Está en la página 1de 12

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

SHURA YA MAIMAM (T) Inawatangazia Waumini wote kuwa kutakuwa na Ibada ya Itkaaf. Mahali: Masjid Mtambani, Kinondoni Siku: Jumamosi, Desemba 28, 2013 Muda: Saa tatu (3:00) usiku. Baada ya Sala ya Ishaai.

Itkaaf Masjid Mtambani

Ni kweli dhulma kubwa wamefanyiwa Madinah


Ila Elimu kwanza sio kutoa vijana shule Tutaumwa mara ngapi ndio tujifunze? Uk. 6
Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA Kuu Zanzibar, imetakiwa kufuta kesi ya mauwaji ya Padiri Mushi inayomkabili Omar Musa Makame. Akitoa hoja hiyo, Wakili anayesimamia kesi hiyo, Abdalla Juma, alisema kuwa muda umeshakuwa ni mwingi na ushahidi bado haujakamilika, hivyo ni vyema kesi hiyo kufutwa. Akaongeza kusema kuwa, kama inabidi kesi kuendelea kuwepo, basi mtuhumiwa apatiwe dhamana. Kwa kuwa muda umeshakuwa mwingi na ushahidi hadi hii leo haujapatikana, basi kesi ifutwe au Mtuhumiwa apewe dhama, alisema Wakili huyo Mahakamani hapo. H a t a h i v y o , mwendesha Mashitaka wa Serikali, Issa Mgongo, alipingana na ombi hilo la kutaka kesi ifutwe na kusema ombi hilo hakubaliani nalo kama lilivyotolewa na Wakili Inaendelea Uk. 3 OMAR Musa Makame.

ISSN 0856 - 3861 Na. 1105 SAFAR 1435, IJUMAA , DESEMBA 27, , 2013 - JAN. 2, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Inshaa Allah, usikose Ibada hii adhwiim. Kny: Amir wa Shura ya Maimam.

Kesi ya mauwaji ya Padri Mushi ifutwe-Wakili Juma


Mtuhumiwa nje kwa dhamana

MOJA ya nyumba iliyoteketezwa kwa moto kijiji cha Lwange, Kilindi Tanga.

Wananchi ndio waamuzi wa mwisho Katiba mpya

Maalim Seif ataka viongozi bora CUF Uk. 3

2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri/Habari
AN-NUUR
waliovamia nyumbani kwake. Bw. Musa Masanja wa Sakasaka Wilaya ya Meatu, alidai kuporwa shilingi 300,000 pamoja na simu mbili za mkononi na askari wa Operesheni. Katika Wilaya ya Itilima,Kijiji cha Mbogo Bw. Sita Rumala alidai kupigwa na kuvunjwa mkono. Alionesha wajumbe wa Kamatu mkono uliokuwa umefungwa bandeji ngumu (P.O.P). Bw. Munanka Machumbe (24) ambaye ni bubu alipigwa risasi tatu zilizomjeruhi mapajani na kuharibu sehemu za siri wakati akijaribu kuwahoji Askari wa Operesheni kwa ishara sababu za kumtesa baba yake. Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Ali Mohamed (70) wa kijiji cha Iputi, alidai kurushwa kichura na kutandikwa bakora na Askari wa Operesheni Tokomeza. Hayo ni baadhi tu ya matendo maovu yaliyobainishwa na Kamati ya Bunge, yaliyofanywa na wale waliopewa dhamana ya kutekeleza operesheni hiyo. Bila shaka matendo mengi machafu ya namna hii yamefanywa katika maeneo mengine ya nchi, ambako Kamati ya Bunge haikuweza kufika na

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014


kuyabaini. Tuseme tu kwamba vitendo vya namna hii si vigeni kwa vyombo vyetu vya dola. Huu umekuwa ndio utaratibu wa vyombo hivi tangu zamani na yamekuwa ni mazoea. Tumeshuhudia mara nyingi tu, maafisa wa vyombo hivi wakipongezwa, wakipewa zawadi na hata kupandishwa vyeo kilawanapofanya ukatili dhidi ya raia wema. Tumezopa kuona hata katika maandamano tu ya kisiasa au ya kidini, askari wa kutuliza ghasia (FFU) hutumia fursa hiyo kupekua mifuko ya watu wanaowakamata na kuwachukulia kila walichokikuta. Hili La Operesheni T o k o m e z a p i a linatukumbusha yale ya Mtwara katika sakata la gesi. Huko yapo madai ya kuvunjwa haki za binadamu kupitia vitendo vya ukamataji na utesaji dhidi ya raia. Pamoja na kuelezwa mateso yaliyopata raia, hakuna aliyechunguzwa wala kuchukuliwa hatua, zaidi ya wenye mamlaka kuwatetea watesaji. Hata hivyo, tunaunga mkono mapendekezo ya Kamati ya Bunge kwa Serikali, kwamba iunde chombo ambacho kitakuwa na jukumu la kusimamia na kutathmini utendaji kazi wa vyombo vyake vya dola, hasa katika shughuli za operesheni, sisi tunasema hata katika maandamano. Iwapo utaratibu huo utakuwepo, ni wazi kwamba vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa opereshini za vyombo vya dola vitadhibitiwa. Ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wa operesheni hizi za kijeshi utasaidia kupunguza uzembe na kuondoa mazoea ya baadhi ya maafisa wa vyombo hivi vya dola kujichukulia sherria mkononi na kukiuka haki za watu kutesa wananchi. Tukumbushe tu kwamba tumeshawahi kusema siku za nyuma kwamba, kuna haja ya serikali kuwa na FBI yao, ili kuwa na chombo huru kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuchunguza vyombo vingine vya dola ili vinapofanya jinai, kiwepo chombo huru cha kufuatilia na kushughulikia jinai hizo. Hata hivyo tunaishauri Serikali kuwabana wote waliohusika na vitendo vya kinyama, mateso na udhalilishaji dhidi ya watuhumiwa, iwachukulie hatua stahiki.

AN-NUUR

Tukiwa na 'FBI' yetu uovu huu utakoma


UKATILI uliotokea katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza, ni matokeo ya kulea mazoea ya baadhi ya maofisa wa ya vyombo vya dola, kutumia nafasi za kufanya ukatili bila kuchukuliwa hatua. Ripoti iliyotolewa Bungeni hivi karibuni na Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Daud Lembeli, kuhusu utekelezwaji wa operesheni Tokomeza Ujangili, imebaionisha wananchi kupa madhara makubwa, huku kukiwa hakuna taarifa za kukamatwa majangili ambao ndio waliokusudiwa katika operesheni hiyo. Watu wasio na hatia wamepata ulemavu wa kudumu, wengine kupoteza maisha kwa mfano, marehemu Emiliana Gasper Maro wa Gallapo Babati. Watuhumiwa wengine waliodaiwa kupoteza maisha wakati wa Operesheni Tokomeza ni Bw. Wegesa Kirigiti wa Kijiji cha Remagwe, Bw. Peter Masea wa Kijiji cha Mrito (Tarime), Bw. Mohamed Buto (Masasi) na Gervas Nzoya (Kasulu). Nyumba za wananchi zimechomwa moto, kwa mfano katika Kijiji cha Kabage Wilaya ya Mpanda Katavi. Mifugo imeuliwa kikatili kwa kuchomwa moto na kupigwa risasi, ngombe 60 wameuliwa kwa kupigwa risasi. Katika ripoti hiyo imeelezwa kuwa mali za raia zilipotea au kuporwa, wananchi walifanyiwa vitendo vya kikatili ambavyo vilikiuka haki za kibinadamu kama kubakwa, kucharazwa bakora, kupewa adhabu za kijeshi nk. Kwa ujumla tunaweza tusema kuwa Operesheni Tokomeza Majangili, iligeuka kuwa Operesheni Tesa Wananchi, hasa wafugaji. Kutokana na matokeo ya uchunguzi wa kamati hiyo, inavyoonekana Operesheni Tokomeza, kabla ya kusitishwa kupitia tamko la Serikali lililotolewa Bungeni Novemba 1, 2013, ni kama iliwalenga wananchi wasio na hatia na walipewa dhamana kujipatia mali kwa njia haramu, huku ikiwaacha wahusika halisi wa ujangili. Ukiacha jeshi la Wananchi, vikosi vingine vilivyoshiriki katika operesheni hiyo ni Polisi, askari wa TANAPA, TSF na NCAA. Hawa ndio wahusika wakuu wa unyama uliobainika dhidi ya wananchi. Tumebainishwa wazi kwamba baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa katika operesheni hiyo, walidai kudhalilishwa sana. Baadhi ya akina mama walidai kubakwa na kulawitiwa. Kwa mfano; katika Kata ya Iputi, Wilaya ya Ulanga, mwanamke mmoja alidai kubakwa na askari wawili wa Operesheni Tokomeza Ujangili majira ya usiku. Mama mmoja mkazi wa Kata ya Matongo Wilayani Bariadi, alibakwa na askari watatu wa Operesheni Tokomeza Ujangili huku akiwa ameshikiwa mtutu wa bunduki. Bi. Neema Moses wa Babati alidai kuvuliwa nguo na kulazimishwa afanye mapenzi na wakwe zake na pia kuingizwa chupa sehemu zake za siri. Bw. Ali Nyenge wa Kata ya Iputi, Wilaya ya Ulanga alidai kuvuliwa nguo, kumwagiwa maji yaliyochanganywa na chumvi na kuchapwa viboko huku mwanae wa kiume wa miaka 11 akishuhudia. Aidha alilazimishwa kuchora picha ya chatu kwa kutumia wembe kwenye paja lake. W a t u h u m i w a waliokamatwa walifanyiwa upekuzi bila kuhusisha viongozi wa Serikali za maeneo husika na kutokuwepo kwa mashahidi na hati za upekuzi. Kwa mfano Bw. Abdallah Pata na Bi. Flora Mwarabu wa Kata ya Iputi Wilayani Ulanga na Bw. Elias Cosmas Kibuga wa Gallapo Babati, walipekuliwa bila kufuata utaratibu. Baadhi ya watuhumiwa waliopelekwa katika kambi za mahojiano, walidai kupewa adhabu zinazokiuka haki za binadamu. Kwa mfano, Diwani wa Kata ya Sakasaka wilaya ya Meatu Bw. Peter Samwel, alidai kuadhibiwa akiwa mtupu kwa kupewa adhabu za kijeshi kama kuninginizwa kichwa chini miguu juu, kupigwa kwa vyuma na kulazimishwa kufanya mapenzi na mti. Fedha ziliporwa. Kwa mfano, katika Wilaya ya Ulanga Kata ya Iputi, mwananchi alidai kuporwa sanduku la VICOBA lenye shilingi 750,000 pamoja na simu ya mkononi na askari wa Operesheni Tokomeza

Wasomi watakiwa kujiunga kwa wingi TAMPRO


Na Mwandishi wetu ya Kusimamisha Dini ya Allah na ni Ibada. Naye Amiri wa Jumuia hiyo Bw. Musa Mziya, katika ripoti yake ya mwaka kwa mgeni rasmi, alisema Jumuia hiyo ilianzishwa mwaka 1997 kwa madhumuni ya kuwaunganisha wataalamu Waislamu popote walipo Tanzania, ili kuweza kuitumikia dini yao kuwa kutumia taaluma zao mbalimbali walizojaaliwa na Mwenyezi Mungu, kuusaidia umma kujiletea maendeleo. Alisema Jumuiya hiyo kwa sasa ina matawi 17 na wanachama 900 nchi nzima. Alisema licha ya kuongeza wanachama, pia matawi mengi ya TAMPRO yameimarishwa na kufanya idadi ya matawi yote kufikia 17. Aliyataja matawi hayo kuwa ni Mwanza, Dodoma, Arusha, Tanga, Morogoro, Iringa, Tabora, Kagera, Shinyanga, Kigoma, Manyara, Lindi, Ruvuma, Mara, Singida, Mkuranga na Kilosa. Ilielezwa kuwa juhudi zinafanyika kufungua matawi katika mikoa iliyosalia. Katika taarifa yake kwa mgeni rasmi na wanachama, Bw. Mziya alisema Jumuia iliendelea na mradi wa ujenzi wa majengo shule ya Sotele iliyopo Mkuranga mkoani pwani, mradi ambao unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Kiislamu (IDB) kwa kiasi cha dola 289,000 na kumalizika mwaka 2012. Akitoa mwelekeo wa TAMPRO 2013-2014, Amir Mussa Kundecha, amesema kuwa mwaka ujao Jumuia itaendelea kujikita zaidi katika kubuni mikakati mbalimbali ya kuharakisha maendeleo ya jamii, ili kupata matokeo ya kuridhisha. Amesema Jumuia hiyo itaen delea kusimamia malengo yake kama yalivyoainishwa kwenye katiba, ili kujiimarisha kiuchumi. Tutaendelea na ukusanyaji wa ada za wanachama na hapa nitoe wito kwa wanachama wote wa TAMPRO kuhakikisha wanalipa michango yao kwa moyo moja, ili jumuia iweze kutekeleza mipango yake iliyojiwekea. Alisema kuwa TAMPRO inatarajia kuzindua rasmi mradi wake wa jengo (TAMPRO House) kwa kuwakaribisha wadau mbalimbali kuwekeza katika mradi huo. Aliongeza kuwa mwaka ujao, TAMPRO itaimarisha zaidi miradi iliyopo ya Baiytulmaal, gazeti la Nasaha, TAMPRO SACCOS na mradi wa ufugaji wa ngombe uliopo wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani. Alisema TAMPRO inatarajia kuunda tawi jingine la mkoa wa Dar es salaam mapema mwaka ujao ili kuyafanya makao makuu ya Jumuia hiyo kushughulika na mambo muhimu ya kitaifa.

JUMUIA ya Wanataaluma wa Kiislamu (TAMPRO) wametakiwa kujivunia Uislamu wao na kufanya kazi kwa bidii. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natti, katika mkutano wa mwaka wa jumuia hiyo uliofanyika juzi katika hoteli ya Lamada, Ilala Jijini Dar es Salaam. Mkurugunzi huyo amewataka Viongozi wa Jumuia kuwahamasisha zaidi Waislamu kujiunga kwa wingi na jumuiya hiyo, ili kujenga mshikamano na umoja wa wataalamu hao. Aidha Mkurugenzi huyo amewataka Waislamu kuacha kulalamika na kuwataka kuwa watendaji zaidi, ili kuweza kufikia malengo yao na kuikoa jamii na wimbi kubwa la umasikini. Aidha alisema kuwa matajiri wengi nchini ni Waislamu na iwapo wakitumia utajiri wao katika kuusaidia Uislamu, uislamu na jamii nzima kwa ujumla itafika mbali. Amewataka wasomi wa Kiislamu kujitambua na kujivunia kuwa Waislamu mahapa popote watakapokuwa na waitumie bahati hiyo kutenda yalio mema na kufuata maelekezo ya muumba wao. Aliwakumbusha wasomo hao kufanya kazi kwa bidii popote watakapokuwa kwani wapo kwenye Jihadi

Habari/Tangazo

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

Na Bakari Mwakangwale

Wananchi ndio waamuzi wa mwisho Katiba mpya


itapigiwa kura ya maoni na Watanzania wote. Pamoja na mchakato huo kupitia hatua zote hizo, lakini mwamuzi wa mwisho katika hili ni nyinyi wananchi, kwa kuwa hatua ya mwisho itarudi kwenu na mtapiga kura ya maoni kusema ndiyo au hapana, lakini ili upige kura ni lazima utimize sifa. Alisema Maalim Seif. Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, alisema hivi sasa kuna Watanzania wengi hawana vitambulisho vya kupiga kura na kwamba tangu daftari la kupigia kura liboreshwe, kuna vijana wengi ambao wamefikia umri wa miaka 18 na kuendelea, ambao wana sifa ya kupiga kura lakini hawana vitambulisho. Maalim Seif, alisema Chama Cha Wananchi CUF kinaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhakikisha Watanzania wote wenye sifa ya kupiga kura, wanatumia haki yao ya kuweza kupiga kura kwa Bara na Visiwani. Vijana ndio matarajio ya Taifa, kwa hiyo ukiwanyima nafasi maana yake hukuwapa fursa ya kuamua kama Katiba hii inawaridhisha ama haiwarizishi, sasa serikali itafanyaje katika hili itajua yenyewe. Alisema Maalim Seif. Maalim Seif alisema katika kuliendea suala hili kumekuwa na mkanganyiko, alidai awali serikali ilitangaza kuwa hakutakuwa na sababu za kuwepo kwa Daftari la Kudumu la Wapiga kura kwa upande wa Tanzania Bara, badala yake kitakachotumika katika kupiga kura ni kitambulisho cha Uraia ambacho kinatolewa na NIDA. Serikali imetangaza kupitia Bunge kwamba Daftari la kudumu litakuwepo na litaboreshwa, Tume ya Uchaguzi ya Tanzania Bara (NEC) wamesema hawana uwezo wa kuboresha Daftari hilo. Sasa Serikali ituambie lipi ni lipi. Lakini kwa vyovyote itakavyokuwa, tunaitaka Serikali ihakikishe hakuna Mtanzania atakayenyimwa haki yake ya kuamua hatma ya Katiba Mpya, wote lazima wapige kura. Alisema Maalim Seif. Alisema endapo Wananchi wakipitisha kwa asilimia sabini, au zaidi ya theluthi mbili hiyo itatoa heshima kwa Tanzania. Lakini endapo Katiba ikipitishwa kwa asilimi 50.1, maana yake ni kwamba nusu wameikubali na nusu wameikataa na kwamba, ikiwa hivyo kutakuwa hakuna katiba hapo. Katika hatua nyingine, Maalim Seif anaunga mkono wito wa Rais Jakaya Kikwete wa kuwakutanisha wadau mbalimbali kabla ya Bunge la Katiba, kwa lengo la kuipitia Rasimu hiyo ili kuondoa tofauti miongoni mwa makundi. Alisema kikao hicho kitaangalia mambo makubwa ambayo yana maslahi na Tanzania na kutolea mfano kuwapo wananchi wanaotaka kuendelea mfumo uliopo wa Serikali mbili na wale wanaotaka kuingia katika mfumo wa Shirikisho wa Serikali tatu. Katiba tunayo itaka si katiba ya Chama chochote bali ni Katiba ya Watanzania wote, tunataka Katiba ambayo Mtanganyika aridhike nayo na katiba ambayo Mzanzibar ataridhika nayo. Kama tutakwenda katika Bunge la Katiba na kila chama na msimamo wake, waliowengi watashinda na wakishinda Katiba itapatikana, lakini haitokuwa Katiba ya Tanzania bali itakuwa katiba yao peke yao. Alitahadharisha Maalim Seif. Akizungumzia kuhusu uchaguzi ndani katika Chama chake unaoendelea hivi sasa, aliwataka wanachama kushiriki katika chaguzi hizo na kuchagua viongozi safi. Alisema umakini unatakiwa katika zoezi hilo kwani viongozi watakaoingia katika Chama, ndio wanatarajiwa kuwa majemadali katika uchaguzi wa Serikali za Vijiji, vitongoji na mitaa hapo mwakani sambamba na uchaguzi Mkuu 2015. A k a w a t a k a wanachama kuacha makundi miongoni mwao kwa kuwa hayajengi zaidi ya kubomoa. Alisema mgombea mzuri ni yule anayejinadi kwa kueleza amekifanyia nini Chama na si kumpaka matope mgombea mwenzake. M a a l i m S e i f aliiongozana na viongozi mbalimbali wa Chama hicho kufungua Ofisi za Serikali za Mtaa wa Ununio Kata ya Kunduchi, pamoja na ile ya Mtaa wa Basihaya, Kata ya Bunju.

CHAMA Cha Wananchi CUF, kimesema wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio watakaokuwa waamuzi wa mwisho katika kuipitisha au kuikataa Katiba mpya. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Msonge, Jimbo la Kawe, Jijini Dar es Salaam Ijumaa ya wiki iliyopita. Maalim Seif alisema hivi sasa mchakato wa Tanzania kupata Katiba mpya unaendelea na kwamba, kuna matumaini mwishoni mwa mwezi huu Tume ya Jaji Joseph Warioba, itatoa rasimu ya mwisho na kuikabidhi kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar Dk. Mohammed Shein. Alisema viongozi hao wakishapokea rasimu hiyo, watashauriana ili waitishe Bunge la Katiba ambalo kazi yake kubwa itakuwa ni kuijadili rasimu hiyo, kisha kutoka na rasimu ya mwisho ambayo

Inawatangazia Waislamu wote kuwa kuimeandaa safari ya Hijja mwaka 2014 sawa na mwaka 1435 Hijria kwa USD 3,600. Kutakuwa na punguzo la asilimia 18 kuanzia muda huu mpaka Machi 22, 2014 Itakuwa dola 952 tu. Kuanzia 23 Machi 2014 kuna punguzo la asilimia 8 mpaka Juni 2014 itakuwa dola 3,312 tu. Mambo yatakayogharamiwa ni semina za Hijja, huduma za afya na kuchanja, airport charge na tiketi za ndege, nyumba Makka na Madina, Ihram na kuchinja kwa ajili ya Tama-Tuu, chakula wakati wote, usafiri na ziara Makka na Madina, Mahema Mina na Arafa. Umra mwezi wa Ramadhani itakuwa ni dola US 1975. Fomu zinapatikana Ofisi ya AHLUL DAAWA Dar es Salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini- nyumba namba 26 mkabala na Showroom ya magari Tel: 0713 730444 au 0773 804101 au 0785 930444 au 0773 930444. Ofisi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484 982 au 0777 413 987. Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es Salaam Tel: 0784453838. Abdalla Saleh Mazrui (Hoko) Dar es Salaam Tel: 0715 724 444. Dukani kwa Abdalla Hafidh Mazrui Wete Pemba Tel: 0777 482 665. Dukani kwa Mohammed Hafidh Mazrui Mkoani Pemba Tel: 0777 456 911, Sheikh Daud Khamis Sheha Tel: 0777 679 692, Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar Tel: 0777 417 736. Wahi kulipa ofisi ya Ahlul Daawa Dar es Salaam Tel: 0713 730 444 au 0773 804 101 au 0785 930 444. Ofisi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484 982 au 0777 413 987. Maalim Seif Humoud Salim Tel: 0777 417 736. Sheikh Salim Mohamed Salim Tel: 0774 412 974 au Account No 048101000030 NBC Kariakoo. Atakayemaliza taratibu zote mwanzo ndiye atakayeshughulikiwa mwanzo. Ukilipa kwa njia ya Account kwanza piga simu 0774 412 975. Kumbuka kikundi cha AhlulDaawa kwa bei nafuu kuliko wote na huduma bora kuliko wengi Wabillah Tawfiq

AHLUL DAAWA HAJJ AND TRAVEL AGENCY

Inatoka Uk. 1 wa Mtuhumiwa. Alisema, ombi la pili la dhamana lifanyiwe kazi likizingatia mashariti yatakayowekwa na mahakama. Kufuatia hoja hizo za pande mbili za kesi, Mahakama Kuu ilitoa dhamana kwa mtuhumiwa wa Mauwaji ya Padri Evaristus Mushi wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Omar Musa Makame. Akitoa dhamana hiyo, Jaji Mkuu Omar Othman Makungu, amesema mtuhumiwa huyo amepewa mashariti mawili: Moja kuwa atalazimka kupata wadhamini wawili watakoweka dhamana ya laki tano kila mmoja wakiwa na vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi (ZAN ID).

Kesi ya mauwaji ya Padri

Sharti la pili ni kuwa na barua ya sheha na kuripoti katika Mahakama mbele ya Mrajis Mkuu kila siku ya Jumatatu. Mapema mwendesha mashitaka wa serikali, Abdalla Issa Mgongo, alidai mahkamani hapo kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo kesi hiyo ipangiwe siku nyengine kwa kutajwa. Mtuhumiwa Omar Musa Makame anadaiwa kumpiga risasi na kumuua Padre Mushi Februari 17 mwaka huu wakati akienda kuongoza Ibada ya Jumapili asubuhi katika kanisa la Mtakatifu Teresia liliopo Beit el Raas nje kidogo ya Mji wa Zanzibar . Alitiwa mbaroni Machi 17, mwezi mzima baada ya tukio.

4
Na Omar Msangi Assalaam alaykum wtw. Kaka Msangi makala yako ya leo (Ijumaa iliyopita) ya: Waislamu TZ hatujachelewa Jihad imenichanganya. Ni vipi Waislamu wanaweza kupambana na serikali inayowapendelea Wakristo halafu Wakristo wasichukizwe?...Kaka Msangi, hii U-turn katika reporting kipindi hiki vipi? Huo ni ujumbe wa maneno ambao niliupokea kutoka mmoja wa wasomaji Ijumaa iliyopita mchana. Msomaji mwingine naye alikuwa na haya ya kuniambia, alisema: Muambieni Muhariri wenu Bwana Omar Msangi majibu aliyopewa ukurasa wa 8 An nuur ya jana anatakiwa abadilike na atafute habari katika vyombo vya habari kama Somalimemo.net Swahili. com atapata habari za Waislamu duniani sio kutoa habari katika vyanzo vya makafiri na akiendelea na kudhoofisha jihad, Allah atamuangamiza yeye. Kwa sasa hatujamtoa katika dini ila akiendelea tutamkufurisha na kumuona ni munafiki na kama anaogopa kuandika habari za jihad aache sio kurudisha nyuma Mujahidina. Bado kuna ujumbe mwingine ambao nao ningependa kuunukuu: AA ndugu Mhariri mfahamishe Omar Msangi kuwa Uislamu unatenguka kama udhu, yeye anaipinga Jihad kwa kuhofia kuviacha vitu vyake vizuri kama mke, watoto, nyumba, gari n.k akumbuke kuwa vyote hivyo ataviacha kwa lazima na akumbuke Qaarun katika suratu Qaswaswi aya ya 76, je, alienda na mali zake kaburini? Aache unafiki. Yupo wapi Rais wa wanafiki duniani Abdallah ibnu Ubaay ibnu Suluul? Hao wanaomtumia hawatomsaidia kitu siku ya kisimamo. Aaangalie suratu Abasa aya 34-37 Zimetajwa aya hapa labda na zenyewe niziweke ili ionekane maana mtuma ujumbe aliyoikusudia. Hakika Karuni alikuwa katika watu wa Musa, lakini aliwafanyia dhulma. Na tulimpa hazina ambazo funguo zake zinawatopeza watu wenye nguvu (kuzichukua). Walimwambia watu wake: Usijione (usijigambe) hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanaojiona. (28:76) Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye. Na mamaye na babaye. Na mkewe na wanawe. Kila mtu miongoni mwao siku

Maoni yangu

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014


kukaa jirani na Msikiti. Kuwamaliza kabisa Waislamu, akafanya juhudi kusoma na kujua Quran, lugha ya Kirabu, Kituruki pamoja na Kifursi. Na hivyo ndivyo walivyofanya makachero wengi waliotumwa kupitia Wizara maalum iliyoitwa Ministry of the Commonwealth ndani ya serikali ya Uingereza. Walisoma Kiarabu na Kituruki na wajifinya watu waliosilimu waliohama kutafuta mahali pa kusoma Quran. Muingereza huyu anasema alijifanya ni yatima aliyekuja kutafuta maisha Uturuki na kuusoma Uislamu. Sheikh Ahmed Efendi, aliyempokea akamtendea wema kama Uislamu unavyoagiza kuwafanyia wageni na waliosilimu. Hapana shaka wakati ule mtu angesimama na kuhoji, mnamuamini vipi huyu Mzungu mpaka mnamkaribisha hadi chumbani, angesomewa Aya na Hadithi za fadhila za kuwakirimu wageni na kuwahudumia watu waliosilimu! Hoja hapa ni tahadhari. Kuchukua tahadhari! Sio kupinga takrima kwa wageni na waliosilimu! Na kule Syria hoja sio kupinga Jihad, lakini je, kinachofanyika ni Jihad kweli au ndio yale yale ya kumtoa Gadhafi na kuwafungulia milango mabeberu waporaji na maadui wa Uislamu? Kachero Hempher anasema anawaonea huruma Waislamu, watu wenye dini bora kabisa, lakini wamekuwa hamnazo. Hawajui kinachotokea duniani kwa hiyo inakuwa wepesi kwao kughilibiwa na kutumiwa kujidhuru wao wenyewe. What surprised me was the fact that Islam, such a noble religion as it was, was being degenerated in the hands of these conceited people who were quite unaware of what was going on in life. Haya ndiyo anayosema Hempher, kwamba Uislamu dini nzuri kabisa, lakini imekuwa mikononi mwa watu wajivuni ambao, labda kwa kutokujua thamani ya kitu walicho nacho, au kutokujua siasa chafu zinazoendelea duniani, wamekuwa hamnazo, hawana umakini wowote wala tahadhari kiasi kwamba dini hiyo inaangamizwa mikononi mwao wakitizama. Na hapa ndipo ilipo nukta ya muhimu katika makala zangu zote. Ukiwa mwanaharakati, adui wa Uislamu atakujia na mbinu za kiharakati, lakini za kukupotosha. Inaendelea Uk. 10

AN-NUUR

Tuna safari ndefu


Suala ni kujua, tusifanye kwa ujinga Yako wapi matawi Kossovo, Taliban Ya Sensa vipi, tumeyatafakari vizuri?
kura Tumbatu, Bububu, Nungwi, Mji Mkongwe, Raha Leo n.k. Rudi katika yale maandamano ya Januari 2001 ambapo baadhi ya watu walitoka kwa kujitoa kabisa mithili ya kupigania Dini, lakini mgombea Urais mwenyewe ambaye watu walikuwa wakimpigania kuwa kaporwa Urais wake, wakati huo yeye yupo Ulaya wakati watu wakipigwa risasi na virungu. Amerudi baadae kuja kutoa ubani Pemba akiandamana na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru! Ukiyajumlisha yote haya, leo matawi ya CUF ya Taliban, Gaza, Kossovo, Kandahar, Lebanon, Chechnya, imebaki ni historia. Nguvu, muda na mali imepotea bure. Namkumbuka Sheikh wangu mmoja (marehemu sasa Mungu amrehemu) alibubujikwa machozi aliposikia mgombea Urais, Zanzibar, kupitia CUF kashindwa! Kuyasema haya na kufanya tathmini hii, haina maana kupinga au kuwakatisha tamaa Waislamu wasiingie na kushiriki siasa za vyama. Hoja hapa ni kuwa waingie huku wakijua na kanuni zake na michezo yake michafu inayofanyikia ili wajiandae kupambana nayo. Katika sensa ya idadi ya watu iliyopita, Waislamu walitaka kipengele cha dini kiingizwe katika sensa. Swali ni hili: Kama katika uchaguzi mkuu, ambapo kura zinahesabiwa kituoni, kuna mawakala na matokeo hutolewa hapo hapo, lakini kura zinaibiwa. Unapiga kura yako, na huioni. Je, katika sensa ambapo wahesabuji zaidi ya asilimia 80 labda si Waislamu, lakini pia hakuna mawakala na hao nao wakishahesabu, huwapa kamati maalum na kukaa na makaratasi hayo kwa miezi kadhaa kabla ya kutoa matokeo, na hao wengi pia sio Waislamu; tulikuwa na uhakika gani kwamba idadi itakayotolewa ingekuwa sahihi? Kuhoji hivyo, haina maana kupinga msimamo wa Waislamu kutaka kipengele cha dini kuwekwa katika sensa, wala sio kudunisha umuhimu wa kujulikana kwa uhakika, hiyo atakuwa na lake la kumtosha. (80:34-37) Aliwahi kulalamika Augustino Lyatonga Mrema kuwa wakati wa uchaguzi mkuu, hata zile kura za watu wake alioamini kuwa walimpigia kura, hazikuonekana. Ziliibiwa. Hivi sasa matawi ya CUF kama Chechnya, Kandahar, Gaza, Taliban, Bosnia, Kossovo, imekuwa ni historia. Hizo zilikuwa zile zama ambapo vijana kwa wazee na akina mama wa Kiislamu, walijitosa katika chama cha CUF kwa sera zake za Haki Sawa kwa Wote wakiamini kuwa haki za Waislamu zitapatikana kupitia siasa za vyama vingi. Kinyume na wana-CCM ambao inadaiwa kuwa kwenda katika mikutano walikuwa wakikodishiwa magari na kupewa posho, hawa walikuwa wakitoa pesa zao kukodi mafuso na mabasi, ikawa ni msururu wa magari, kwenda katika mikutano. Lakini baada ya kuona kuwa hata kura zao walizopiga, pamoja na kuwa na mawakala, bado ziliibiwa kiasi cha kukosa Diwani/Mbunge hata katika yale maeneo ambayo waliamini kuwa wao ni wengi na wakiwa na uhakika wa kushinda, vijana wakaanza kurudi nyuma. Iliwachukua muda mrefu kujua kuwa siasa ni mchezo mchafu na ukiingia nawe ujue namna ya kucheza huo mchezo mchafu! Wao walidhani, suala ni kujiandikisha na kupiga kura tu. Kura yako inahesabiwa, umeshinda au umeshindwa. Wakashangaa kuona hata kura zao walizopiga, kwa maana kuwa kama walikuwa 100 katika eneo na wote walipiga kura, lakini baada ya kuhesabiwa, mgombea wao, hana hata kura moja au ana 5 tu, 95 ambazo wenyewe walipiga hazionekani! Hivi majuzi katika mkutano wa CUF uliofanyika Donge, walisimama makada wa CCM waliohama chama hicho, wakitoa ushuhuda jinsi walivyokuwa wakipiga kura zaidi ya 10. Mtu anakaa Donge, anapewa kadi ya kupigia idadi ya Waislamu na Wakristo. Lakini swali ni je, Waislamu walijiandaa vipi kukabiliana na michezo michafu kama ile inayofanyika katika uchaguzi mkuu? Katika vita ya Iran na Iraq, Saddam Hussein alikuwa akisaidiwa na Marekani. Akipewa mpaka silaha za sumu. Ambacho alikuwa hafahamu Saddam ni kuwa Marekani haikuwa inamsaidia ili ashinde vita, bali ilitumia vita ile ili kuzidhoofisha nchi zote mbili ili hatimaye ibakie Super Power moja tu Mashariki ya Kati; Israel. La kusikitisha ni kuwa mpaka sasa zipo nchi za Kiarabu wala somo hili halijaeleweka. Wanaungana na nchi za Ulaya kuchagiza Iran iadhibiwe na izuiwe kuwa na silaha za nyukilia. Lakini hazifunui mdomo kuhoji silaha za Israel! Ndio hizo hizo zinazofadhili makundi yanayojiita ya Jihad yanayopigana Syria. Wenyewe hawana utawala bora wala kutawala kwa Kitabu na Sunnah, lakini wanafadhili makundi yanayodai kupigania Shariah isimame Syria! Ilikuwepo Khilafah ambayo iliporomoka wakati makao makuu yake yakiwa Istanbul, Uturuki. Kipo kitabu kimechapishwa mwaka 2001 na kupewa jina: CONFESSIONS of A British Spy and British Enmity Against Islam. Ndani ya kitabu hicho kachero aliyetajwa kwa jina moja la Hempher, anaeleza jinsi ilivyokuwa kazi nyepesi kuiangusha Khilafah hiyo kwa kuwatumia Waislamu wenyewe. Anasema, yeye alijifanya ni mtoto yatima asiye na ndugu na aliyesilimu na kujiita Muhammad. Hiyo ilitosha kwa Masheikh kumkumbatia huku wakinukuu Aya na Hadithi juu ya fadhila za kumkirimu mgeni, na hasa mtu kama yeye aliyetoka katika Ukafiri na kusilimu. Hawakuingiwa na wasiwasi wowote kabisa kuwa anaweza kuwa ni adui aliyejifanya kusilimu. Akakaribishwa hadi chumbani kwa Sheikh aliyemtaja kwa jina la Sheikh Ahmed Efendi na akapewa nyumba ya

Udukuzi unakiuka katiba ya Marekani


Jaji wa mahakama katika jimbo moja nchini Marekani Jaji Richard Leon, amesema kuwa tabia ya shirika la ujasusi la Marekani NSA, kukusanya data kwenye simu za watu binafsi ni kinyume na katiba ya nchi hiyo. Jaji Leon alisema kuwa tabia hiyo inaingilia uhuru wa taarifa za faragha za watu na kuwa haistahili na kwamba hivi sasa wamarekani hawaishi kwa amani kwani simu zao zote zinadukuliwa. Mmoja wa watu waliolishitaki shirika hilo kwa kufanya udukuzi wa simu za mkononi za watu na kukusanya data nyingi ya watu binafasi, Lary Klayman, amesema kuwa shirika hilo sharti lijue kuwa linakwenda kinyume na sheria. Larry Klayman, aliongea na BBC baada ya Jaji Richard Leon, kuamua kuwa udukuzi wa simu unaofanywa na Shirika hilo la Ujasusi la Marekani unakiuka katiba ya nchi, kwa kukusanya taarifa kwa njia isiyofaa. Baadhi ya taarifa ambazo hukusanywa na shirika hilo ni namba za simu za watu, nyakati walizopiga simu na tarehe walizopiga simu zao. Sakata kuhusu tabia ya serikali ya Marekani kufanyia simu za watu udukuzi, lilifichuliwa na kachero mtoro wa NSA Edward Snowdon, katika juhudi zao za kutafuta taarifa za kijasusi. Jaji Leon alitoa agizo la muda la kuzuia shirika hilo kuendeleza udukuzi ingawa anasuburi serikali kukata rufaa. Ikulu ya White House ilipuuza pendelezo la kupewa msamaha Bw. Snowden ambaye alikimbilia nchini Urusi baada ya kufichua taarifa hizo, ili aweze kuacha kuendelea kufichua taarifa hizo.

Habari za Kimataifa

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

RAIS Rohan wa Iran.

RAIS Obama wa Marekani.

Waasi Sudan Kusini wadhibiti mji wa Bor


JUBA Jeshi la Sudan Kusini limesema haliudhibiti tena mji muhimu wa Bor, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza kwa jeshi hilo kukiri kushindwa katika mapigano yanayoendelea kwa siku ya kadhaa sasa kati ya makundi ya Wanajeshi yanayopingana. Mapigano hayo makali kati ya pande mbili za Rais Salva Kiir na yale yanayomuunga mkono aliyekuwa Makamu wake aliyefukuzwa serikalini, Riek Machar, yanatishia kuitumbukiza nchi hiyo kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Msemaji wa Jeshi la Sudan Kusini, Kanali Philip Aguer, alinukuliwa akisema wiki iliyopita kuwa wanajeshi waasi wanaomtii aliyekuwa makamu wa Rais wa nchi hiyo Riek Machar, wameutwaa mji wa Bor. Amesema viongozi katika mji huo ambao ni mji mkuu wa jimbo la Jonglei, hivi sasa hawapokei simu zao, hatua inayoifanya serikali kuu kuamini kwamba wamejiunga na waasi. Kanali Aguer amesema wamepoteza udhibiti wa mji wa Bor na kwamba

Vikosi UN kupelekwa kulinda usalama


milio ya risasi imesikika usiku kucha, ingawa bado hawana taarifa kuhusu waathirika au watu walioyakimbia makazi yao kwa kuwa operesheni za kijeshi bado zinaendelea. Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Martin Nesirky alisema raia 19 wameuawa katika mji wa Bor, kwa mujibu wa taarifa zimetolewa na shirika la Msalaba Mwekundu nchini Sudan Kusini. Amesema wasiwasi pia umeongezeka katika majimbo ya Unity na Upper Nile na mji wa Torit huku mapigano yakisambaa katika miji mingine ya taifa hilo tajiri kwa mafuta. Waziri wa Habari wa Sudan Kusini, Michael Makuei Lueth, amesema kiasi watu 500, wengi wao wakiwa wanajeshi, wameuawa na wengine 700 wamejeruhiwa katika mapigano hayo yaliyoanza katika jaribio la mapinduzi mwishoni mwa wiki iliyopita. Rais Salva Kiir, amesema yuko tayari kuanza mazungumzo na Makamu wake aliyemfukuza kazi mwezi Julai, Riek Machar. Kiir anamlaumu Machar kuhusika na jaribio la mapinduzi lililoshindwa na kuanzisha mapigano. Hata hivyo Machar amekanusha madai

UN yatakiwa ifuatilie silaha za nyuklia za Israel


NEW YORK Mwakilishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa Bw. Bashar Jaafari, amesema kuwa baada ya kufungwa faili la silaha za kemikali za nchi hiyo, Umoja wa Mataifa sasa unapasa kuanza kushughulikia kikamilifu silaha za nyuklia na zile za vijidudu zinazomilikiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel. Akizungumza Jumatatu wiki hii wakati wa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York, kinachojadili matukio ya Mashariki ya Kati hasa mgogoro wa Syria, Bw. Jaafari alisema kuwa, Syria ilikubali kuwa mwanachama wa Taasisi ya Kuzuia na Kusambazwa Silaha za Kemikali na iliandaa mazingira ya kutokomezwa silaha zake zote za kemikali kwa kushirikiana na wakaguzi wa Umoja wa Mataifa. Bw. Jaafari aliongeza kuwa, iwapo Umoja wa Mataifa unataka amani ya kudumu ipatikane katika eneo la Mashariki ya Kati, unapaswa kuanza kuchukua hatua za kutokomezwa silaha za kemikali na zile za nyuklia zinazomilikiwa na utawala wa Israel. Mwakilishi huyo wa S yria kat ik a Um oja wa Mataifa aliongeza kuwa, kuna migogoro mingi iliyotokea katika eneo la Mashariki ya Kati imesababishwa na taarifa za uwongo na kusisitiza kwamba, mashambulio ya Marekani dhidi ya nchi za Iraq na Afghanistan ni mifano miwili inayothibitisha ukweli huo.

hayo. Wakati huo huo mawaziri wa mambo ya nje kutoka mataifa manne ya Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Mashariki na Pembe ya Afrika-IGAD, wameelekea Sudan Kusini kuanza juhudi za kumaliza mapigano hayo yanayozusha hofu ya kugeuka kuwa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mawaziri hao wanatokea Kenya, Djibouti, Ethiopia na Uganda. Kwa upande wake, Marekani imeelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu mapigano ya Sudan Kusini, huku Waziri wake wa mambo ya nje, John Kerry akitoa wito wa kuwepo utulivu. Marekani na Uingereza zimeanza kuwaondoa wafanyakazi wake kutoka Juba. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon mapema wiki hii aliitisha mkutano wa Baraza la Uslama UN kujadili hali ya Sudan Kusini na imeazimiwa kupelekwa majeshi ya kusimamia usalama nchini humo. Maelfu ya raia wa Sudan Kusini wameyakimbia makazi yao na kwenda kutafuta hifadhi kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa tangu yalipozuka mapigano siku ya Jumapili.

6
Na Omar Msangi BADO yanazidi kufichuka mambo ya kutisha katika kile walichofanyiwa Waislamu wa Kilindi kiasi miezi miwili iliyopita. Kwa hakika ni mambo ya kusikitisha na kuhuzunisha ambayo hayakutarajiwa kufanyiwa mwananchi katika nchi yake huru. Ni wazi kuwa kila mwenye chembe ya imani, utu na ubinadamu, atalaani vitendo kama hivyo vinavyodaiwa kufanywa na walinzi wa usalama wa raiya na mali zao. Inavyofahamika, hata kama ni jambazi, hukamatwa na kufikishwa mahakamani akashitakiwa huku haki zake zote za kibinadamu zikizingatiwa. Lakini yaliyojiri Kilindi, ni hadithi nyingine kabisa. Watu wamepigwa r i s a s i , m a l i zimeharibiwa, nyumba zimechomwa moto na mali kuporwa. Kwa sasa hakuna la ziada la kusema ila kuungana na watu wote wema kulani ukatili huo. Kwa tuhuma zozote zitakazo kuwa, hakuna namna ya kuhalalisha mambo waliyofanyiwa watu wa Madina na vijiji vingine vya Kilindi. Baada ya utangulizi huo, niseme kuwa inabidi kila wakati kuwa makini tusiunganishe mambo tukashindwa kuyaelewa kila moja kwa muktadha wake. Kwa mfano, mtu akipinga uingiliaji kati wa nchi za Marekani na NATO katika mgogoro wa Syria, haina maana kuwa anaunga mkono udikiteta na utawala mbaya anaodaiwa kuwa nao Bashar al Assad. Na ndio hivyo hivyo, kupinga baadhi ya Waislamu kujitenga na kuanzisha vijiji vya kwao pekee wakidai kusimamisha utawala wa Kiislamu ndani ya nchi, haina maana kuunga mkono ukatili, mauwaji na udhalimu unaodaiwa kufanywa na polisi walipovamia baadhi ya vijiji hivyo. Ni kweli Saddam Hussein alikuwa dikiteta kama ambavyo inaweza kudaiwa kuwa alikuwa Muammar Gadhafi na sasa Bashar al Assad. Swa l i ni j e, mtindo uliotumika kumngoa Saddam, umeleta nafuu yoyote kwa watu wa Iraq? Hilo ndio swali la kuhoji na kufanyia tathmini. W a p o w a t u katika Afghanistan

Makala

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014


wakidai kuwa wanamtoa dikiteta waliyemlani kuwa hana Uislamu na hataki Libya itawaliwe kwa Kitabu na Sunnah. Swali ni je, hivi sasa Libya kinachotawala ni Kitabu? Je, hivi sasa Libya kuna Ukhalifah? Hali ya usalama kwa raia nayo ikoje? U k i a n g a l i a Afghanistan, Iraq, Libya na hata kule Pakistan ambapo kunadaiwa kuna vita dhidi ya ugaidi, hakuna wananchi walichovuna ila umwagikaji damu, mauwaji ya mamia ya maelfu ya watu wasio na hatia. Na hata baada ya vita kumalizika, walichovuna na wanachoendelea kufaidi ni vita ya wenyewe kwa wenyewe (civil war). Ni vita ya kikabila na kati ya makundi ya mirengo tofauti ya kidini (Shia/Sunni). Hakuna salama tena. Hakuna salama kwa sababu mabeberu waliopanga vita ndio hatimaye walikusudia iwe hivyo. Yale madai ya huruma ya kibinadamu ilikuwa danganyatoto. Na kwa bahati mbaya wakapatikana Waislamu wakawaunga mkono wakidhani wakimpindua Saddam/ Gadhafi, watapata fursa ya kusimamisha Uislamu! Ni upumbafu huo huo unaojitokeza kwa suala la Syria hivi sasa. Isingekuwa Urusi na China kuweka Veto, hivi sasa Marekani na NATO zingekwishaingia Syria na kumngoa Bashar al Assad kama zilivyofanya Libya. Swali ni je, Marekani na NATO wanafanya hivyo ili kutoa fursa kwa Mujahidina kusimamisha Uislamu? Wanaojiita Al-Nusra Front na Jeshi la Uislamu (the Army of Islam), wanapigana Syria kupambana na jeshi la serikali wakiamini kuwa wapo katika Jihad na akingoka Bashar al Assad watasimaisha Khilafah. Wiki iliyopita wanajihad hao walifanya mauwaji ya kutisha katika mji wa Andra ulio kiasi cha kilometa 20 kasikazini mwa Damascus. Baadhi ya taarifa zinasema kuwa zaidi ya watu 80 waliuliwa wakati wapiganaji hao walipoteka mji huo. Walichofanya ni kuuwa kila aliye wa kabila ya Bashar (Alawites), Shia, Druze na kila anayeonekana kumuunga mkono Rais Inaendelea Uk. 7

AN-NUUR

Ni kweli dhulma kubwa wamefanyiwa Madinah


walichekelea kungolewa Taliban. Picha za video zikawaonyesha baadhi ya Waislamu wa Afghanistan (hasa wa madhehebu ya Shia na Waislamu

Ila Elimu kwanza sio kutoa vijana shule Tutaumwa mara ngapi ndio tujifunze?
wasiokuwa wakitaka nchi hiyo itawaliwe Kiislamu) wakipiga mateke maiti za askari wa Taliban waliouliwa na makombora ya Marekani.

Tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya Uislamu?


MIEZI michache iliyopita vyombo vya habari vilisheheni taarifa ya magaidi waliokuwa katika vijiji vya Handeni. Taarifa zilifika Tanga kuwa kulikuwa na magaidi wanaishi katika mahandaki na operesheni maalum ilikuwa ikifanyika kuwateketeza. P r o p a g a n d a ikaenezwa kuwa walikuwa hawaitambui serikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Habari zilivuja Tanga mjini na vitongoji vyake kuwa kuna vijiji vimeteketezwa. Kwa hakika kuna watu waliletwa Hospitali ya Bombo wakiwa na majeraha ya risasi.

Lakini hali ikoje leo? Wapo pia waliochekelea kupigwa Saddam na wengine wakashika silaha kushirikiana na NATO Kumngoa Gadhafi. Wenyewe

Kwa watu waliofika Hospitali ya Bombo kwa kweli waliwaona vijana waliokuwa wamefungwa pingu wakiwa katika vitanda vyao huku wakilindwa na askari. Taarifa zikafika vilevile kuwa kuna watoto wadogo wamefikishwa Tanga baada ya kukutwa porini. Watoto hawa walikuwa wamehifadhiwa katika moja ya shule za hapo mjini. Katika hali kama hiyo, vilevile zikafika taarifa tofauti kwa Waislamu wa Tanga kuwa hao walioletwa Hospitali ya Bombo na watoto waliookotwa porini, ni Waislam wa vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande walioshambuliwa na askari pasi na sababu. Juhudi za Umoja wa Taasisi za Kiislamu Tanga (SHITA) chini ya Mayor Omari Guledi na Katibu wake Ahmed Mustafa kukutana na Mkuu wa Mkoa Chiku Galawa kupata ukweli zikagonga mwamba. Hali ikawa tete baada ya Sheikh Rajab Ramadhani Chambuso mmoja katika masheikh vijana mjini Tanga kukamatwa na kuwekwa rumande kisha kuhamishwa Handeni ambako alifunguliwa kesi ya ''kushawishi mauaji.'' Ikavuma kuwa Inaendelea Uk. 7

7
Inatoka Uk. 6 Bashar. Hivi sasa mamilioni ya raia wasio na hatia wanataabika katika kambi za wakimbizi wakiwa hawana msaada wa kutosha katika majira haya ya baridi kali. Yamewafika masaibu haya kutokana na vita ya wapinzani wanaodai kupigana Jihad kumngoa Bashar al Assad. L a m u h i m u kufahamika hapa ni kuwa, hawa Al Nusra, hawakuanza katika mgogoro huu wa Syria. Na hawa al-Nusra Front, al Qaidah, Jeshi la Kiislamu (Iraq) na Lashkar-e-Taiba (LeT) katika Pakistan, ni makundi ya Kiislamu yanayofadhiliwa na baadhi ya nchi za Kiarabu na ndio yanayotumika kutafuta visingizio vya kupigwa Waislamu yakidaiwa kuwa ni ya kigaidi. Lakini inapokuja kusaidia kumpiga na kumtoa mtu asiyetakiwa na Marekani kama Bashar, hawa hugeuka kuwa maswahiba wakawa wanapewa silaha na mafunzo kutoka Marekani na NATO kupitia nchi za Kiarabu. Maji yamekuwa marefu kwa Free Syrian Army. Kama ilivyokuwa kwa Afghanistan, sasa inaonekana wanaoweza kupambana na jeshi la Bashar ni Waislamu walioaminishwa kuwa wanapigana Jihad. Hapa ndio wanaingia hawa Al-Nusra Front na wenzao. Kupitia kwa Saudi Arabia/Qatar, sasa hawa ndio watakuwa wakipata misaada ya silaha, fedha na kuungwa mkono kidiplomasia. Mapema mwaka 2010 mtandao wa WikiLeaks, ulifichua mawasiliano ya siri ya tarehe 30 Desemba 2009 ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton kwa mabalozi wake (US embassies) akisema kuwa Saudi Arabia imekuwa ndiye mfadhili mkubwa wa makundi ya Jihad ya Kisuni ambayo kwa msamiati wa Kimarekani, ni magaidi. Makundi hayo ni pamoja na Al-Nusra, na ndiyo yanayotumiwa kupigana Syria hivi leo. Wapo watu ndani ya AlNusra (hasa wale walio katika mawasiliano ya moja kwa moja na Prince Bandar Ben Sultan a.k.a. Bandar Bush) wanaweza wakajua

Makala

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

Ni kweli dhulma kubwa wamefanyiwa Madinah


mchezo unaofanyika. Lakini pia wapo vijana wengi wasio na hatia, ambao wataingia Syria wakidhani wanapigana Jihad ya kweli! Wana uchungu kama anavyodhihirisha msomaji aliyenitumia ujumbe wa simu akilaani watu wanaowakatisha tamaa na kuwavunja nguvu Mujahidina. Hawa ndio mwandishi mmoja anawasifia akisema wameigeuza Syria kuwa machinjio ya brainwashed, triggerhappy Jihadi fighters eager to meet their maker. A k i m a a n i s h a machinjio ya vijana waliopumbazwa wakadhani wanapigana Jihad na katika kufanya hivyo, watakutana na Mola wao wakiwa Mashaheed. Anaongeza akisema kuwa kwa kupumbazwa na kufanya hivyo wanauwa maelfu ya watu wasio na hatia. B a a d a y a k uelez a ukweli na kufichua uhusiano uliopo baina ya makundi haya ya Jihad, baadhi ya nchi za Kiarabu na Marekani, mwandishi amewaita wapiganaji hawa kuwa ni fanatic groups ambao maadhali wanapata misaada ya fedha, silaha, logistical support, unprecedented diplomatic clout and ideological guidance, wataendelea kuisumbua na kuiangamiza Syria kufanikisha lengo la mabeberu. (Soma: Prince Bandars Reign of Terror By Ahmad Barqawi, November 27, 2013) Hoja ya msingi hapa sio kukubali au kukataa Jihad. Kupinga ushirika

Tunapiga vita ugaidi au ni vita dhidi ya Uislamu?


Inatoka Uk. 6 Tanga na habari za kutisha kuhusu dhulma iliyopita katika vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande. Habari hizi alielezwa na mahabusi wenzake katika hivyo vijiji vilivyoshambuliwa. Sheikh Chambuso katika hotuba aliyotoa katika moja ya misikiti maarufu

p a t a k u w a n a m a a n d a m a n o kushinikiza kuachiwa kwa Sheikh Chambuso. Askari wa FFU walizingira misikiti kadhaa Ijumaa hiyo, lakini hapakuwa na maadamano yoyote. Alipopata dhamana na kuachiwa Sheikh Chambuso alikuja

Tanga, aliwafahamisha Waislamu kuhusu misikiti iliyovujwa na kuchomwa moto, Qur'an zilizochomwa moto na nyumba za Waislamu z iliz o t e ke t e z wa kwa kisingizio cha ugaidi. Wananchi jioneeni wenyewe yote hayo katika hizi picha. (Maelezo ya msomaji An nuur)

wa Marekani na Jeshi la Kiislamu, haina maana kumuunga mkono Assad na ubaya wote anaodaiwa kuwa nao. Hoja ni kukataa k u t u m i w a . Kupumbazwa ukadhani unapigana Jihad, kumbe unatumiwa. Unapigana huku anayekupa msaada anapanga namna ya kukuangamiza baada ya kumaliza kazi aliyokutuma bila kutambua. Ujinga huu ndio inapasa Waislamu waepukane nao. Madina Madina ni kijiji kilichoanzishwa miaka ya 1990s, waanzilishi wakidai kuwa kwa kujitenga na kuishi hapo wataweza kusimamisha Shariah ndani ya nchi inayodaiwa haina dini! Walijenga na wakajishughulisha na kilimo na biashara mbalimbali. Pamoja na waanzilishi, baadae walipatikana pia watu wa kuhamia. Hata hivyo, baadae baadhi waliamua kuhama baada ya kuingia sera ya kutaka watu watoe watoto wao shule ikidaiwa kuwa kupeleka watoto shule ni ukafiri. Wapo waliohama baada ya kushindwa kukubaliana na sera hiyo na wapo waliobaki, lakini watoto wao wakaendelea kusoma. Lakini wapo pia ambao walitoa watoto wao shule. Hivi karibuni kuna vijana waliacha shule, wengine wakiwa kidato cha sita na baadhi wakiwa vyuo vikuu. Hawa inaaminika kuwa baada ya kuacha masomo, walikwenda Madina na kuanza maisha huko. Walitoweka katika mazingira ya kutatanisha, baadae ikafahamika kuwa wapo Madina. Baadhi ya vijana hawa walitoka katika shule za vipaji maalum kwa maana kuwa walikuwa vijana wenye akili nzuri na kwa hivyo tarajio la ummah wa Kiislamu na nchi kwa ujumla. Wapo pia baadhi ambao walikuwa wakimalizia masomo yao ya udakitari (medicine) katika moja ya vyuo vikuu nchini. Wanajulikana kwa majina na wala sio habari za amini ukipenda. Swali hapa ni je, ukirejea ile amri ya kwanza kwa Mtume (s.a.w) ya Iqra, inakubalika kuwazuiya Inaendelea Uk. 8

8
Inatoka Uk. 7 watoto kusoma? Inakubalika katika Uislamu kumtoa kijana aliye kidato cha sita au Chuo Kikuu ili aende Madina kwa kumlaghai kuwa hayo ni maandalizi ya kusimamisha Shariah? Katika jumla ya malalamiko ya Waislamu nchini ni kuwa wamebaguliwa katika elimu na ajira. Je, mtu ambaye leo katika karne hii ya 21 ya sayansi, tekinolijia, IT na utandawazi, anampumbaza kijana wa kidato cha sita/chuo kikuu na kumtoa katika masomo kwa madai kuwa huo ni ukafiri, ni kupoteza muda, bali akajitenge katika kijiji cha pekee kungoja Jihad, utasema huo ndio Uislamu? Au ndio namna ya kusimamisha Uislamu? Ieleweke vizuri hapa kuwa hoja sio kukubali au kupinga Jihad. Wala sio kuunga mkono au kupinga kusimamisha Khilafah. Hoja ya msingi hapa ni njia ya kupita. Kama ilivyokuwa Rwanda, kule Bangui, Afrika ya Kati, chuki imetumbukizwa baina ya Waislamu na Wakristo, sasa wanachinjana kijiji kwa kijiji. Seleka haijaanzishwa kama kikundi cha kupigania Uislamu, wala hawana mpango kabisa na kusimamisha Shariah! Mabeberu wamepata mwanya wa kuleta majeshi yao kwa kisingizio cha kulinda amani. Wakati wananchi wakiuwana, mabeberu wanavuna dhahabu, almasi na uranium. Imekuwa Congo (DCR) nyingine. Hebu natupate fundisho kama ni wenye akili. Katika nchi zote ambazo mabeberu wanatamani kuzikalia hivi sasa katika mtindo mpya wa ukoloni, uchochoro wao muhimu wa kupita, ni kupandikiza machafuko. Mahali pasipo na ugaidi, watapiga sana propaganda kuwa kuna magaidi huku wakitumia vyombo vya habari mpaka ikubalike ili wapate fursa ya kusema wanaingiza FBI wao na Marine wao na drone zao kusaidia kupambana na magaidi. Wakishaingia hawatoki. Na kwa upande mwingine, ukishapandikizwa huo ugaidi, ujue hautakwisha. Kila siku itakuwa watu ni kulipuana tu. Ndio hali ilivyo Yemen, Pakistan,

Makala

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014


ukatili na mauwaji yanayodaiwa kufanywa wakati ilipofanyika operesheni katika vijiji hivyo. Hata kama kuna jambo ovu lililokuwa limefanyika katika vijiji hivyo, lakini hiyo haihalalishi kutoa adhabu ya jumla ambapo watu walipigwa, kuporwa mali, nyumba na mali kuchomwa moto. Kutambua udhaifu ndio umadhubuti wa mtu Katika mambo yanayomfanya mtu kuwa madhubuti na kupiga hatua katika maendeleo, ni kutambua na kukubali madhaifu yake. Kujua mapungufu aliyonayo na kujitahidi kuyaondoa. Ukifumbia macho makosa na madhaifu yako, ni wazi hutaenda popote. Ni pale mtu anabakia kuwalaumu wengine, kumbe tatizo ni yeye mwenyewe. Sasa katika hili ni lazima tukubali kuwa kuna upumbafu umeingia miongoni mwetu Waislamu. Kutoa watoto shule si katika kupigania dini, bali ni kuungamiza ummah wa Kiislamu. Kuendesha darsa za kuwahimiza vijana kujichimbia mahali ili kwenda Somalia/Syria au Madina kwa lengo la kujiandaa kwa namna yoyote kuleta yale yanayotokea Bangui, ni Inaendelea Uk. 10

AN-NUUR

Ni kweli dhulma kubwa wamefanyiwa Madinah

SHEIKH Rajab Chambuso (katikati). Afghanistan, Iraq, Somalia, Libya na sasa Kenya nayo inaelekea huko huko. Westgate Mall Shopping Centre attack na maguruneti, hayatakoma. Hivi hatukumbuki ile kampeni yao ya kudai kila wakati kuwa Afrika Mashariki kuna kitisho cha kushambuliwa na magaidi wakionya watu wao wasitembelee miji ya nchi hizo? Tumesahau yale madai kuwa mtoto wa shule ya msingi aliingia katika moja ya balozi zao na kigeleni cha mafuta ya taa akitaka kufanya ugaidi? W a l e v i j a n a waliokatisha masomo yao wakiwa kidato cha sita, hawakufanya hivyo ila baada ya kuhudhuria darsa zinazoendeshwa na watu ambao unaweza kusema kuwa hawa ni mawakala wanaotumiwa k u p a n d i k i z a vurugu/ugaidi. Wanachoaminishwa vijana hao ni kuwa kusoma ni kupoteza muda bure. Muhimu kwao ni kwenda kupigana/kupambana na makafiri. Kwa hiyo, wao huacha shule kwa imani thabiti kuwa wanalofanya ni jambo la dini. Lakini mwisho wa yote ni kutumiwa kuleta vurugu itakayoangamiza Uislamu wenyewe na nchi. Zipo taarifa za uhakika kuwa walipoingia vijana hawa Madina kati ya mwezi wa sita na saba mwaka huu, biashara ya mayai ya kuku wa kienyeji ilikuwa kubwa sana. Wenyeji walikuwa hawana uwezo wa kupata kifungua kinywa kwa mayai. Lakini kuingia wao, ikawa hakuna yai linalotagwa ila, limepata mnunuzi. Hawa ni vijana waliokuwa shuleni na vyuoni wakisoma kwa mkopo wa serikali na kwa kutumiwa pesa za matumizi na wazazi wao. Na wazazi wao wanajulikana uwezo wao wa kiuchumi. Huu uwezo wa kwenda kuishi na kujitegemea huko Madina, waliupata wapi? Hata hivyo, pamoja na kuhoji mambo haya, kama nilivyosema awali, sote kwa pamoja kwa hakika tunapaswa kulani kwa nguvu zote

Mahitaji ya Vifaa yanayohitajika kufikia hatua ya Zege la Jamvi PLOT No. 152 Block A, Masjid Jumuiyatil Islamia Ubungo Darajani.
Na Mahitaji 1 2 3 4 5 6 7 8 9 Nondo 12 MM Nondo 8 MM Binding Wire 20 MAWE 200 CM KOKOTO 70 CM Mchanga 40 CM Cement Mbao Cypruss Misumari JUMLA NDOGO Deni la Mkandarasi (mjenzi) JUMLA KUU 35,657,000.00 Nb: haya ni Mahitaji kwa ajili ya Zege la Jamvi Kwa mawasiliano zaidi Tupigie Mwenyekiti 0754 462 050 Katibu 0719 760 777 Mwenyekiti Kamati ndogo ya ujenzi ( Goha) 0787 318 116. International Commercial Bank No A/c 00001/01/601059/01 au A/c 0000/01/ 0009/94/02. Au tutembelee katika Msikiti wetu uliopo Ubungo Darajani. Wabillah Taufiq Size Pcs Pcs Kg Lori Lori Lori Mifuko 16 Kg Idadi 120 60 1 20 7 4 350 120 10 @ 18,000 8000 52000 250000 750000 13500 9000 3000 Tshs 2,160,000.00 480,000.00 52,000.00 5,000,000.00 5,250,000.00 4,725,000.00 1,080,000.00 30,000.00 19,657,000.00

Msaada ujenzi wa Msikiti

220,000 880,000.00

Kwa nini tunamkumbuka Mandela?


wale ambao alipata kuwatangazia adhabu ya kifo kabla ya hapo. Mfano mzuri aliouonyesha mzee Nelson Mandela, baada ya kuwa huru na Rais mwenye madaraka na mamlaka kamili ya dola, ni kusamehe na kusafisha nafsi yake isiwe na doa la chuki, hasira na kutaka kulipa kisasi kwa wale ambao walikuwa ni mahasimu wake waliomfunga na kumtesa jela kwa takriban miongo mitatu. Mzee Mandela alifikia hivyo, kwa sababu yeye hakutaka Afrika ya Kusini ijitawale ili hatimaye yeye mwenyewe ndiye awe mtawala. Alifanya kazi ya kudai uhuru kwa miaka mingi na akateseka gerezani kwa miaka mingi, lakini akaishi madarakani kwa miaka michache mno na akawaachia wana wengine wa Afrika ya Kusini kuendesha hatamu za uongozi wa nchi yao. Hilo lilitokea kwa sababu Mzee Madiba hakuingia madarakani kupitia kampeni za chama chake, kwa kumpindua mtu na wala si kwa kile kinachojulikana leo nguvu ya umma. Mandela ambaye alikuwa akijiamini na muumini wa kile alichokipigania na ambaye hakukubaliana na mtu yeyote kumchagulia rafiki au adui, lengo kuu la harakati zake lilikuwa ni kuwakomboa ndugu zake wa Afrika ya Kusini wote, kutokana na dhulma ya ubaguzi na utumwa. Mandela kwa umri wake wote alioishi katika sayari hii Dunia, hatukupata kusikia kwamba alipata kushiriki katika ubaguzi wa kidini katika nchi yake. Na hiyo ndio sababu iliyowafanya Waislamu wa Afrika ya Kusini kumpenda sana Mzee Mandela na kumpa sifa nzuri zinazomstahiki. Tukitaka kulinganisha baina ya uongozi wa Mzee Mandela na viongozi wengine wa Dunia, tutaona kwamba ipo tofauti kubwa. Kwani hali hii tuliyo nayo leo duniani, hali ya ukosefu wa amani, vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyotapakaa kila pembe ya Dunia, sababu yake kuu ni viongozi wabaya, waroho wa madaraka waliopo hapa duniani. Wao hao ndio wanaoshinikiza na kupalilia chuki za kidini baina ya raia wao, vita vya kimadhehebu na wao ndio wanaoshabikia kumdhalilisha mwanaadamu kwa kutaka kumnyanganya ustaarabu wake wa asili na badala yake kumletea ustaarabu wanao utaka wao, kwa matakwa na matashi yao. Miongoni mwa hayo ni kampeni wanayoifanya ili watu wote waikubali ndoa ya jinsia moja, jambo ambalo halikubaliwi na dini zote za mbinguni, si Uislamu, Ukristo wala Uyahudi. Mzee Mandela kwa umri wake wa miaka 95 aliyojaaliwa kuishi hapa duniani, tunaona kwamba ni mtu aliyebahatika sana, ukilinganisha na maisha ya viongozi wen g in e wa k isia sa walioishi katika karne yake. Aliyepata kuwa

Makala

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

Na Sheikh Abdallah Bawazir NDIO utaratibu wetu sisi waumini wa dini iliyoletwa hapa duniani na Mtume Muhammad (s.a.w.), kumtanguliza kiongozi wetu kila tunapotaka kutaja tabia njema au mtu yeyote mwenye tabia njema. Kwa sababu hivyo ndivyo tulivyofundishwa na Mola wetu na aidha yeye Mtume Muhammad (s.a.w.), ndiye mkamilifu wa tabia njema. Hayo ndio mafundisho yetu katika Uislamu wala hayahitaji mjadala. Hata hivyo, sio ajabu kumpata mtu na wala mtu huyo si Muislamu kamwe, lakini akawa ana tabia fulani njema na nzuri kinyume cha Muislamu mwenyewe ambaye ilikuwa ni wajibu wake kuwa na tabia hizo, kwa kuwa ndio mafundisho ya dini yake. Kusamehe ni tabia mashuhuri ya Bwana Mtume Muhammad (s.a.w.), hasa pale anapokuwa na uwezo na amri ya kuweza kumuadhibu a n a y e s t a h i k i kuadhibiwa. Mfano hai wa hilo katika maisha yake, unapatikana katika kipindi alipoiteka Makka pasina umwagaji wa damu na kuwa chini ya himaya ya dola yake kikamilifu. Aliwasamehe watu waliomkosea hata

MZEE Nelson Mandela. Rais wa Misri Gamal Abde Nasser, yeye pia alizaliwa mwaka huo huo wa 1918 mwaka aliozaliwa Mandela. Lakini Gamal alifariki mapema mwaka 1970 akiwa na umri wa miaka 52 tu. Baadhi ya viongozi waliobahatika kuupata umri wa Mzee Madiba au karibu yake ni Habib Buurqiba 1903 2000 wa Tunisia, Aden Osman 1908 wa Somalia, Dakta Azikiwe 1904 1996 wa Nigeria na Ahmed Ben Bella wa Algeria 1916 2012. Aidha Mzee Mandela amebahatika kufariki Dunia katika hali hii, akiwa bado anapendwa na kuheshimiwa na watu, bila ya kupata mitihani na misukosuko katika kipindi chake kifupi cha uraisi mpaka anajiuzulu mwenyewe kwa ridhaa yake. Bahati kama hii wameikosa wengi miongoni mwa viongozi wa kisiasa wa Bara letu la Afrika na badala yake, walikufa katika hali mbaya na ya dhuluma. Miongoni mwao ni Ahmed Ben Bella wa Algeria, Patrice Lumumba wa Congo au Alhaji Aboubakar Tafawa Balewa, katika dhuluma isiyosahaulika iliyomkuta mwaka 1966 huko Nigeria. Mfano mwingine wa karibu ni dhuluma aliyofanyiwa Dkt. Mohammed Mursi wa Misri, kwa kunyanganywa Serikali kihuni baada ya kushika madaraka kwa mwaka mmoja tu. Sheikh Abdallah Ahmad Bawazir +255 767 215 898

Inatoka Uk. 12

Mwakilishi apendekeza liwati wanyongwe


wa t o t o , m wa k i l i s h i huyo alisema, adhabu kunyongwa ikiambatana na viboko 50, ndio itakayomaliza tatizo la vitendo vya udhalilishaji watoto Zanzibar. Aidha Bw. Hamad alipendekeza adhabu ya kifungo cha miaka kumi jela kwa wazazi watakaobainika kuficha vitendo vya ubakaji watoto, kwa kuhofia

mdogo. Mwakilishi wa jimbo la Wete, Asaa Othman, alisema ingawa mataifa ya nje yataingilia kati sheria hiyo kwa madai ya haki za binadamu, lakini watu wanaofanya vitendo hivyo ndio wanavunja haki hizo. Akichangia hoja binafsi ya azimio la vitendo vya udhalishaji

jamaa zao kupelekwa k a t i k a v y o m b o v ya sheria. Hoja binafsi hiyo iliyowasilishwa mapema wiki hii na mwakilishi wa viti Maalum Mgeni Hassan Juma, inataka kuanzishwa sheria na mikakati itayosaidia kukomesha vitendo vya udhalishaji watoto vinavyongezeka Zanzibar.

10

Inatoka Uk. 4

Tuna safari ndefu Ni kweli dhulma kubwa wamefanyiwa Madinah


Ndio nikawa najenga hoja kuwa wapo vijana wanapotoshwa wakidhani wapo katika Jihad, lakini ukweli wanatoswa katika mambo ambayo mwishowe yatauangamiza Uislamu wenyewe. Katika kilele cha kilio cha Waislamu Tanzania kuwa wamedhulumiwa katika elimu, kijana umebahatika umefika hadi kidato cha sita au Chuo Kikuu, unaambiwa acha masomo nenda Madina kajiandae na Jihad!!! Unakubali! Hii akili gani? Nchi za Kiarabu ndio zilizotumiwa na Marekani kukusanya vijana kutoka nchi mbalimbali kwenda kupigana Afghanistan kumtoa Mrusi. Huo ukawa ndio mwanzo wa al-Qaidah. Baada ya vita kumalizika, nchi hizo hizo za Kiarabu zikaungana na Marekani na NATO kuwapiga na kuwaangamiza Mujahidina waliokuwa Afghanistan. Ambao walisalimika kutokana na carpet bombing ya B-52 Stratofortress, wakaishia Guantanamo na wengine bado wanasakwa kupitia visingizio mbalimbali, hukamatwa na kupelekwa Marekani ambapo hutasikia nchi ya Kiarabu wala nchi wanakotoka, wakisimama kuwatetea! Ni nchi hizo hizo, zilizotumika kukusanya na kuwasaidia wapiganaji walioshiriki katika kumtoa Gadhafi. Leo tena wanatumika kukusanya nguvu ya kupigana Syria! Kama somo la al Qaidah halikueleweka, tunaona kutahadharisha juu ya uwezekano wa kutumiwa na maadui wa Uislamu tukidhani tunapigania Dini, ni kuwakatisha tamaa na kuwadhoofisha Mujahidina, basi tutakuwa maadhura! Wala tusitarajie msaada wa Mwenyezi Mungu katika hali hii ya kufanya mambo kwa ujinga na mihemko. Nimalizie kwa zile siasa za Iran na Iraq. Wapo watu waliunga mkono Iraq wakidhani ku wa kin a ch op ig wa vita ni Ushia. Na zipo nchi pia za Kiarabu ziliungana na Iraq iliyokuwa ikisaidiwa na Marekani katika vita ya mwaka 1980 kati ya Iraq na Iran kwa siasa hizo za Urabu na Ufursi/Ushia na Usuni. Lakini Marekani yenyewe haikuwa na mpango wa kumsadia Saddam kushinda vita hiyo. Washington did not want either side to win. We wanted to avoid victory by both sides. Liliripoti gazeti la New York Times la Januari 26, 1992 likimnukuu msemaji mmoja katika utawala wa Rais Ronald Reagan. Akaliweka uzuri jambo hilo Henry Kissinger aliponukuliwa akisema: I hope they kill each other and too bad they both cant lose. (Shahram Chubinl and Charles Trip, Iran and Iraq at War (1988) U k i a n g a l i a propaganda inayopigwa juu ya madai kuwa kuna magaidi Tanzania na wanaonyoshewa kidole ni Waislamu. Haya ukiyaunganisha na chuki inayojengwa kati ya Waislamu na Wakristo ikidaiwa kuwa Waislamu wamepania kuchoma makanisa na kuuwa viongozi wa Kikristo; haitakuwa vigumu kuona kuwa kinachopandikizwa hapa ni chuki na vita ya wenyewe kwa wenyewe (civil war). Na Civil War, sio Jihad. Hii ndiyo hoja yangu. Civil war sio Jihad. Kinyume chake itakuwa ni kile alichosema Kissinger: I hope they kill each other. Syria hivi sasa wanauwana wenyewe kwa wenyewe. Mwisho wa yote ni kudhoofika na kuiacha Israel ikiwa imebaki na mtu mmoja tu wa kumhofia, Iran. Afrika ya Kati wanauwana Waislamu na Wakristo. Uislamu hautasimama katika nchi hiyo kupitia vita baina ya Slka na "Anti-balaka". Huo ndio ukweli. Inatoka Uk. 8 kuangamiza Uislamu na Waislamu. Pakistan ilianza kulipuliwa misikiti. Mara wa Shia, mara wa Sunni, huku propaganda inapigwa katika vyombo vya habari kuwa wahusika ni Sunni/ Shia. Msikiti wa Shia unalipuliwa waumini wanauliwa, vyombo vya habari vinadai kuwa waliohusika ni Al Qaidah/Talaban au magaidi wa Kisuni. Mara Shia nao wanadaiwa kufanya hivyo. Mitaani nako zinapigwa darsa kuwa Shia kafiri/Sunni kafiri!!! Matokeo yake Pakistan (nchi ya Kiislamu pekee ya kwanza kuwa na nyukilia) imegeuzwa kuwa kama mwanasesere. Haiwezi kukohoa tena mbele ya India. Imekuwa ni aibu kwa Waislamu wote duniani badala ya kuwa nchi ya kuwatoa kimasomaso Waislamu. Siasa zilizoanza kujitokeza hapa nchini katika miaka ya hivi karibuni, ni kupandikiza chuki/ mauwaji ya Waislamu na Wakristo. K w a upande mmoja inapigwa propaganda kuwa Waislamu ni magaidi waliokamia kuuwa Wakristo na kulipua makanisa. Kwa upande mwingine, Wakristo wanaaminishwa kuwa Waislamu ni maadui zao. Katika hali kama hiyo, ikipatikana sababu, unadhani hali itakuwaje? Bila shaka tulisoma katika magazeti, ilivyozungumzwa walipokamatwa wale v ija n a k u le M twa r a waliokuwa wakifanya mazoezi porini. Katika mazingira kama yale, akitokea mtu akatumika au kichaa tu kwa bahati mbaya, akalipua kanisa, hapana shaka yaweza kutosha kulipua mapigano ya Waislamu/ Wakristo. Mabeberu watakuwa pembeni wakichekelea. Huo utakuwa ndio mwanzo wa kuserereka kuingia katika tope ilipozama Congo (DRC). Lililo la muhimu na la kuzingatia hapa ni kuwa kama ilivyo Pakistan na Iraq, kwamba Uislamu hautasimama kwa mauwaji yanayotokea baina ya Sunni na Shia, hakuna pia Uislamu utakaosimama Tanzania kwa mauwaji ya Waislamu na Wakristo. Kinyume chake itakuwa ni Civil War (vita ya wenyewe kwa wenyewe). Vita ya panzi furaha ya kunguru. Civil War si Jihad. Kuna haja kwa wazazi wa Kiislamu katika kipindi hiki tete, kila mmoja kujua mtoto wake yupo wapi na anafanya nini. Si wakati wa kuamini kila mpita njia anayedai kuwa mwanaharakati. Wanaharakati wengine, ni mawakala na washenga wa ajali. Marekani ilipotaka kumngoa Mrusi Afghanistan, iliona watu wa kutumia ni Waislamu. Ukimuaminisha Muislamu kwamba anapigana Jihad, kazi itakuwa nyepesi. Nchi za Kiislamu zikatumika, hasa Saudi Arabia, kukusanya vijana kutoka nchi mbalimbali duniani, kutoa mafunzo, fedha na silaha kwa Mujahidina. Watu waliacha familia zao, biashara zao na kila chao kupigana Jihad (Allah ndiye Mjuzi atawalipa vipi kwa nia yao njema na jinsi walivyojitoa muhanga). Walifanya hivyo wakiamini kuwa, akiondoka kafiri Mrusi, wanasimamisha Kitabu na Sunna katika Afghanistan. Lakini walichokuwa hawajui ni kuwa wakati wao wanapigana, Marekani inayotumia nchi za Kiarabu kukusanya Mujahidina, nayo inapanga , vita ikiisha wanashughulika vipi na Mujahidina hao. Septemba 11 ikaja, Afghanistan ikavamiwa, maelfu kwa maelfu ya Waislamu wakaangamizwa na B-52 Stratofortres, mamia kwa maelfu wakateswa katika gereza la AbuGhraib na wengine hadi sasa wanateswa Guantanamo. Ambao hawakupatikana ndani ya Afghanistan, wakawa wanasakwa popote walipo. Makachero wa Marekani wanaingia katika nchi yoyote alipomtuhumiwa wao wanamkamata au wanaituma serikali husika wanamkamata na kumkabidhi kwa Marekani kuwashughulikia. Kenya walikamtwa sana, mpaka sasa wengine hawajulikani walipo. K w a w a l e wanaoshabikia kwenda kupigana Syria wakiaminishwa kuwa wanachopigania ni kusimamisha utawala wa Allah, je, wanaelewa nini wanapanga mabeberu dhidi yao baada ya kumaliza kazi ya kumngoa Bashar? Kama wanajua, wamejiandaa vipi kukabiliana nao? Haya ndiyo maswali ya kujiuliza. Wasije kushangaa kama alivyoshangaa Saddam Hussein akaambiwa, kumbe we mjinga sana. Saddam alishangaa inakuwa vipi Marekani inamgeuka wakati alikuwa swahiba mpaka akapewa silaha za sumu kuipiga Iran, Marekani nayo ikamshangaa kama alidhani kuwa Marekani inampenda na inamsaidia katika agenda zake. (Saddam) Hussein must have been too stupid to understand how the United States would react. Alijisemea Balozi April Glaspie akimshangaa Saddam Hussein kwa ujinga wake uliokithiri akadhani kuwa Marekani itamsaidia katika mipango yake ya kuingia Kuwait. Mpaka dakika ya mwisho kabla hajaingia Kuwait, Saddam aliaminishwa kuwa Marekani haitaingilia kati na kwa upande mwingine alioneshwa kuwa ana haki na kipande cha ardhi alichokuwa akipigania. Akatoswa. Ni hivyo hivyo, watakuwa wajinga sana ambao wanadhani Marekani, Ufaransa na Uingereza zitakuwa zinatoa misaada na kushinikiza Bashar angolewe madarakani ili hatimaye Jeshi la Kiislamu litawale Syria! Halikadhalika watakuwa wajinga sana wanaodhani kuwa hii propaganda ya kutia chuki baina ya Waislamu na Wakristo Tanzania kama ikiachwa na kuzaa mapambano ya wenyewe kwa wenyewe (Civil War), itakuwa sababu ya kuondoka dhulma na kusimama Uislamu Tanzania. Hakuna anayepinga madai ya Waislamu Tanzania. Wala hakuna anayepinga kuwa inahitajika juhudi kusimamisha Dini ya Allah. Suala ni je, haki za Waislamu zinapiganiwa vipi? Hoja ni Uislamu unasimamishwa vipi?

Makala

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

11

Inatoka Uk. 12 unaotumika kwenye mikutano ya nchi wanachama wa SAPCO. Amesema kutokana kushindwa kuwakamata wahalifu hao na kuibwa upanga huo, ipo haja ya kulifanyia mabadiliko zaidi jeshi hilo, badala ya kufanyiwa mabadiliko ya kamishna pekee. Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud, amesema kumetokea vitendo vingi vya uhalifu lakini jeshi hilo limeshindwa kuwakamata wahalifu husika. Amesema hali hiyo bado inaonesha kuwa jeshi hilo lina matatizo na kuunga mkono ushauri uliotolewa na Mwakilishi huyo wa kutaka jeshi hilo kufanyiwa mabadiliko ya uongoizi. Kuhusu wizi wa upanga wa dhahabu uliotokea mikononi mwa Jeshi la Polisi Zanzibar, Bw. Aboud alisema uchunguzi unaendelea

Wawakilishi wataka mabadiliko zaidi Jeshi la Polisi Zanzibar


huku nchi ya Bostwana, itakayokuwa Mwenyekiti wa mkutano wa SAPCO ikijitolea kutoa upanga mwengine bila malipo. Na Mwanishi Maalum, Zbar Awali Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, alilitaka Jeshi la polisi Zanzibar kutekeleza na kusimamia sheria za nchi, ili wananchi waendelee kuishi katika hali ya amani na usalama. Maalim Seif Sharif Hamad, alitoa rai hiyo wakati akizungumza na Kamishna mpya wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame, ofisini kwake Migombani Zanzibar. Katika mazungumzo yao, Maalim Seif alisema licha ya polisi kuwa na jukumu kubwa la kulinda usalama wa raia na mali zao, jeshi hilo pia linapaswa kuwa mstari wa mbele katika utekelezaji na usimamizi wa sheria. Alisema kuwa licha ya kuwepo sheria nzuri katika nchi, lakini kwa muda mrefu jeshi hilo limekuwa likisuasua katika utekelezaji wa sharia hizo hali inayosababisha kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria na vitendo vya uhalifu na ukiukwaji wa haki za binadamu. Hivyo akalitaka jeshi hilo kuondosha muhali katika kusimamia utekelezaji wa sheria, ili kuona kwamba sheria zilizotungwa zinafuatwa na kuleta ufanisi katika jeshi hilo na taifa kwa ujumla. Maalim Seif alisisitiza kuwa iwapo sheria zilizopo zitatekelezwa ipasavyo, jamii itaziheshimu na kuepukana na vitendo vya uvunjaji wa sharia hizo, na hatimaye kufikia malengo yaliyokusudiwa. Hata haya matuta yanayowekwa kila pahala barabarani sio dawa ya kuzuia ajali, lakini naamini alama za barabarani iwapo zitafuatwa pamoja na kudhibiti mwendo wa madereva, basi ajali nyingi zitaepukwa, alisema Maalim Seif. Aidha alilishauri Jeshi hilo kuimarisha uhusiano wake na raia wema, ili kusaidia kuwafichua wahalifu na watu wanaojihusisha na vitendo viovu, vikiwemo uingizaji na utumiaji wa dawa za kulevya. Alisema ofisi ya Kamishna huyo bado inakabiliwa na changamoto ya dawa za kulevya, hivyo kulitaka jeshi hilo kufanya juhudi za makusudi za kuondoa changamoto hiyo na kuahidi kuwa serikali itatoa kila ushirikiano kwa Kamishna huyo mpya, ili kuhakikisha kuwa anatekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Kwa upande wake, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame, amemuhakikishia Makamu wa Kwanza wa Rais kuwa atatekeleza majukumu yake ya kusimamia sheria, ili wananchi waendelee kuishi katika hali ya amani na usalama. Alisema jeshi la polisi kupitia kitengo chake cha uchunguzi litaimarisha utafiti, ili kupata taarifa za uhakika za kuweza kukabiliana na wahalifu na kuhakikisha usalama wa raia na mali zao. Kamishna Makame aliongeza kuwa, atatumia uzoefu alionao katika masuala ya teknolojia ya mawasiliano, ili kuona kuwa kitengo hicho kinafanya kazi kwa uhakika na kuleta ufanisi uliokusudiwa. Alisema mafanikio aliyoyapata katika kipindi cha miaka 30 ndani ya jeshi la polisi, yametokana na mashirikiano aliyopata kutoka kwa viongozi na wananchi na kuomba mashirikiano zaidi, ili aweze kufikia matumaini na matarajio ya taifa katika ulinzi wa raia na mali zao.

Habari/Tangazo

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

AN-NUUR

UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION ZANZIBAR

13

INTERNATIONAL UNIVERSITY OF AFRICA - KHARTOUM

TH

GRADUATION

The Principal of the University College of Education, Zanzibar (UCEZ), cordially invites all graduands of the academic year 2012/2013 to the 13th Graduation. The Ceremony will be held on Saturday 18th January 2014 at the University College premises. The Second Vice-President of Zanzibar HON. EMBASSADOR SEIF ALI IDD will be the Guest of Honour. All graduands are required to confirm their participation to the Academic Office not later than on Friday 10th January 2014. Graduands are reminded to pay Tzs. 10,000/= (non-refundable) before Thursday 16th January 2014 for graduation gowns. Please note that travel, meals and boarding expenses will be met by the graduands themselves. All graduands are requested to report at the College by 3:00 pm on Friday 17th January 2014 for rehearsal and logistical briefings. Graduands who will not participate in rehearsal will not be allowed to take part in the event. For more information contact the University College on the following address: The Academic Office, University College of Education Zanzibar P.O. Box: 1933 Zanzibar. Tel: +255242234102 Email: amacez@zitec.org Website. www. ucez.ac.tz Mobile: 0776-463405/ 0773-181786

12

AN-NUUR
MAKALA

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

12

SAFAR 1435, IJUMAA DESEMBA 27 , 2013-JAN. 2, 2014

Soma Gazeti la AN-NUUR kila Ijumaa

AN-NUUR

Wawakilishi wataka mabadiliko zaidi Jeshi la Polisi Zanzibar Mwakilishi


WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi wametaka Jeshi la Polisi Zanzibar lifanyiwe mabadiliko zaidi ya uongozi, kutokana na kushindwa kuwakamata wahalifu wa vitendo vya mauwaji, tindikali na walioiba upanga wa dhahabu ndani ya jeshi hilo. Mwakilishi wa jimbo la Chaani, Ussi Jecha, amesema jeshi la polisi Zanzibar limeshindwa kukabiliana na vitendo hivyo na kuitia doa Tanzania kwa kuibiwa upanga wa dhahabu Inaendelea Uk. 11

Maalim Seif akutana na Kamishna mpya apendekeza liwati wanyongwe


Na Mwandishi Wetu

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa pamoja na Kamishna mpya wa jeshi la polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame, baada ya mazungumzo yao ofisini kwake Migombani.

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imeshauriwa kutunga sheria itakayotoa adhabu ya kunyongwa hadi kufa, mtu atakayepatikana na h a t i a ya k u m b a k a au kumlawiti mtoto
Inaendelea Uk. 9

Hali ya Skuli ya Kengeja mbaya


Mimi ni Skuli ya Sekondari Kengeja. N i m e z a l i w a mnamo mwaka 1922. Nimetoa elimu kwa watu wengi sana wa Kengeja na maeneo jirani kama vile Mwambe, Kiwani, Kangani kwa kipindi cha

nyuma wakati wa kuanzishwa kwangu. K w a s a s a naendelea kutoa elimu bado, ingawa nimechoka sana kutokana na uchakavu wa majengo yangu.

Naomba msaada kwa Serikali na wasamaria wema kunifanyia alau ukarabati tu na ikiwezekana kujengwa upya niwe na sura mpya kama hii inayoonekana hapa chini.

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

También podría gustarte