
La Tano, kutokwa na manii
kwa njia iliofanywa; kama
vile kwa kujichezea kwa
mkono wake, kwa mkono
wa mkewe au kwa mkono
wa m t u m we n g i n e ; a u
kwa njia yoyote ile itakayo
sababisha kutokwa na manii.
Kuba'tilika Saumu kwa
sababu ya kutokwa na manii
kama tulivyoeleza hapa kuna
hoja zaidi ya kuba'tilisha
Saumu kwa vile kuingilia
utupu bila ya kutokwa na
manii kunaba'tilisha saumu,
basi hivi kutokwa na manii
kwa sababu ya kitendo ni hoja
zaidi ya kuba'tilika Saumu.
Ikiwa manii yatamtoka mtu
kwa sababu ya kufikiri au
kuota, katika hali hizi saumu
yake haitaba'tilika.
La Sita na Saba, kuingia
kwenye hedhi au kuingia
kwenye nifasi, hivi ni kwa
vile asli ya kusihi Saumu ni
kwa yule ambae hayumo
kwenye damu ya hedhi wala
kwenye damu ya nifasi.
Lau litamtokea lolote kati
ya mawili haya nae yumo
kwenye saumu, basi saumu
yake itaba'tilika; hivi ni kwa
qauli ya Sayyidah 'Aisha r.a.:
Tulikua tukipatwa na
hedhi nasi tuko na Mtume
wetu Mpenzi s.a.w., ikawa
tunaamrishwa kulipa Saumu,
wala hatuamrishwi kulipa
Sala.
Lau kama saumu inasihi
kwa aliomo kwenye hedhi,
basi Mtume wetu Mpenzi
s.a.w. asingali amrisha
kuilipa hio Saumu. Hivi
kutoamrishwa kulipa Sala ni
katika maumbile ya wepesi
yaliomo kwenye dini.
La Nane, kutokwa na
akili kwa njia yoyote. Hivi
ni kwa qauli ya Mtume
wetu Mpenzi s.a.w.:
"Imeondolewa kuhisabiwa
kwa watu watatu, miongoni
mwa hao watatu ni mgonjwa
wa akili (mwandaazimu).
La Tisa, kujitoa katika
Uislamu kwa njia yoyote ile,
kwa maneno au kwa vitendo
au kwa itikadi; hivi ni kwa
Qauli ya Mwenyezi Mungu
Mtukufu:
"Na yeyote katika nyinyi
akiacha Dini yake akafa nae
ni kafiri, basi hao ndio ambao
'amali zao zimeharibika
duniani na Akhera". (Al
Baqara : 217).
Vile vile amesema
Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Bila shaka ukimshirikisha
Mwenyezi Mungu 'amali
zako zitaanguka,.......".
(Azzumar : 65).
La Kumi, kuzimia; ikiwa
kutaendelea kutwa nzima
bila ya kuzindukana japo
kwa muda mchache, hivyo
saumu yake itaba'tilika,
ikiwa atazindukana japo
muda mchache Saumu
yake haitaba'tilika. Hivi ni
tafauti na kulala, akilala hata
kutwa nzima Saumu yake
haitaba'tilika.

17

MAKALA

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Salam ni nguzo miongoni mwa nguzo za swala

Na Sheikh Shmad Ragab Alsheshtawi.

SHUKURANI zote
anastahiki Mwenyezi
Mungu na rehema na
amani zimfikie Nabii
Muhammad ( S. A.W.)na
sahaba zake.
Ibada
ambazo
ametulazimisha Mola
wetu mlezi haikuwa ni
jambo lolote isipokuwa ni
mazoezi ya vitendo katika
kuendeleza kuitangaza
amani kati ya viumbe
(watu) kwa mfano Swala
tunagundua kuwa ndani
yake kuna ukumbusho wa
vyanzo wa salam (amani)
katika sehemu nyingi
kwanza pale unaposema
tashahudi (Tahiyatu) haifai
swala isipokuwa atoe
Muislamu salaam.
Ajitolee yeye mwenyewe
na awatolee waja wa
Mwenyezi Mungu walio
pembeni yake (amani
iwe juu yetu na waja wa
Mwenyezi Mungu walio
wema) na kutoka katika
nguzo hii inakuwa kwa
kutoa salam ambayo ni
moja ya nguzo za swala
basi muislamu huimaliza
swala yake kwa kusema
((amani iwe juu yenu na
rehema za Mwenyezi
Mungu na baraka zake))
kuliani kwake na kushotini
kwake.
Hata kama atakuwa
anaswali peke yake
hakuna hata mtu mmoja
pembezoni mwake hii ni
kuendeleza vyanzo vya
amani katika maisha ya
watu na baada ya hapo
atatoka katika swala na
haruhusiwi kusimama
hadi aombe dua hii:
Ewe Mwenyezi Mungu
wewe ni amani na kwako
ndiko kunakotoka
amani basi tupe uhai
wa amani umetakasika
ewe mwenye Utukufu
na Ukarimu)) haya yote
hupatikana katika swala
ama katika funga ndani
yake kuna mazoezi ya
kimatendo katika kueneza
amani (salam) imehimiza

sheria ya uislamu kwa


wale wote wanaofunga
wakati wa kufunga kwao
wazichunge ndimi zao na
wavizuie viungo vyao kwa
kila jambo litakalopelekea
kupunguza malipo ya
funga.
Amesema Mtume
[S.A.W] ((Itakapokuwa
siku ya funga ya mmoja
wenu asiongee maneno
machafu kama vile
kutongoza kukumbatiana
kubusu nk na wala
asiseme maneno ya ujinga
na wala asiseme kwa
sauti ya juu na akitokea
mtu akataka kugombana
naye au kumtukana na
aseme mimi nimefunga
mimi nimefunga)) na
wala Asilipize baya kwa
baya bali alipize baya
kwa zuri kwa ajili ya
kuendeza salam. amesema
Mwenyezi Mungu ((na

kwa kigezo cha dini wala


utaifa au rangi au lugha
na mengineyo)) haya
yalipatikana katika Hija
ya kuaga pale alipokuwa
akiwahutubia watu wote.
B) U m e h i m i z a
uislamu juu ya kuheshimu
nafsi ya binadamu na
k u i h i f a d h i k wa k e n a
umeharamisha (umezuia)
kuifanyia uadui wa aina
yoyote kama uadui wa
kuiua na aina nyingine
na ikazingatia sheria ya
uislamu kwamba uadui
wowote wa nafsi moja
basi ni sawa na kuzifanyia
n a f s i z o t e n a ye y o t e
atakeyiokoa nafsi moja
basi ni sawa na yule
aliyeokoa nafsi za watu
wote. amesema Mwenyezi
Mungu mtukufu ((kwa ajii
ya hilo tumewaandikia
ban i Israili k wamba
mwenye kuiua nafsi moja

pale wanaposema na wajinga husema


amani)) inakuja sasa nguzo ya Hija kwa
ajili ya kumpa mazoezi muislamu tena ni
mazoezi ya matendo kabla ya mazoezi ya
nadharia juu ya kusambaza amani uislamu
humkataza muislamu katika hoja juu ya
vitendo vyote vitakavyopelekea kuingilia
hata mke wa halali na ufasiki na mjadala
na kuwaudhi watu kwa maneno na vitendo
na pia kukata miti na kuua wanyama bali
wanahitajika kuhifadhi nafsi na vinginevyo
katika mambo yaliyotajwa katika vitabu vya
sunna na hadithi na fiqhi (sheria) amesema
Mwenyezi Mungu ((Imehalalishwa kwenu
kuvua baharini na chakula chake ni
starehe kwenu na ni haramu kwenu
kuwinda nchi kavu wakati miwa viwanja
vya Makka na mnaendelea na ibada na
muogopeni Mwenyezi Mungu ambaye
kwake mtakusanywa)) mtafufuliwa.
Pia kuna idadi kubwa ya misingi na
vyanzo vya amani ambavyo vimewekwa na
sheria ya kiislam kwa ajili ya kuhakikisha
vyanzo vya amani vinamea duniani kati
ya watu miongoni mwa vyanzo hivyo ni
A) usawa kati ya watu wote . hapana
tofauti kati ya tajiri na masikini na
mwenye cheo na asiye na cheo na mwenye
umaarufu na asiye na umaarufu. watu
wote ni sawa kama alivyosema Mwenyezi
Mungu mola mlezi ((Enyi watu sisi
tumekuumbeni kutokana na Mwanamume
na Mwanammke na tukakufanyeni mataifa
na makabila ili mujuane kwa hakika mbora
wenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule
anayemuogopa sana Mungu)) kwa hakika
Mwenyezi Mungu ni mjuzi na ana habari
zote)) imekuja katika hadithi toka kwa
mtume [S.A.W] (( nyote nyinyi mnatokana
na Adamu na Adamu anatoka na udongo
hivyo zindukeni mufahamu kuwa hakuna
ubora wa mwarabu kwa siye mwarabu
wala kwa mwekundu kwa mweupe. na
haya ndiyo aliyoyatangaza Mtume [S.A.W]
katika hotuba yake ya mwisho kwa wito
huu (enyi watu na wala hakusema Enyi
waislamu wale Enyi waumini na kwa
hivi ndivyo uislamu hauwabagui watu

bila ya haki au akafanya


uharibifu wowote duniani
huyo atakuwa ni sawa na
mtu aliyeua watu wote
na yeyote atakayemukoa
mtu mmoja basi ni sawa
na aliyewaokoa watu
wote)) hivyo basi haifai
kumuua mtu bila ya haki
iliyoruhusu sheria ya
kiislamu na wala haifai
kumfanyia uadui mjumbe
au balozi na wale wenye
kufikia hali ya ujirani au
kupata amani na kuishi
katika nchi yetu kama vile
watalii na watumishi wa
kiserikali za nchi nyingine
(Diplomatik) na wengineo
katika wale tunaoungana
nao kwa mahusiano na
kubadilishana manufaa
na mambo yanayo
waunganisha watu kwa
teknolojia ya kisasa.
C) Tu n a p o i t a z a m a
Surat Al-hujurat tunaikuta

sura hii ina misingi ya


vyanzo vikubwa juu ya
vyanzo ambavyo vimekuja
katika mbele ya muongozo
kwa idadi kubwa na miito
mbalimbali ambayo
ameielekeza Mola wetu
mlezi juu ya ibada ya
waumini kama vile kuwepo
k wa wa s i o wa i s l a m u
na kuwapatanisha
waliogombana na
kukataza kudharauliana
na kubezana kupeana
majina mabaya na
kuchunguzana na
kutetana (kusengenyana)
na kufanyiana umbea
(kueneza habari za uzushi
na uongo na mambo
mengineyo mengi tuu
ambayo yatapelekea
kuharibu hata kuondoa
kabisa udugu wetu wa
kibinadamu.

18

Makala

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

KUMBUKUMBU
Na Alhaj Abdallah
Tambaza
MWEZI kama huu miaka
minne iliyopita, Rais Jakaya
Kikwete ilibidi akatishe
ziara nchini Botswana na
kurudi nyumbani kuongoza
maelfu ya waombolezaji
jijini Dar es Salaam katika
mazishi ya mmoja wa watu
mashuhuri kupata kutokea
katika ukanda wa Afrika
Mashariki na Kati. Alikuwa
bingwa wa usomaji Quran;
bingwa wa unajimu; bingwa
wa tiba asilia; mtaalamu wa
nyota (horoscope) na pia
mwanasiasa nguli.
Safari ya Sheikh Yahya
kusaka elimu ilihamia
Zanzibar. Kule alikwenda
kujiunga na Zanzibar
Muslim Accademy
iliyokuwa ikiongozwa na
Mudir (principal) kutoka
chuo cha Al-azhar Sharif cha
Misri, Sheikh Mohammed
Addahani.
Yahya hakupata nafasi,
kwa sababu kwa mujibu wa
mudir wa chuo, hakufikia
vigezo vilivyohitajika
kujiunga chuoni pale.
Akisimulia kisa hicho,
Sheikh Ahmed Haidar
Mwinyimvua, Imam Mkuu
wa Masjid Mwinyikheri,
Kisutu Dar es Salaam,
aliyekuwa mwanafunzi
chuoni pale anasema:
Yahya aliondoka zake,
lakini siku chache baadaye
Mudir Addahani aliisikia
Quran Tukufu ikisomwa
katika Sauti ya Unguja na
mtu ambaye hakupatapo
kumsikia kabla; alitaka
kujua alikuwa nani yule
aliyesoma Qurani kwenye
Sauti ya Unguja.
Akajibiwa, Ah! ni
yule kijana Yahya ambaye
ulimkataa kujiunga na
Accademy yako.
Alijiuma vidole, akasema
yalikuwa ni makosa, atafutwe
haraka aje kujiunga na chuo
mara moja, anasema Sheikh
Haidar.
Pamoja na Sheikh Ahmed
Haidar, wanazuoni wengine
mashuhuri hapa nchini,
ambao alikutana nao pale
Muslim Accademy Zanzibar,
ni Sheikh Harith bin Khelef
(aliyekuja kuwa Mufti na
Kadhi Mkuu Zanzibar ),
Sheikh Mohammed Ali
Gongabure, aliyetoka
Mbwera, Kusini mwa
Tanzania na Khamis Said
Khalfan wa Madrassa ya
Mtoni jijini Dar es Salaam.
Hapa pia, mwanafunzi
Ya h y a a l i k u m b a n a n a
m s u k o s u k o m we n g i n e ;
maana alikuja kumkosoa
Mudir Addahani, kwamba
alikuwa akiwapendelea
wanafunzi fulani fulani
katika utoaji wake wa maksi.
Alifukuzwa chuo
kwa utovu wa nidhamu.
A l i o n d o k a n a k we n d a

Sheikh Yahya Hussein-2

AL-MARHUUM Sheikh Yahya Hussein (kushoto) akiwa na Rais wa Zanzibar Dkt.


Ali Mohamed Sheikh (kulia) wakati wa uhai wake.
nchi za Uarabuni alikoasisi
taasisi iliyojulikana kama
World Muslim Congress na
baadaye kuwa Katibu Mkuu
wa East African Muslim
Welfare Society (EAMWS)
Makao Makuu nchini Kenya.
Nchini Misri, pamoja na
watu wengine, alikutana na
mujawiid mwenzake Sheikh
Mahmuud Khalil Alkhusar,
aliyempeleka kwa Mufti wa
al-Azhar University, Sheikh
Mahmuud Shaltut.
Ahmed Haidar, akiwa
sasa mwanafunzi pale alAzhar anaelezea:
Iliandaliwa hafla kubwa
katika Continental Hotel
mjini Cairo, ambapo mbele
ya m a q a r i i ( wa s o m a j i )
wakubwa kama Mustapha
Ismail, Abdulbasit
Abdulsamad, Mahmud
na nduguye Mohammed
Alminshawi na Mufti wa
al-Azhar Yahya alisoma
Qurani ya hali juu (classical
and mesmerizing) iliyosikika
live redioni Misri.
Lilikuwa ni tukio la
aina yake, mimi pamoja
na Watanzania wengine
tuliokuwa wanafunzi pale
Cairo na wale wa ubalozini
tulikuwapo ukumbini
tukimsindikiza ndugu yetu,
anasimulia Sheikh Haidar.
Safari ya Sheikh Yahya
haikuishia hapo. Alitembelea
nchini Malaysia na kusoma
Qurani iliyomfanya kiongozi
wa nchi hiyo siku hizo, Tunku
Abdulrahman, amwalike
Ikulu kula naye chakula,
ambako pia alimsomea
tajwiid kwa mara nyengine.
Mjini Amman, Jordan

alikaribishwa na Mfalme
Hassan, ambaye pia
alipumbazika na sauti
nyororo yenye mvuto na
kuliwaza aliyobarikiwa nayo
hayati Sheikh Yahya.
Msomaji zingatia kwamba
halikuwa jambo rahisi kwa
mtu Mweusi wa wakati huo,
kusoma kwa kiwango cha
Sheikh Yahya, tena elimu
yote hiyo akiwa ameipata
nchini mwake.
Katika fani ya tajwiid,
S h e i k h Ya h ya a l i b o b e a
zaidi katika ihkami, njia na
mahadhi; akiwa mzuri zaidi
katika mahadhi ya bayati,
sika na razdi (usomaji wa
Qurani una namna namna,
kama vile za waimbaji
zilivyo na base, tenor, tango,
rhumba na blues).
Kuna majina mengine
alikuwa ameyabuni
mwenyewe kama vile, sika
ya B a g a m o y o a m b a y o
imethibitika kwamba
inapatikana Tanzania tu:
Ah! hiyo razdi gogo
hiyo ni bayati mama ...ehe!
ehe! hapo hebu rudia
tena hapo kidooogo!
Kila mara alisikika Sheikh
Yahya akisema wakati mtu
mwengine akisoma Qurani
na yeye ni msikilizaji.
Katika safari yake ya
Uarabuni, Sheikh Yahya
aliweza kupata fedha nyingi
sana kwa maendeleo ya
dini ya Kiislamu pamoja na
scholarships zizisokuwa na
idadi alizowapatia vijana
wengine kwenda kusoma
huko.
Ukiacha umaarufu wake
katika kusoma Qurani,

Sheikh pia katika kipindi


f u l a n i k a b l a ya U h u r u
alijishughulisha na siasa.
Babake mkuu, Sheikh
H u s s e i n J u m a a l i k u wa
kiongozi wa chama cha siasa
cha UTP (United Tanganyika
Party) na yeye Yahya aliunda
cha kwake cha AMNUT
(All Muslim National Union
of Tanganyika). Ingawa
havikuwa vikikubaliana na
Tanu katika masuala fulani,
lakini madhumuni ya vyama
hivyo yalikuwa ni yaleyale
kama ya Tanukupigania
Uhuru. Sasa sijui ni kwa nini
inasemwa uhuru uliletwa na
Tanu na Nyerere tu? Chama
cha Tanu kilishinda uchaguzi
tu kwnye ballot box 1961
na hivyo kuunda serikali;
lakini kama ni mapambano
dhidi ya mkoloni walifanya
watu wengi akiwamo Sheikh
Yahya.
Wakati mmoja, alipokuwa
jukwaani akihutubia
mkutano wa kisiasa kabla
ya uhuru, Sheikh Yahya
aliwahi kumdhihaki
( r i d i c u l e d ) N ye r e r e n a
wenzake katika TANU, kama
wapiga makelele mfano
wa wanamuziki wasiojua
walitakalo!
Mwanasiasa mwingine
machachari wakati huo
alikuwa ni Zuberi Mtemvu
wa African National
Congress (maarufu
Congress). Katika uchaguzi
kuelekea uhuru, Congress
ya Mtemvu ilikuwa ya pili
baada ya Nyerere. Mikoa
kama vile Bukoba, Tabora
Congress iliibwaga Tanu.
Yahya Hussein alikuwa

Mwafrika wa kwanza katika


nchi za Afrika Mashariki
kutoa Horoscope tafsiri ya
nyota kwenye magazeti
ya Kiingereza na Kiswahili.
Kabla ya hapo kurasa hizo
zilikuwa zikitoka kwenye
magazeti ya London.
Alikuwa mtu wa kwanza
kuwa na gari (saloon) lenye
milango sita Tanzania.
Alikuwa pia mtu wa
kwanza nchini kuwa na
Mobile Van lenye TV screen
ambalo alilitumia kwenye
maonyesho au nje ya nyumba
yake pale Mwembechai na
kuwapatia uhondo wa bure
watu hasa watoto.
Mnamo miaka ya mwanzo
ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Sheikh Yahya alitembelea
visiwani Zanzibar. Akiwa
huko alitiwa mbaroni na
serikali ya Mzee Karume
(hayati) kwa madai kwamba
alikuwa akionekana
a k i z u n g u m z a n a wa t u
wenye asili ya Kiarabu.
Akiwa gerezani kule
Zanzibar, Sheikh Yahya
a l i k u t a n a n a m f u n g wa
mwengine Mwarabu
aliyetokea nchi ya Bahrain.
Habari zinasema, ilikuwa
ni Mwarabu huyo aliyempa
elimu ya utabiri kufuatana na
mwenendo wa nyota pamoja
na uwezo wa kuzungumza
na kupata habari za majini.
Mwarabu yule alikuja
kutoweka gerezani bila
kuonekana na mtu mpaka
leo maana alijigeuza
chura kimazingaumbwe,
anasimulia Maalim Hassan
Yahya, mtoto wa hayati
S h e i k h Ya h ya k w e n y e
kipindi cha Channel Ten
on Monday kilichorushwa
hewani Mei 30, 2011 siku
chache baada ya kifo cha
Sheikh Yahya.
M wa k a 1 9 6 5 , S h e i k h
alihamishiwa Gereza la
Ukonga Dar es Salaam
alikokaa kwa muda na
baadaye aliachiwa huru na
kuja mjini kujikita katika fani
hii mpya ya unajimu.
John Bwire, Mhariri
Mwandamizi wa Magazeti
ya Raia Mwema, anasema
hakuwa akimfahamu Sheikh
Yahya kabla ya kuanza
kusoma magazeti ya Baraza
na Taifa Leo kutoka Kenya:
Nilikuwa mpenzi sana
wa gazeti la Baraza la Kenya
kwenye miaka ya 60 na
70 na humo ndio nikawa
nakutana na utabiri wa nyota
za Sheikh Yahya hakuwa
mtu wa Tanzania peke
yake yule ni hasara kwa
ukanda mzima wa Maziwa
Makuu,amesema Bwire.
Katika utabiri, alianzia
kwenye kutabiri mpira kabla
ya kutoa utabiri wa nyota
magazetini, wakati huo
ambapo hakukuwa na mtu
mwengine aliyeijua fani hiyo
hapa nchini.

Itaendelea toleo lijalo

19

AN-NUUR

Makala ya Mtangazaji

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Israeli Navy Arrests Five Fishermen, Soldiers Injure Farmer in Gaza


KHAN YOUNES,
(WAFA) The Israeli
navy on Wednesday
arrested five Palestinian
fishermen while sailing
offshore the coast of
K h a n Yo u n e s , i n
southern Gaza Strip,
according to local
sources.
WAFA correspondent
said a number of Israeli
naval boats attacked the
fishermen and arrested
them. The five fishermen
were taken to nearby
Israeli Ashdod seaport
by the navy.
Thje fishermen
were identified as
Mohammad Baker,
Haitham Baker, Hassan
Mahmoud Abu Saman,
Hassan Abder-Rahman
A b u S a m a n , a n d
Mohammad Ali Morad.
Meanwhile, a farmer
was injured by Israeli
soldiers live bullets
near the border east of
Khan Younes.
The farmer, 22-yearold Farid Najjar, was
injured with a bullet in
the abdomen, and was
transferred to hospital
for medical treatment.
His medical condition
was described as
moderate.
Israeli naval boats
routinely open fire at
Palestinian fishermen
sailing within the sixnautical-mile allowed
zone for fishing as well
as on farmlands along
the borders, flagrantly
violating the ceasefire
deal.
Israel and the
Palestinian factions
signed a ceasefire deal on
August 26, 2014 ending
the latest 2014 summer
deadly Israeli onslaught
on Gaza which claimed
the lives of over 2,200
people, overwhelmingly
civilians.
Under the ceasefire
d e a l , I s r a e l wa s t o
immediately ease the
blockade imposed on
the strip and expand
the fishing zone off
Gaza's coast, allowing
fishermen to sail as far
as six nautical miles
from shore, and would
continue to expand the
area gradually.

Israeli military court


goes back on Jarrar
release

Palestinian fishermen in the Gaza Strip. (AFP)

US Obama: Israel Continues to Lose Credibility over Peacemaking


WA S H I N G T O N ,
June 3, 2015 (WAFA)
United States President
Barack Obama Tuesday
blamed Israeli Prime
Minister Benjamin
Netanyahu's terms for
diplomacy for failing
to advance peace with
the Palestinians, saying
Israel seems to have
lost its international
credibility as a potential
peacemaker.
In an interview with
the Israeli Channel II,
Obama suggested that
continued US diplomatic
defense for Israel at the
United Nations over
the Palestinian cause
may be reviewed,
though he reaffirmed US
commitment towards
Israeli security.
He said he was
pessimistic about
decades of negotiations
on Palestinian statehood
bearing any fruit during
the 18 months he has
left in office. I don't
see the likelihood of a
framework agreement
The question is how
d o we c r e a t e s o m e
building blocks of trust
and progress.
Obama
said
Netanyahu's position

US President Barack Obama, seen on June 2, 2015.


(AFP/Saul Loeb)

has so many caveats,


so many conditions that
it is not realistic to think
that those conditions
would be met at any
time in the near future.
So the danger is that
Israel as a whole loses
credibility. Already,
the international
community does not
believe that Israel is
serious about a two-state
solution.
We l l , h e r e ' s t h e
challenge. If in fact
there is no prospect of
an actual peace process,
if nobody believes there
is a peace process, then
it becomes more difficult

to argue with those who


are concerned about
settlement construction,
those who are concerned
about the current
situation, he said.
It is more difficult for
me to say to them, 'Be
patient, wait, because
we have a process here.
Obama said that both
Israelis and Palestinians
should work with the
United States to move
off what appears right
now to be a hopeless
situation and move it
back toward a hopeful
situation.

BETHLEHEM (Ma'an) -An Israeli military judge


reversed a ruling to release
Khalida Jarrar on bail,
deeming the Palestinian
parliamentarian as a
"security risk" based on
secret evidence, prisoner
rights group Addameer told
Ma'an.
The ruling came May
28 after an appeal by the
prosecution was upheld by
the military judge, who made
the decision based on secret
evidence provided by the
prosecution.
Jarrar was initially ordered
on May 21 to be released on
bail of 20,000 shekels ($5,160)
in cash and a guarantee from
a third party for the same
amount.
The judge ruled at the
time that the prosecution
had provided insufficient
and out of date evidence that
Jarrar would be a security
risk if released, rights group
Amnesty International
reported.
The prosecution reportedly
told the judge during the May
21 hearing that they would
ensure Jarrar remain in prison
under an administrative
detention order.
As Jarrar has already been
charged, the ruling to keep
her in military custody comes
as a "clear form of arbitrary
detention," Addameer says.
Jarrar was detained on
April 2 from her home in
the Ramallah neighborhood
of al-Bireh. An Israeli army
spokeswoman told Ma'an at
the time that Jarrar had been
detained for being the leader
of a "terrorist organization,"
and had encouraged "terror
activities" in the previous
few weeks.
Official charges made
against Khalida Jarrar on
May 21 included membership
of an illegal organization,
carrying out services for
the illegal organization,
participation in protests and
incitement to violence.

Contact us: P.O Box


20307, 612 UN Road
Upanga West, Dar es
Sa la am Tel: 2152813,
2150643 Fax: 2153257
Email: pict@pal-tz.
orgWebsite: www.pal-tz.
org

AN-NUUR

20

MAKALA

20

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

AN-NUUR

SHAABAN 1436, IJUMAA JUNI 5-11, 2015

Safari ya Hijja Hijiria 1436

Tanzania Muslim Hajj Trust, uandikishaji unaendelea,


gharama za Hijja ni US Dollar 4400, tarehe za Safari ni:
11 na 13 Septemba, kurudi 7 Oktoba, 2015.
Wahi kujiandikisha sasa
Kwa mawasiliano: +255 222 182370
0754 261910; 0717 000065
+255 222181577
0784 272723
0786 383820
website-www.hajjtrust.or.tz
0713 764636

E-mail:info@hajjtrust.or.tz

Kengele ya hatari Yemen

WAKATI mashambulizi
makali yanayofanywa na
ndege za kivita za Saudi
Arabia dhidi ya Yemen
yakiwa yanaingia katika
m w e z i wa k e wa t a t u ,
maelfu ya raia wa nchi hiyo
wameendelea kuuliwa na
wengine wengi kujeruhiwa
huku miundombinu ya nchi
hiyo ikiharibiwa kabisa.
Hata hivyo pamoja na
kutokea madhara hayo
makubwa, kinachoshangaza
wengi ni kwamba bado
hakuna hatua za uhakika
za kupatikana misaada
ya dharura wala jitihada
madhubuti za kumaliza vita
hivyo zilizochukuliwa na
UN, ili kunusuru maisha ya
waathirika wa vita hivyo.
Ripoti za masharika ya
kutetea haki za binadamu
na ya utoaji misaada ya
kibinadamu zinasema kuwa
hadi sasa watu zaidi ya
4,000 wamepoteza maisha
katika mashambulio hayo
ya kinyama, 1000 kati yao
wakiwa ni wanawake na
watoto.
Wakati hali ikiwa hivyo,
zaidi ya Wayemen 7000
wamejeruhiwa katika
mashambulio hayo na
wengi wakiwa ni watoto,
wanawake na wazee.
Miundombinu na makazi
ya raia pia hayajasalimika
na mashambulio hayo ya
nchi kavu, bahari na anga,
ambapo zaidi ya nyumba
1000 zimeharibiwa. Vituo
vya afya vilivyoharibiwa
katika mashambulio hayo

RAIA wa Yemen wakiokoa wenzao waliofukiwa na vifusi na majengo kutokana na


mashambulio ya ndege za kivita za Saudi Arabia yanayoendelea nchini humo.
kuwa, mashambulizi hayo
ya kunywa.
vinafikia 1200.
ya Saudia Arabia nchini
OXFAM linasema hali
Kuhusiana na suala
Yemen yamesababisha zaidi
hiyo ni kengele ya hatari
hilo, Shirika la Kimataifa
ya watu milioni 16, yaani
inayoaashiria hatari ya
la Misaada ya Kibinadamu
thuluthi mbili ya watu wa
kuzuka janga kubwa la afya
Oxfam, limetahadharisha
nchi hiyo kukabiliwa na
nchini Yemen.
kuhusu hali hiyo ya
uhaba mkubwa wa maji safi
Shirika hilo limelaani
kusikitisha na kuongeza

vikali hatua ya Saudia ya


kuendelea kuharibu kwa
mpangilio miundombinu
ya maji nchini Yemen na
kuongeza kuwa, jambo hilo
limewalazimu Wayemen
kunywa maji yasiyo
salama kwa afya zao na
limewasababishia maradhi
mbalimbali yakiwemo ya
malaria na kipindupindu.
Kinachosikitisha ni
kwamba pamoja na
kutolewa kwa takwimu hizo
za kutisha, lakini jamii ya
kimataifa imeamua kukaa
kimya na kutochukua hatua
yoyote kwa lengo la kuzuia
umwagikaji wa damu ya
Wayemen wasio na hatia.
Hali hiyo imekuwa mbaya
zaidi kutokana na Saudi
Arabia ya kuzuia misaada
ya kibinadamu iwafikie
waathirika wa mashambulio
yake huko Yemen.
Watawala wa nchi hiyo
wamedaiwa kuwazuia hata
madaktari wasio na mipaka
kuwahudumia majeruhi
na waathirika wengine
wa mashambulizi hayo
yanayoonekana kuwa ni ya
kibabe na kichokozi nchini
humo.
Daktari Margaret Chan,
M k u r u g e n z i M k u u wa
Shrika la Afya Duniani WHO
alisema, Wayemen wapatao
8,600,000 wanahitajia
matibabu ya dharura.
Aliashiria uhaba mkubwa
wa vifaa za tiba uliopo
huko Yemen na kuongeza
kuwa, wanawake wengi
wajawazito wa nchi hiyo
hawana hata huduma za
msingi za kuwawezesha
kujifungua salama.

KATIKA hali ambayo idadi


kubwa ya waathirika wa
vita vya siku 50 vya Gaza
mwaka 2014 walikuwa ni
watoto wa Kipalestina,
dunia hivi sasa inafanya
juhudi za kuuburuza
mahakamani utawala wa
Kizayuni kutokana na jinai
zake hizo za wazi.
Bi. Leila Zerrougui,
mwakilishi wa Algeria katika
Umoja wa Mataifa na pia ni
mjumbe Maalum wa Katibu
Mkuu wa Umoja huo katika
masuala ya watoto wanaoishi
kwenye maeneo ya vita, kwa
mara ya kwanza ametaka
jina la jeshi la utawala wa
Kizayuni wa Israel liingizwe
kwenye orodha nyeusi ya
Umoja wa Mataifa.
Kila mwaka orodha hiyo
hutaja majina ya serikali
ambazo zinakiuka haki za
watoto katika mapigano ya
kutumia silaha.
Orodha nyeusi ya Umoja

wa Mataifa imepangiliwa
kwa mujibu wa sheria za
kimataifa, misingi ya haki
za binadamu na kulinda
m a t u k u f u ya k i u t u n a
kimaadili dhidi ya nchi
zinazokanyaga misingi hiyo.
Hatua ya mjumbe huyo
maalumu wa Katibu Mkuu
wa umoja wa Mataifa ya
kutaka jeshi la Israel
liingizwe kwenye orodha
hiyo nyeusi, imechukuliwa
kwa kutegemea uchunguzi
uliofanywa na umoja huo
kuhusu jinai zilizofanywa
na jeshi la Israel katika
m a s h a m b u l i z i ya k e ya
kikatili ya siku 50 huko Gaza.
Matokeo ya uchunguzi
huo yametangazwa mwezi
wa Aprili mwaka huu.
R i p o t i ya u c h u n g u z i
huo wa Umoja wa Mataifa
inaonesha kuwa, watoto 500
waliuawa huko Gaza wakati
wa mashambulizi hayo na
3,300 wengine walijeruhiwa

Ban Ki moon hajachukua


uamuzi wowote kuhusu
kuingizwa jina la serikali ya
Israel kwenye orodha hiyo.
Imeelezwa kuwa ni
jambo lisilo na shaka hata
chembe kwamba utawala
wa Kizayuni, umefanya na
unaendelea kufanya jinai
kubwa dhidi ya Wapalestina.
Katika mashambulizi ya
kikatili ya siku 50 huko Gaza,
jeshi la Israel lilitumia mpaka
silaha zilizopigwa marufuku
kuwashambulia kinyama
wakazi wa ukanda huo.
Kilichoshangaza wengi ni
kuona kukifanyika njama za
kutoliingiza jina la utawala
wa Kizayuni kwenye orodha
nyeusi ya Umoja wa Mataifa.
Viongozi wa Palestina
wamelalamikia vikali njama
hizo ambazo wanaamini
zitazidi kuuondolea heshima
Umoja wa Mataifa. (irib).

Kimya cha Umoja wa Mataifa kinatisha

Juhudi za kuliingiza jeshi la Israel orodha nyeusi UN


au kukatwa viungo vya miili
yao.
Ripoti hiyo imeongeza
kuwa, wakati wa
m a s h a m b u l i z i h a y o ya
Gaza, wanajeshi wa Israel
walishambulia shule saba za
Umoja wa Mataifa na kuua
Wapalestina 44.
K a t i k a m u s wa d a wa
orodha nyeusi ya Umoja wa
Mataifa iliyoandaliwa na
mjumbe maalumu wa Ban
Ki moon katika masuala ya
watoto wanaoishi kwenye
maeneo yenye mapigano,
kumetajwa pia jina la Jeshi
la Israel linalojulikana kwa
kifupi IDF, kutokana na jeshi
hilo kushambulia shule na
hospitali wakati wa uvamizi
wake huko Gaza.
Wakati huo huo duru za
kidiplomasia za Umoja wa
Mataifa zimesema kuwa,
Ban Ki moon, anafanya
mikakati ya kuhakikisha
jina la utawala wa Kizayuni

haliingizwi kwenye orodha


ya kila mwaka ya tawala
zilizofanya uvunjaji wa
haki za watoto licha ya nchi
wanachama wa Umoja wa
Mataifa kutaka jina hilo
liwemo.
Ijapokuwa Wizara ya
Mambo ya Nje ya utawala wa
Kizayuni imekanusha habari
za kumshikiniza Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa,
lakini duru za kidiplomasia
za umoja huo zimesisitiza
kuwa, hivi sasa Waisraeli
wanafanya mazungumzo
ya kila upande na maafisa
wa Umoja wa Mataifa ili jina
la utawala huo lisiingizwe
kwenye orodha hiyo nyeusi
ya umoja huo.
Stphane Dujarric,
Msemaji wa Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa amesema
orodha nyeusi ya Umoja huo
itatangazwa wiki chache
zijazo ambapo hadi hivi sasa,

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

También podría gustarte